< Psalms 111 >

1 Praise the LORD. I will give thanks to the LORD with my whole heart, in the council of the upright, and in the congregation.
Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
2 The LORD's works are great, pondered by all those who delight in them.
Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3 His work is honor and majesty. His righteousness endures forever.
Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
4 He has caused his wonderful works to be remembered. The LORD is gracious and merciful.
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
5 He has given food to those who fear him. He always remembers his covenant.
Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
6 He has shown his people the power of his works, in giving them the heritage of the nations.
Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
7 The works of his hands are truth and justice. All his precepts are sure.
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
8 They are established forever and ever. They are done in truth and uprightness.
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9 He has sent redemption to his people. He has ordained his covenant forever. His name is holy and awesome.
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10 The fear of the LORD is the beginning of wisdom. All those who do his work have a good understanding. His praise endures forever.
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.

< Psalms 111 >