< Luke 20 >

1 On one of those days, as he was teaching the people in the temple and preaching the Good News, the priests and Torah-Teachers came to him with the elders.
Siku moja, Yesu alipokuwa akifundisha watu Hekaluni na kuhubiri habari njema, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, pamoja na wazee wa watu wakamjia.
2 They asked him, “Tell us: by what authority do you do these things? Or who is giving you this authority?”
Wakamuuliza, “Tuambie, unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka haya?”
3 He answered them, “I also will ask you one question. Tell me:
Akawajibu, “Nami nitawauliza swali.
4 the baptism of John [Yah is gracious], was it from heaven, or from men?”
Je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”
5 They reasoned with themselves, saying, “If we say, ‘From heaven,’ he will say, ‘Why didn’t you believe him?’
Wakahojiana wao kwa wao wakisema, “Kama tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Mbona hamkumwamini?’
6 But if we say, ‘From men,’ all the people will stone us, for they are persuaded that John [Yah is gracious] was a prophet.”
Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ watu wote watatupiga mawe, kwa sababu wanaamini kwamba Yohana alikuwa nabii.”
7 They answered that they didn’t know where it was from.
Basi wakajibu, “Hatujui ulikotoka.”
8 Yeshua [Salvation] said to them, “Neither will I tell you by what authority I do these things.”
Yesu akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
9 He began to tell the people this parable. “A man planted a vineyard, and rented it out to some farmers, and went into another country for a long time.
Akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima fulani, kisha akasafiri kwa muda mrefu.
10 At the proper season, he sent a servant to the farmers to collect his share of the fruit of the vineyard. But the farmers beat him, and sent him away empty.
Wakati wa mavuno ulipofika, akamtuma mtumishi wake kwa hao wapangaji ili wampe sehemu ya mavuno ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga, wakamfukuza mikono mitupu.
11 He sent yet another servant, and they also beat him, and treated him shamefully, and sent him away empty.
Akamtuma mtumishi mwingine, huyo naye wakampiga, wakamfanyia mambo ya aibu na kumfukuza.
12 He sent yet a third, and they also wounded him, and threw him out.
Bado akamtuma na mwingine wa tatu, huyu pia wakamjeruhi na kumtupa nje ya shamba.
13 The lord of the vineyard said, ‘What shall I do? I will send my agapetos ·beloved, esteemed· son. It may be that seeing him, they will respect him.’
“Basi yule mwenye shamba la mizabibu akasema, ‘Nifanye nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa, huenda yeye watamheshimu.’
14 “But when the farmers saw him, they reasoned among themselves, saying, ‘This is the heir. Come, let’s kill him, that the inheritance may be ours.’
“Lakini wale wapangaji walipomwona, wakasemezana wao kwa wao. Wakasema, ‘Huyu ndiye mrithi. Basi na tumuue ili urithi uwe wetu.’
15 They threw him out of the vineyard, and killed him. What therefore will the lord of the vineyard do to them?
Kwa hiyo wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamuua.” “Sasa basi yule mwenye shamba la mizabibu atawafanyia nini wapangaji hawa?
16 He will come and destroy these farmers, and will give the vineyard to others.” When they heard it, they said, “May it never be!”
Atakuja na kuwaua hao wapangaji, na kuwapa wapangaji wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia hayo wakasema, “Mungu apishie mbali jambo hili lisitokee!”
17 But he looked at them, and said, “Then what is this that is written, ‘The stone which the builders rejected, the same was made the chief cornerstone'?
Lakini Yesu akawakazia macho, akasema, “Basi ni nini maana ya yale yaliyoandikwa: “‘Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni’?
18 Everyone who falls on that stone will be broken to pieces, but it will crush whomever it falls on to dust.”
Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagwa kabisa.”
19 The chief priests and the Torah-Teachers sought to lay hands on him that very hour, but they feared the people— for they knew he had spoken this parable against them.
Walimu wa sheria na viongozi wa makuhani wakatafuta njia ya kumkamata mara moja, kwa sababu walifahamu kwamba amesema mfano huo kwa ajili yao. Lakini waliwaogopa watu.
20 They watched him, and sent out spies, who pretended to be upright, that they might trap him in something he said, so as to deliver him up to the power and authority of the governor.
Kwa hiyo wakawa wanamchunguza na kutuma wapelelezi waliojifanya kuwa wenye haki ili wapate kumtega kwa maneno asemayo, ili wamtie katika uwezo na mamlaka ya mtawala.
21 They asked him, “Teacher, we know that you say and teach what is right, and are not partial to anyone, but truly teach the way of God.
Hivyo wale wapelelezi wakamuuliza, “Mwalimu, tunajua unasema na kufundisha yaliyo kweli wala humpendelei mtu, bali wafundisha njia ya Mungu katika kweli.
22 Does Torah ·Teaching· permit us to pay taxes to Caesar [Ruler], or not?”
Je, ni halali sisi kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
23 But he perceived their craftiness, and said to them, “Why do you test me?
Lakini Yesu akatambua hila yao, kwa hiyo akawaambia,
24 Show me a denarius [one day’s wage]. Whose image and inscription are on it?” They answered, “Caesar’s [Ruler]’s.”
“Nionyesheni dinari. Je, sura hii na maandishi haya yaliyoko juu yake ni vya nani?”
