< Luke 10 >

1 Now after these things, the Lord also appointed seventy others, and sent them two by two ahead of him into every city and place, where he was about to come.
Baada ya hayo, Bwana aliwachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawiliwawili, wamtangulie katika kila kijiji na mahali ambapo yeye mwenyewe alitaka kwenda.
2 Then he said to them, “The harvest is indeed plentiful, but the laborers are few. Pray therefore to the Lord of the harvest, that he may send out laborers into his harvest.
Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache. Kwa hivyo, mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.
3 Go your ways. Behold, I send you out as lambs among wolves.
Sasa nendeni; fahamuni kwamba ninawatuma ninyi kama kondoo wanaokwenda kati ya mbwa mwitu.
4 Carry no purse, nor wallet, nor sandals. Greet no one on the way.
Msichukue mfuko wa fedha, mkoba, wala viatu; msimsalimu mtu yeyote njiani.
5 Into whatever house you enter, first say, ‘Shalom ·Complete peace· be to this house.’
Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza wasalimuni hivi: Amani iwe katika nyumba hii!
6 If a seeker of shalom ·complete peace· is there, your shalom ·complete peace· will find its rest with him; and if there isn't, it will teshuvah ·completely return· to you.
Kama akiwako mwenye kupenda amani, amani yenu itakaa naye, la sivyo, itawarudieni.
7 Remain in that same house, eating and drinking the things they give, for the laborer is worthy of his wages. Don’t go from house to house.
Kaeni katika nyumba hiyo mkila na kunywa wanavyowapeni, maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msiende mara nyumba hii mara nyumba ile.
8 Into whatever city you enter, and they receive you, eat the things that are set before you.
Kama mkifika mji fulani na watu wakiwakaribisha, kuleni wanavyowapeni.
9 Heal the sick who are therein, and tell them, ‘God’s Kingdom has come near to you.’
Ponyeni wagonjwa walioko huko, waambieni watu: Ufalme wa Mungu umekaribia kwenu.
10 But into whatever city you enter, and they don’t receive you, go out into its streets and say,
Lakini mkiingia katika mji wowote, wasipowakaribisheni, tokeni; nanyi mpitapo katika barabara zao semeni:
11 ‘Even the dust from your city that clings to us, we wipe off against you. Nevertheless know this, that God’s Kingdom has come near to you.’
Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu tunawakung'utieni. Lakini, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
12 I tell you, it will be more tolerable in that day for Sodom [Burning] than for that city.
Hakika nawaambieni, siku ile mji huo utapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Sodoma.
13 “Woe to you, Chorazin! Woe to you, Bethsaida! For if the mighty works had been done in Tyre and Sidon which were done in you, they would have made teshuvah ·complete repentance· long ago, sitting in sackcloth and ashes.
“Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika kule Tiro na Sidoni, watu wake wangalikwishavaa mavazi ya gunia kitambo, na kukaa katika majivu kuonyesha kwamba wametubu.
14 But it will be more tolerable for Tyre and Sidon in the judgment than for you.
Hata hivyo, Siku ya Hukumu ninyi mtapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Tiro na Sidoni.
15 You, Capernaum [Village-Comfort, Village-Compassion], who are exalted to heaven, will be brought down to Hades / Sh'ol ·Place of the dead·. (Hadēs g86)
Na wewe Kafarnaumu, unataka kujikweza mpaka mbinguni? La; utaporomoshwa mpaka Kuzimu.” (Hadēs g86)
16 Whoever listens to you listens to me, and whoever rejects you rejects me. Whoever rejects me rejects him who sent me.”
Halafu akasema, “Anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; na anayekataa kuwapokea ninyi, anakataa kunipokea mimi. Yeyote anayekataa kunipokea, anakataa kumpokea yule aliyenituma.”
17 The seventy teshuvah ·completely returned· with joy, saying, “Lord, even the demons are subject to us in your name!”
Baadaye, wale sabini na wawili walirudi wamejaa furaha, wakisema, “Bwana, hata pepo wametutii tulipolitaja jina lako.”
18 He said to them, “I saw Satan [Adversary] having fallen like lightning from heaven.
Yeye akawaambia, “Nilimwona Shetani jinsi alivyokuwa anaporomoka kama umeme kutoka mbinguni.
19 Behold, I give you authority to tread on serpents and scorpions, and over all the power of the enemy. Nothing will in any way hurt you.
Naam, nimewapeni uwezo wa kukanyaga nyoka na ng'e, na uwezo juu ya nguvu zote za yule adui; hakuna chochote kitakachowadhuru.
20 Nevertheless, don’t rejoice in this, that the spirits are subject to you, but rejoice that your names are written in heaven.”
Hata hivyo, msifurahi kwa sababu pepo wamewatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.”
21 In that same hour Yeshua [Salvation] rejoiced in Ruach haKodesh [Spirit of the Holiness], and said, “I thank you, O Abba ·Father familiar, Dear Dad·, Lord of heaven and earth, that you have hidden these things from the wise and understanding, and revealed them to little children. Yes, Abba ·Father familiar, Dear Dad·, for so it was well-pleasing in your sight.”
Saa ileile, Yesu akafurahi kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akasema, “Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewaficha wenye hekima na elimu mambo haya, ukawafumbulia wadogo. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza.”
22 Turning to the disciples, he said, “All things have been delivered to me by 'Avi ·my Father·. No one knows who the Son is, except the Abba Father, and who the Abba Father is, except the Son, and he to whomever the Son desires to reveal him.”
