< Yochanan 7 >

1 After these things, Jesus was walking in Galilee, for he would not walk in Judea, because the Jewish leaders sought to kill him.
Baada ya hayo, Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea mkoani Yudea kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wanataka kumwua.
2 Now the Jewish festival, the Feast of Tabernacles, was near.
Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
3 So his brothers said to him, "Depart from here, and go into Judea, that your disciples also may see your works that you are doing.
Basi ndugu zake wakamwambia, “Ondoka hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wazione kazi unazozifanya.
4 For no one does anything in secret when he himself seeks to be known openly. If you do these things, show yourself to the world."
Mtu hafanyi mambo kwa siri kama anataka kujulikana kwa watu. Maadam unafanya mambo haya, basi, jidhihirishe kwa ulimwengu.”
5 For even his brothers did not believe in him.
(Hata ndugu zake hawakumwamini!)
6 Jesus therefore said to them, "My time has not yet come, but your time is always ready.
Basi, Yesu akawaambia, “Wakati wangu ufaao haujafika bado. Lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa.
7 The world cannot hate you, but it hates me, because I testify about it, that its works are evil.
Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini mimi wanichukia kwa sababu mimi nauambia wazi kwamba matendo yake ni maovu.
8 You go up to the feast. I am not yet going up to this feast, because my time is not yet fulfilled."
Ninyi nendeni kwenye sikukuu hiyo. Mimi siendi kwenye sikukuu hiyo, maana saa yangu ifaayo haijafika.”
9 After he had said this, he stayed in Galilee.
Alisema hayo kisha akabaki huko Galilaya.
10 But when his brothers had gone up to the feast, then he also went up, not publicly, but as it were in secret.
Baada ya ndugu zake kwenda kwenye sikukuu, Yesu naye alikwenda, lakini hakuenda kwa hadhara bali kwa siri.
11 The Jewish leaders therefore sought him at the feast, and said, "Where is he?"
Viongozi wa Wayahudi walikuwa wanamtafuta kwenye sikukuu hiyo; Wakauliza: “Yuko wapi?”
12 There was much murmuring among the crowds concerning him. Some said, "He is a good man." But others said, "Not so, but he leads the crowd astray."
Kulikuwa na minong'ono mingi katika umati wa watu. Baadhi yao walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “La! Anawapotosha watu.”
13 Yet no one spoke openly of him for fear of the Jewish leaders.
Hata hivyo hakuna mtu aliyethubutu kusema, habari zake hadharani kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi.
14 But when it was now the midst of the feast, Jesus went up into the temple and taught.
Sikukuu hiyo ilipofikia katikati, Yesu naye alikwenda Hekaluni, akaanza kufundisha.
15 Then the Jewish leaders were astonished, saying, "How does this man know such writings, having never been educated?"
Basi, Wayahudi wakashangaa na kusema “Mtu huyu amepataje elimu naye hakusoma shuleni?”
16 Jesus therefore answered them, "My teaching is not mine, but his who sent me.
Hapo Yesu akawajibu, “Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
17 If anyone desires to do his will, he will know about the teaching, whether it is from God, or if I am speaking from myself.
Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe.
18 He who speaks from himself seeks his own glory, but he who seeks the glory of him who sent him is true, and no unrighteousness is in him.
Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
19 Did not Moses give you the Law, and yet none of you keeps the Law? Why do you seek to kill me?"
Je, Mose hakuwapeni Sheria? Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishika Sheria. Kwa nini mnataka kuniua?”
20 The crowd answered, "You have a demon. Who seeks to kill you?"
Hapo watu wakamjibu, “Una wazimu wewe! Nani anataka kukuua?”
21 Jesus answered them, "I did one work, and you are all amazed.
Yesu akawajibu, “Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia.
22 Moses has given you circumcision (not that it is of Moses, but of the fathers), and on the Sabbath you circumcise a boy.
Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa ninyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato.
23 If a boy receives circumcision on the Sabbath, that the Law of Moses may not be broken, are you angry with me, because I made a man completely healthy on the Sabbath?
Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi Sheria ya Mose isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato?
24 Do not judge according to appearance, but judge righteous judgment."
Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki.”
25 Therefore some of them of Jerusalem said, "Is not this he whom they seek to kill?
Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, “Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu?
26 Look, he speaks openly, and they say nothing to him. Can it be that the rulers indeed know that this is the Messiah?
Tazameni sasa! Anawaonya hadharani, wala hakuna mtu anayemwambia hata neno. Je, yawezekana kuwa viongozi wametambua kweli kwamba huyu ndiye Kristo?
