< Luke 21 >

1 He looked up, and saw the rich people who were putting their gifts into the treasury.
Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
2 He saw a certain poor widow casting in two lepta.
Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
3 He said, "Truly I tell you, this poor widow put in more than all of them,
Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
4 for all these put in gifts from their abundance, but she, out of her poverty, put in all that she had to live on."
Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
5 As some were talking about the temple and how it was decorated with beautiful stones and gifts, he said,
Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
6 "As for these things which you see, the days will come, in which there will not be left here one stone on another that will not be thrown down."
“Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
7 They asked him, "Teacher, so when will these things be? What is the sign that these things are about to happen?"
Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
8 He said, "Watch out that you do not get led astray, for many will come in my name, saying, 'I am he,' and, 'The time is near.' Therefore do not follow them.
Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
9 When you hear of wars and disturbances, do not be terrified, for these things must happen first, but the end won't come immediately."
Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
10 Then he said to them, "Nation will rise against nation, and kingdom against kingdom.
Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
11 There will be great earthquakes, famines, and plagues in various places. There will be terrors and great signs from heaven.
Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
12 But before all these things, they will lay their hands on you and will persecute you, delivering you up to synagogues and prisons, bringing you before kings and governors for my name's sake.
Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
13 It will turn out as a testimony for you.
Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
14 Settle it therefore in your hearts not to meditate beforehand how to answer,
Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
15 for I will give you a mouth and wisdom which all your adversaries will not be able to withstand or to contradict.
kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
16 You will be handed over even by parents, brothers, relatives, and friends. They will cause some of you to be put to death.
Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
17 And you will be hated by everyone because of my name.
Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
18 But not a hair of your head will perish.
Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
19 "By your endurance you will win your lives.
Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
20 "But when you see Jerusalem surrounded by armies, then know that its desolation is near.
Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
21 Then let those who are in Judea flee to the mountains. Let those who are in the midst of her depart. Let those who are in the country not enter it.
Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
22 For these are days of vengeance, that all things which are written may be fulfilled.
Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
23 Woe to those who are pregnant and to those who nurse infants in those days. For there will be great distress in the land, and wrath to this people.
Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
24 And they will fall by the edge of the sword and be led captive into all the nations. And Jerusalem will be trampled down by non-Jewish people until the times are fulfilled. And there will be times of the non-Jewish people.
Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
25 And there will be signs in the sun, and moon, and stars, and on the earth distress of nations in perplexity because of the roaring of the sea and the waves;
Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
26 people will be fainting from fear, and from expectation of the things which are coming on the world, for the powers of the heavens will be shaken.
Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
27 Then they will see the Son of Man coming in a cloud with power and great glory.
Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
28 But when these things begin to happen, look up, and lift up your heads, because your redemption is near."
Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
29 He told them a parable. "See the fig tree, and all the trees.
Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
30 When they are already budding, you see it and know by your own selves that the summer is already near.
Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
31 Even so you also, when you see these things happening, know that the Kingdom of God is near.
Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
32 Truly I tell you, this generation will not pass away until all things are accomplished.
Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
33 Heaven and earth will pass away, but my words will by no means pass away.
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
34 "So be careful, or your hearts will be loaded down with carousing, drunkenness, and cares of this life, and that day will come on you suddenly.
Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
35 For it will come like a snare on all those who dwell on the surface of all the earth.
kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
36 Therefore be watchful all the time, praying that you may be able to escape all these things that will happen, and to stand before the Son of Man."
Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
37 Every day Yeshua was teaching in the temple, and every night he would go out and spend the night on the mountain that is called Olivet.
Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
38 All the people came early in the morning to him in the temple to hear him.
Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.

< Luke 21 >