25 He said to them, “Then give to Caesar [Ruler] the things that are Caesar’s, and to God the things that are God’s.”
Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Akawaambia, “Basi mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
26 They were not able to trap him in his words before the people. They marveled at his answer, and were silent.
Wakashindwa kumkamata kwa yale aliyokuwa amesema hadharani. Nao wakashangazwa mno na majibu yake, wakanyamaza kimya.
27 Some of the Sadducees [Morally-upright] came to him, those who deny that there is a resurrection.
Baadhi ya Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza,
28 They asked him, “Teacher, Moses [Drawn out] wrote to us that if a man’s brother dies having a wife, and he is childless, his brother should take the wife, and raise up children for his brother.
“Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu wa mtu akifa na kumwacha mkewe bila mtoto, basi huyo mtu inampasa amwoe huyo mjane ili amzalie ndugu yake watoto.
29 There were therefore seven brothers. The first took a wife, and died childless.
Basi palikuwepo ndugu saba. Yule wa kwanza akaoa, akafa bila kuzaa mtoto.
30 The second took her as wife, and he died childless.
Kisha yule wa pili akamwoa huyo mjane, naye akafa bila mtoto,
31 The third took her, and likewise the seven all left no children, and died.
naye wa tatu pia akamwoa. Vivyo hivyo ndugu wote saba wakawa wamemwoa huyo mwanamke, na wote wakafa pasipo yeyote kupata mtoto.
32 Afterward the woman also died.
Mwishowe, yule mwanamke naye akafa.
33 Therefore in the resurrection whose wife of them will she be? For the seven had her as a wife.”
Sasa basi, siku ya ufufuo huyo mwanamke atakuwa mke wa nani, maana aliolewa na ndugu wote saba?”
34 Yeshua [Salvation] said to them, “The children of this age marry, and are given in marriage. (aiōn g165)
Yesu akawajibu, “Katika maisha haya watu huoa na kuolewa. (aiōn g165)
35 But those who are considered worthy to attain to that age and the resurrection from the dead, neither marry, nor are given in marriage. (aiōn g165)
Lakini wale ambao wamehesabiwa kwamba wanastahili kupata nafasi katika ulimwengu ule na katika ufufuo wa wafu, hawaoi wala hawaolewi. (aiōn g165)
36 For they can’t die any more, for they are like the angels, and are children of God, being children of the resurrection.
Hawa hawawezi kufa tena, kwa maana wao ni kama malaika. Wao ni watoto wa Mungu, kwa sababu ni watoto wa ufufuo.
37 But that the dead are raised, even Moses [Drawn out] showed at the bush, when Yahweh said ‘The God of Abraham [Father of a multitude], the God of Isaac [Laughter], and the God of Jacob [Supplanter].’
Hata Mose alidhihirisha kuwa wafu wanafufuka, kwa habari ya kile kichaka kilichokuwa kikiwaka moto bila kuteketea, alipomwita Bwana, ‘Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.’
38 Now he is not the God of the dead, but of the living, for all are alive to him.”
Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa kuwa kwake wote ni hai.”
39 Some of the Torah-Teachers answered, “Teacher, you speak well.”
Baadhi ya walimu wa sheria wakasema, “Mwalimu, umesema sawasawa kabisa!”
40 They didn’t dare to ask him any more questions.
Baada ya hayo hakuna mtu aliyethubutu kumuuliza maswali tena.
41 He said to them, “Why do they say that the Messiah [Anointed one] is David [Beloved]’s son?
Kisha Yesu akawaambia, “Imekuwaje basi wao husema Kristoni Mwana wa Daudi?
42 For David [Beloved] himself says in the book of Psalms,
Daudi mwenyewe anasema katika Kitabu cha Zaburi: “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume,
43 ‘Yahweh said to adoni [my Lord], “Sit at my right hand until I make your enemies a footstool for your feet.”’
hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
44 “David [Beloved] therefore calls him Lord, so how is he his son?”
Ikiwa Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ basi atakuwaje mwanawe?”
45 In the hearing of all the people, he said to his disciples,
Wakati watu wote walikuwa wanamsikiliza, Yesu akawaambia wanafunzi wake,
46 “Beware of the Torah-Teachers, who like to walk in long robes, and phileo ·affectionately love, have high regard for· greetings in the marketplaces, the best seats in the synagogues, and the best places at feasts;
“Jihadharini na walimu wa sheria. Wao hupenda kutembea wakiwa wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa kwa heshima masokoni. Hupenda kukaa kwenye viti vya mbele katika masinagogi, na kukaa kwenye nafasi za heshima katika karamu.
47 who devour widows’ houses, and for a pretense make long prayers: these will receive greater condemnation.”
Wao hula nyumba za wajane, na ili waonekane kuwa wema, wanasali sala ndefu. Watu kama hawa watapata hukumu iliyo kuu sana.”

< Luke 20 >