< Judges 6 >

1 And the children of Israel did that which was evil in the sight of the LORD, and the LORD delivered them into the hand of Midian seven years.
Wana wa Israeli wakafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana; naye akawatia mikononi mwa Midiani kwa miaka saba.
2 And the hand of Midian prevailed against Israel; and because of Midian the children of Israel made for themselves the dens which are in the mountains, and the caves, and the strongholds.
Uwezo wa Midiani uliwanyanyasa Israeli. Kwa sababu ya Midiani, watu wa Israeli walitengeneza makao wenyewe kutoka kwenye mabwawa katika milima, mapango, na ngome.
3 And so it was, when Israel had sown, that Midian, Amalek, and the Kedemites would come up against them.
Kisha ikawa kwamba wakati wowote Waisraeli walipopanda mazao yao, Wamidiani na Waamaleki na watu kutoka mashariki waliwavamia Waisraeli.
4 And they camped against them, and destroyed the increase of the earth, as far as Gaza, and they left no sustenance in Israel, as well as sheep, or ox, or donkey.
Waliweza kutengenezajeshi lao juu ya ardhi na kuharibu mazao, mpaka njia ya Gaza. Hawakuacha chakula huko Israeli, wala kondoo wala ng'ombe wala punda.
5 For they came up with their livestock and their tents and their camels. They would come in like locusts in number, and they were innumerable. And they came into the land to ravage it.
Kila wakati wao na mifugo yao na mahema walipokuja, walikuja kama kundi la nzige, na haikuwezekana kuhesabu watu au ngamia zao. Walivamia ardhi ili kuiharibu.
6 Israel was brought very low because of Midian; and the children of Israel cried to the LORD.
Midiani iliwadhoofisha Waisraeli sana mpaka watu wa Israeli wakamwita Bwana.
7 It happened, when the children of Israel cried to the LORD because of Midian,
Watu wa Israeli walipomwomba Bwana kwa sababu ya Midiani,
8 that the LORD sent a prophet to the children of Israel, and he said to them, "Thus says the LORD, the God of Israel, 'I brought you up from the land of Egypt, and brought you forth out of the house of bondage;
Bwana alimtuma nabii kwa wana wa Israeli. Nabii akawaambia, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nimekuleta kutoka Misri; Nilikutoa nje ya nyumba ya utumwa.
9 and I delivered you out of the hand of the Egyptians, and out of the hand of all who oppressed you, and drove them out from before you, and gave you their land;
Naliwaokoa kutoka kwenye mikono ya Wamisri, na kutoka kwenye mkono wa wote waliokuwa wakikunyanyasa. Niliwafukuza mbele yenu, na nimewapa nchi yao.
10 and I said to you, "I am the LORD your God; you shall not fear the gods of the Amorites, in whose land you dwell." But you have not listened to my voice.'"
Niliwaambia, “Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu; Nimewaamuru msiabudu miungu ya Waamori, ambao mnaishi katika nchi yao. Lakini hamkuitii sauti yangu.”
11 The angel of the LORD came, and sat under the oak which was in Ophrah, that pertained to Joash the Abiezrite: and his son Gideon was beating out wheat in the winepress, to hide it from the Midianites.
Basi malaika wa Bwana akaja na kukaa chini ya mwaloni huko Ofra, uliokuwa wa Yoashi (Mwabiyezeri), wakati Gidioni, mwana wa Yoashi, akitenganisha ngano katika sakafu, katika kikapu cha divai-kuificha toka kwa Wamidiani.
12 The angel of the LORD appeared to him, and said to him, "The LORD is with you, mighty warrior."
Malaika wa Bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nanyi, mpiganaji mwenye nguvu!
13 Gideon said to him, "Oh, my lord, if the LORD is with us, why then has all this happened to us? Where are all his wondrous works which our fathers told us of, saying, 'Didn't the LORD bring us up from Egypt?' But now the LORD has cast us off, and delivered us into the hand of Midian."
Gideoni akamwambia, Oo, bwana wangu, ikiwa Bwana yu pamoja nasi, kwa nini basi yote haya yanatupata? Je, yako wapi matendo yake yote mazuri ambayo baba zetu walituambia, waliposema, 'Je! si Bwana aliyetukomboa kutoka Misri?' Lakini sasa Bwana ametuacha na kututia mikononi mwa Midiani. '
14 The LORD looked at him, and said, "Go in this strength of yours and save Israel from the hand of Midian. Look, haven't I sent you?"
Bwana akamtazama na kusema, “Nenda katika nguvu uliyo nayo tayari. Uiokoe Israeli kutoka mkononi wa Midiani. Je, sikukutuma?”
