< Psalms 124 >

1 [A Song of Ascents. By David.] If it had not been the LORD who was on our side, let Israel now say,
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Kama Bwana asingalikuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa:
2 if it had not been the LORD who was on our side, when men rose up against us;
kama Bwana asingalikuwa upande wetu, wakati watu walipotushambulia,
3 then they would have swallowed us up alive, when their wrath was kindled against us;
wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangalitumeza tungali hai,
4 then the waters would have overwhelmed us, the stream would have gone over our soul;
mafuriko yangalitugharikisha, maji mengi yangalitufunika,
5 then the proud waters would have gone over our soul.
maji yaendayo kasi yangalituchukua.
6 Blessed be the LORD, who has not given us as a prey to their teeth.
Bwana asifiwe, yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
7 Our soul has escaped like a bird out of the fowler's snare. The snare is broken, and we have escaped.
Tumeponyoka kama ndege kutoka mtego wa mwindaji; mtego umevunjika, nasi tukaokoka.
8 Our help is in the name of the LORD, who made heaven and earth.
Msaada wetu ni katika jina la Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.

< Psalms 124 >