< Psalms 28 >

1 [By David.] To you, YHWH, I call. My rock, do not be deaf to me; lest, if you are silent to me, I would become like those who go down into the pit.
Zaburi ya Daudi. Ninakuita wewe, Ee Bwana, Mwamba wangu; usiwe kwangu kama kiziwi. Kwa sababu ukinyamaza nitafanana na walioshuka shimoni.
2 Hear the voice of my petitions, when I cry to you, when I lift up my hands toward your Most Holy Place.
Sikia kilio changu unihurumie ninapokuita kwa ajili ya msaada, niinuapo mikono yangu kuelekea Patakatifu pa Patakatifu pako.
3 Do not draw me away with the wicked, with evildoers who speak peace with their neighbors, but mischief is in their hearts.
Usiniburute pamoja na waovu, pamoja na hao watendao mabaya, ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri, lakini mioyoni mwao wameficha chuki.
4 Give them according to their work, and according to the wickedness of their doings. Give them according to the operation of their hands. Bring back on them what they deserve.
Walipe sawasawa na matendo yao, sawasawa na matendo yao maovu; walipe sawasawa na kazi za mikono yao, uwalipe wanavyostahili.
5 Because they do not regard the works of YHWH, nor the operation of his hands, he will break them down and not build them up.
Kwa kuwa hawaheshimu kazi za Bwana, na yale ambayo mikono yake imetenda, atawabomoa na kamwe hatawajenga tena.
6 Blessed be YHWH, because he has heard the voice of my petitions.
Bwana asifiwe, kwa maana amesikia kilio changu nikimwomba anihurumie.
7 YHWH is my strength and my shield. My heart has trusted in him, and I am helped. Therefore my heart greatly rejoices. With my song I will thank him.
Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu, moyo wangu umemtumaini yeye, nami nimesaidiwa. Moyo wangu unarukaruka kwa furaha nami nitamshukuru kwa wimbo.
8 YHWH is the strength of his people. He is a stronghold of salvation to his anointed.
Bwana ni nguvu ya watu wake, ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.
9 Save your people, and bless your inheritance. Be their shepherd also, and bear them up forever.
Waokoe watu wako na uubariki urithi wako; uwe mchungaji wao na uwabebe milele.

< Psalms 28 >