15 He said to him, "O Lord, how shall I save Israel? Look, my family is the poorest in Manasseh, and I am the least in my father's house."
Gideoni akamwambia, “Tafadhali, Bwana, nawezeje kuwaokoa Israeli? Angalia, familia yangu ni dhaifu zaidi katika Manase, na mimi si muhimu katika nyumba ya baba yangu.”
16 And the LORD said to him, "Surely I will be with you, and you shall strike the Midianites as one man."
Bwana akamwambia, “Nitakuwa pamoja nawe, nawe utalishinda jeshi lote la Midiani kama mtu mmoja.”
17 He said to him, "If now I have found favor in your sight, then show me a sign that it is you who talk with me.
Gideoni akamwambia, “Ikiwa unapendezwa na mimi, nipe basi ishara kwamba wewe ndio unenena nami.
18 Please do not go away, until I come to you, and bring out my present, and lay it before you." He said, "I will wait until you come back."
Tafadhali, usiondoke hapa, mpaka nitakapokuja kwako na kuleta zawadi yangu na kuiweka mbele yako.” Bwana akasema, “Nitasubiri mpaka utakaporudi.”
19 Gideon went in, and made ready a kid, and unleavened cakes of an ephah of meal: the meat he put in a basket, and he put the broth in a pot, and brought it out to him under the oak, and presented it.
Gideoni akaenda, akaandaa mwana mbuzi, na efa moja ya unga akafanya mikate isiyotiwa chachu. Akaiweka nyama hiyo katika kikapu, na akaweka mchuzi ndani ya sufuria na kuviletea chini ya mti wa mwaloni, akavitowa.
20 The angel of God said to him, "Take the meat and the unleavened cakes, and lay them on this rock, and pour out the broth." And he did so.
Malaika wa Mungu akamwambia, “Chukua nyama na mikate isiyotiwa chachu, ukaweke juu ya mwamba huu, ukamwage mchuzi juu yake.” Gideoni akafanya hivyo.
21 Then the angel of the LORD put forth the end of the staff that was in his hand, and touched the flesh and the unleavened cakes; and there went up fire out of the rock, and consumed the flesh and the unleavened cakes; and the angel of the LORD departed out of his sight.
Kisha malaika wa Bwana akashika ncha ya fimbo mkononi mwake. Kwa hiyo akagusa nyama na mikate isiyotiwa chachu; moto ukatoka nje ya mwamba, ukateketeza nyama na mikate isiyotiwa chachu. Kisha malaika wa Bwana akaenda, na Gideoni hakuweza kumwona tena.
22 Gideon saw that he was the angel of the LORD; and Gideon said, "Alas, Lord GOD. Because I have seen the angel of the LORD face to face."
Gideoni alielewa kuwa yule alikuwa malaika wa Bwana. Gideoni akasema, “Ewe Bwana MUNGU! Kwa maana nimemwona malaika wa Bwana uso kwa uso!”
23 The LORD said to him, "Peace be to you. Do not be afraid. You shall not die."
Bwana akamwambia, “Amani iwe kwako! Usiogope, huwezi kufa.”
24 Then Gideon built an altar there to the LORD, and called it "The LORD is Peace." To this day it is still in Ophrah of the Abiezrites.
Basi Gideoni akamjengea Bwana madhabahu huko. Aliiita, “Bwana ni Amani.” Hadi leo bado iko katika Ofra ya jamaa ya Waabiezeri.
25 It happened the same night, that the LORD said to him, "Take your father's bull, even the second bull seven years old, and tear down the altar of Baal that your father has, and cut down the Asherah that is beside it;
Usiku huo, Bwana akamwambia, “Twaa ng'ombe wa baba yako, na ng'ombe wa pili wa umri wa miaka saba, ukaondoe madhabahu ya Baali, ambayo ni ya baba yako, na kukata Ashera iliyo karibu nayo.
26 and build an altar to the LORD your God on the top of this stronghold, in the orderly manner, and take the second bull, and offer a burnt offering with the wood of the Asherah which you shall cut down."
Jenga madhabahu kwa Bwana, Mungu wako juu ya mahali pa kukimbilia, na kuijenga njia sahihi. Toa ng'ombe ya pili kama sadaka ya kuteketezwa, ukitumia kuni kutoka Ashera uliyoikata. '
27 Then Gideon took ten men of his servants, and did as the LORD had spoken to him: and it came about, because he feared his father's household and the men of the city, so that he could not do it by day, that he did it by night.
Gideoni akachukua watumishi wake kumi na kufanya kama Bwana alivyomwambia. Lakini kwa sababu aliogopa sana watu wa nyumba ya baba yake na watu wa mji hakufanya hivyo wakati wa mchana, alifanya hivyo usiku.