Kisha akasema, “Baba yangu ameweka yote mikononi mwangu. Hakuna amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala amjuaye Baba ni nani ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana anataka kumfunulia hayo.”
23 Turning to the disciples, he said privately, “Blessed are the eyes which see the things that you see,
Halafu akawaelekea wafuasi wake akawaambia, “Heri wanaoona yale mnayoyaona ninyi!
24 for I tell you that many prophets and kings desired to see the things which you see, and didn’t see them, and to hear the things which you hear, and didn’t hear them.”
Hakika, manabii na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona ninyi wasiyaone, na kusikia yale mnayoyasikia wasiyasikie.”
25 Behold, a certain lawyer stood up and tested him, saying, “Teacher, what shall I do to inherit eternal life?” (aiōnios g166)
Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, “Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
26 He said to him, “What is written in the Torah ·Teaching·? How do you read it?”
Yesu akamwuliza, “Imeandikwa nini katika Sheria? Unaelewaje?”
27 He answered, “You shall have agapao ·total devotion love· to MarYah [Master Yahweh] your God with all your heart, with all your soul, with all your strength, and with all your mind; and your neighbor as yourself.”
Akamjibu, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
28 He said to him, “You have answered correctly. Do this, and you will live.”
Yesu akawaambia, “Vema! Fanya hivyo, nawe utaishi.”
29 But he, desiring to justify himself, asked Yeshua [Salvation], “Who is my neighbor?”
Lakini yeye akitaka kujihakikishia kuwa mwema akamwuliza Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
30 Yeshua [Salvation] answered, “A certain man was going down from Jerusalem [City of peace] to Jericho [Fragrant, Moon], and he fell among robbers, who both stripped him and beat him, and departed, leaving him half dead.
Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko. Alipokuwa njiani, alivamiwa na majambazi, wakamnyang'anya mali yake na kumpiga, wakamwacha amelala pale nusu mfu.
31 By chance a certain priest was going down that way. When he saw him, he passed by on the other side.
Kumbe, kuhani mmoja akawa anapita barabara ileile, akamwona, akapita kando.
32 In the same way a Levite [Descendant of United with] also, when he came to the place, and saw him, passed by on the other side.
Hali kadhalika na Mlawi mmoja, alipofika mahali akamwona, akapita kando.
33 But a certain Samaritan [person from Watch-mountain], as he traveled, came where he was. When he saw him, he was moved with compassion,
Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa anasafiri, alifika pale yule mtu alipokuwa, naye alipomwona, alimwonea huruma.
34 came to him, and bound up his wounds, pouring on oil and wine. He set him on his own animal, and brought him to an inn, and took care of him.
Akamwendea, akamtibu majeraha yake kwa kumtia mafuta na divai; na kuyafunga halafu akampandisha juu ya punda wake akampeleka katika nyumba moja ya wageni akamuuguza.
35 On the next day, when he departed, he took out two denarii (2 days wages), and gave them to the host, and said to him, ‘Take care of him. Whatever you spend beyond that, I will repay you when I teshuvah ·completely return·.’
Kesho yake akatoa fedha dinari mbili akampa yule mwenye nyumba, akamwambia, Muuguze mtu huyu; na chochote utakachotumia zaidi, nitakulipa nitakaporudi.”
36 Now which of these three do you think seemed to be a neighbor to him who fell among the robbers?”
Kisha Yesu akauliza, “Kati ya hao watatu, ni yupi aliyeonyesha kuwa jirani yake yule aliyevamiwa na majambazi?”
37 He said, “He who showed eleos ·merciful compassion in action· on him.” Then Yeshua [Salvation] said to him, “Go and do likewise.”
Yule mwalimu wa Sheria akamjibu, “Ni yule aliyemwonea huruma.” Yesu akamwambia, “Nenda ukafanye vivyo hivyo.”
38 As they went on their way, he entered into a certain village, and a certain woman named Martha [Lady mistress, Strong bitterness] received him into her house.
Walipokuwa safarini, waliingia katika kijiji kimoja na mwanamke mmoja, aitwaye Martha, alimkaribisha nyumbani kwake.
39 She had a sister called Mary [Rebellion], who also sat at Yeshua [Salvation]'s feet, and heard his word.
Martha alikuwa na dada yake aitwaye Maria; huyu aliketi karibu na Yesu akisikiliza mafundisho yake.
40 But Martha [Lady mistress, Strong bitterness] was distracted with much serving, and she came up to him, and said, “Lord, don’t you care that my sister left me to serve alone? Ask her therefore to help me.”
Lakini Martha alikuwa anashughulika na mambo mengi. Basi, akamwendea Yesu, akamwambia, “Bwana, hivi hujali kwamba dada yangu ameniacha nishughulike peke yangu? Mwambie basi, anisaidie.”
41 Yeshua [Salvation] answered her, “Martha [Lady mistress, Strong bitterness], Martha [Lady mistress, Strong bitterness], you are anxious and troubled about many things,
Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, unahangaika na kusumbuka kwa mambo mengi.
42 but one thing is needed. Mary [Rebellion] has chosen the good part, which will not be taken away from her.”
Kitu kimoja tu ni muhimu. Maria amechagua kitu bora zaidi ambacho hakuna mtu atakayemnyag'anya.”

< Luke 10 >