< Psalms 76 >

1 [For the Chief Musician. On stringed instruments. A Psalm by Asaph. A song.] In Judah, God is known. His name is great in Israel.
Mungu amefanya mwenyewe kujulikana katika Yuda; jina lake ni kuu katika Israeli.
2 And his abode is in Salem, and his lair in Zion.
Hema yake iko salemu; makao yake yako yako Sayuni.
3 There he broke the flaming arrows of the bow, the shield, and the sword, and the weapons of war. (Selah)
Huko ndiko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita. (Selah)
4 Glorious are you, and excellent, more than mountains of game.
Wewe unang'aa sana na huufunua utukufu wako, ushukapo kutoka milimani, ambako uliwauwa mateka.
5 Valiant men lie plundered, they have slept their last sleep. None of the men of war can lift their hands.
Wenye moyo shujaa walitekwa nyara; walilala mauti. Mashujaa wote walikuwa wanyonge.
6 At your rebuke, God of Jacob, both chariot and horse are cast into a deep sleep.
Kwa kukemea kwako, ewe Mungu wa Yakobo, wote gari na farasi walilala mauti.
7 You, even you, are to be feared. Who can stand in your sight when you are angry?
Wewe, ndiyo wewe, ni wa kuogopwa; ni nani awezaye kusimama mbele yako wakati ukiwa na hasira?
8 You pronounced judgment from heaven. The earth feared, and was silent,
Kutoka mbinguni wewe uliifanya hukumu yako isikike; nchi iliogopa na ikaa kimya
9 when God arose to judgment, to save all the afflicted ones of the earth. (Selah)
wakati wewe, Mungu, ulipoinuka kutekeleza hukumu na kuwaokoa wote wa nchi walio onewa. (Selah)
10 Surely the wrath of man praises you. The survivors of your wrath are restrained.
Hakika hukumu ya hasira yako dhidi ya binadamu itakuletea wewe sifa; wewe hujifunga mwenyewe hasira yako iliyo baki.
11 Make vows to the LORD your God, and fulfill them. Let all of his neighbors bring presents to him who is to be feared.
Wekeni nadhiri kwa Yahwe Mungu wenu na kuzihifadhi. Nao wote wamzungukao yeye mleteeni zawadi yeye ambaye ni wa kuogopwa.
12 He humbles the spirit of princes. He is feared by the kings of the earth.
Yeye huzikata roho za wakuu; huogopwa na wafalme wa nchi.

< Psalms 76 >