28 When the men of the city arose early in the morning, look, the altar of Baal was broken down, and the Asherah was cut down that was by it, and the second bull was offered on the altar that was built.
Asubuhi wakati watu wa mji walipoamka, madhabahu ya Baali imebomolewa, na Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwa, na ng'ombe wa pili ametolewa sadaka kwenye madhabahu iliyojengwa.
29 And they said to one another, "Who has done this thing?" When they inquired and asked, they said, "Gideon the son of Joash has done this thing."
Watu wa mji wakaambiana, “Ni nani aliyefanya jambo hili?” Walipokuwa wakiongea na wengine na kutafuta majibu, wakasema, 'Gidioni mwana wa Yoashi amefanya jambo hili.”
30 Then the men of the city said to Joash, "Bring out your son, that he may die, because he has broken down the altar of Baal, and because he has cut down the Asherah that was by it."
Ndipo watu wa mji wakamwambia Yoashi, “Mtoe mtoto wako ili afe, kwa sababu ameibomoa madhabahu ya Baali, na kwa sababu ameikata Ashera karibu nayo.”
31 Joash said to all who stood against him, "Will you contend for Baal? Or will you save him? He who will contend for him, let him be put to death while it is yet morning: if he is a god, let him contend for himself, because someone has broken down his altar."
Yoashi akawaambia wote waliompinga, “Je, ninyi mtamsihi Baali? Je, mtamuokoa? Mtu yeyote atakayemtetea, basi atauawa asubuhi hii. Ikiwa Baali ni mungu, basi atajitetea mwenyewe wakati mtu anaibomoa madhabahu yake.”
32 Therefore on that day he named him Jerubbaal, saying, "Let Baal contend against him, because he has broken down his altar."
Kwa hiyo siku hiyo wakamwita Gideoni “Yerubaali,” kwa sababu alisema, “Baali ajijitetee dhidi yake,” kwa sababu Gidioni alivunja madhabahu ya Baali.
33 Then all Midian and Amalek and the Kedemites assembled themselves together; and they crossed over, and camped in the Valley of Jezreel.
Basi Wamidiani wote, Waamaleki, na watu wa mashariki walikusanyika pamoja. Wakavuka Yordani na wakapanga katika bonde la Yezreeli.
34 But the Spirit of the LORD came on Gideon; and he blew a trumpet; and Abiezer was gathered together after him.
Lakini Roho wa Bwana akaja juu ya Gideoni. Gideoni akapiga tarumbeta, akawaita jamaa ya Abiezeri, ili wapate kumfuata.
35 He sent messengers throughout all Manasseh; and they also were gathered together after him: and he sent messengers to Asher, and to Zebulun, and to Naphtali; and they came up to meet them.
Aliwatuma wajumbe wote katika Manase, na wao pia, waliitwa nje kumfuata. Naye akatuma wajumbe kwa Asheri, na Zabuloni, na Naftali; nao wakaenda kumlaki.
36 Gideon said to God, "If you will save Israel by my hand, as you have spoken,
Gideoni akamwambia Mungu, “Ikiwa ungependa kunitumia kuokoa Israeli, kama ulivyosema,
37 look, I will put a fleece of wool on the threshing floor; if there is dew on the fleece only, and it is dry on all the ground, then shall I know that you will save Israel by my hand, as you have spoken."
tazameni, ninaweka ngozi ya samazi kwenye sakafu. Ikiwa kuna umande tu juu ya ngozi, na ni kavu duniani, basi nitajua kwamba utanitumia kuokoa Israeli, kama ulivyosema.”
38 It was so; for he rose up early on the next day, and pressed the fleece together, and wrung the dew out of the fleece, a bowl full of water.
Hivi ndivyo ilivyotokea-Gideoni aliamka mapama asubuhi, akaikamua ngozi hiyo, na akatoa umande kwenye ngozi, wa kutosha kujaza bakuli kwa maji.
39 Gideon said to God, "Do not let your anger be kindled against me, and I will speak but this once. Please let me make one more test with the fleece; let it now be dry only on the fleece, and on all the ground let there be dew."
Gideoni akamwambia Mungu, 'Usinikasirikie, nitasema tena kwa mara nyingine. Tafadhali niruhusu nijaribu tena kwa kutumia ngozi. Wakati huu uifanye kavu, na iwe na umande juu ya ardhi yote kuzunguka.
40 God did so that night, for it was dry on the fleece only, and there was dew all over the ground.
Mungu alifanya kile alichoomba usiku huo. Ngozi ilikuwa kavu, na kulikuwa na umande katika ardhi yote iliyozunguka.

< Judges 6 >