< Psalms 53 >

1 [For the Chief Musician. To the tune of "Mahalath." A contemplation by David.] The fool has said in his heart, "There is no God." They are corrupt, and have done abominable iniquity. There is no one who does good.
Mpumbavu husema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wamepotoka na kufanya machukizo; hakuna mmoja atendaye mema.
2 God looks down from heaven on the descendants of Adam, to see if there are any who are wise, who seek after God.
Toka mbinguni Mungu hutazama chini kwa wanadamu kuona kama kuna yeyote mweye akili, amtafutaye yeye.
3 Every one of them has gone back. They have become filthy together. There is no one who does good, no, not one.
Wote wamekengeuka. Kwa pamoja wamepotoka. Hakuna atendaye mema, hata mmoja.
4 Have evildoers no knowledge, who eat up my people as they eat bread, and do not call on God?
Je, wale wanao fanya uovu hawana uelewa - wale walao watu wangu kana kwamba wanakula mkate na hawamuiti Mungu?
5 There they will be in great fear, where no fear had been, for God will scatter the bones of those who encamp against you. You will put them to shame, because God has rejected them.
Wao walikuwa katika hofu kuu, ingawa hakuna sababu ya kuogopa ilikuwepo hapo; maana Mungu ataitawanya mifupa ya yeyote atakaye kusanyika dhidi yako; watu kama hao wataaibishwa kwa sababu Mungu amewakataa wao.
6 Oh that the salvation of Israel would come out of Zion. When God brings back his people from captivity, may Jacob rejoice, may Israel be glad.
Oh, kwamba wokovu wa Israel ungepatikana Sayuni! Wakati Mungu atakapowaleta watu wake kutoka kifungoni, ndipo Yakobo atashangilia na Israeli itafurahi!

< Psalms 53 >