27 However we know where this man comes from, but when the Messiah comes, no one will know where he comes from."
Kristo atakapokuja hakuna mtu atakayejua mahali alikotoka, lakini sisi tunajua alikotoka mtu huyu!”
28 Jesus therefore called out in the temple, teaching and saying, "You both know me, and know where I am from. I have not come of myself, but he who sent me is true, whom you do not know.
Basi, Yesu alipokuwa anafundisha Hekaluni alipaaza sauti na kusema, “Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui.
29 I know him, because I am from him, and he sent me."
Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.”
30 They sought therefore to take him; but no one laid a hand on him, because his hour had not yet come.
Basi, watu wakataka kumtia nguvuni, lakini hakuna mtu aliyethubutu kumkamata kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
31 But many in the crowd believed in him. They said, "When the Messiah comes, he won't do more signs than those which this man has done, will he?"
Wengi katika ule umati wa watu walimwamini, wakasema, “Je, Kristo akija atafanya ishara kubwa zaidi kuliko alizozifanya huyu?”
32 The Pharisees heard the crowd murmuring these things concerning him, and the chief priests and the Pharisees sent officers to arrest him.
Mafarisayo waliwasikia watu wakinong'ona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni.
33 Then Jesus said, "I will be with you a little while longer, then I go to him who sent me.
Yesu akasema, “Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma.
34 You will seek me, but won't find; and where I am, you cannot come."
Mtanitafuta lakini hamtaniona, maana pale nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika.”
35 The Jewish leaders therefore said among themselves, "Where will this man go that we won't find him? Will he go to the Diaspora among the Greeks, and teach the Greeks?
Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki?
36 What is this word that he said, 'You will seek me, but won't find; and where I am, you cannot come'?"
Ana maana gani anaposema: Mtanitafuta lakini hamtanipata, na mahali nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika?”
37 Now on the last and greatest day of the feast, Jesus stood and said in a loud voice, "If anyone is thirsty, let him come to me and drink.
Siku ya mwisho ya sikukuu hiyo ilikuwa siku maalum. Yesu alisimama, akasema kwa sauti kubwa, “Aliye na kiu na aje kwangu anywe.
38 He who believes in me, as the Scripture has said, from within him will flow rivers of living water."
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: Anayeniamini mimi, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka moyoni mwake!”
39 But he said this about the Spirit, which those believing in him were to receive. For the Spirit was not yet given, because Jesus was not yet glorified.
(Alisema hayo kumhusu Roho ambaye wale waliomwamini yeye watampokea. Wakati huo Roho alikuwa hajafika kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.)
40 Some of the crowd therefore, when they heard these words, said, "This is truly the Prophet."
Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, “Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!”
41 Others said, "This is the Messiah." But some said, "What, does the Messiah come out of Galilee?
Wengine wakasema, “Huyu ndiye Kristo!” Lakini wengine walisema, “Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?
42 Hasn't the Scripture said that the Messiah comes of the offspring of David, and from Bethlehem, the village where David was?"
Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!”
43 So there arose a division in the crowd because of him.
Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.
44 Some of them would have arrested him, but no one laid hands on him.
Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.
45 The officers therefore came to the chief priests and Pharisees, and they said to them, "Why did you not bring him?"
Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, “Kwa nini hamkumleta?”
46 The officers answered, "No man ever spoke like this man."
Walinzi wakawajibu, “Hakuna mtu aliyepata kamwe kusema kama asemavyo mtu huyu!”
47 The Pharisees therefore answered them, "You are not also led astray, are you?
Mafarisayo wakawauliza, “Je, nanyi pia mmedanganyika?
48 Have any of the rulers believed in him, or of the Pharisees?
Je, mmekwisha mwona hata mmoja wa viongozi wa watu, au mmoja wa Mafarisayo aliyemwamini?
49 But this crowd that does not know the Law is accursed."
Lakini umati huu haujui Sheria ya Mose; umelaaniwa!”
50 Nicodemus (he who came to him before, being one of them) said to them,
Mmoja wao alikuwa Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu. Basi, yeye akawaambia,
51 "Does our Law judge a man, unless it first hears from him personally and knows what he does?"
“Je, Sheria yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza na kujua anafanya nini?”
52 They answered him, "Are you also from Galilee? Search, and see that no prophet comes from Galilee."
Nao wakamjibu, “Je, wewe pia umetoka Galilaya? Haya, kayachunguze Maandiko Matakatifu nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki kamwe nabii!”
53 Then everyone went to his own house,
Basi, wote wakaondoka, kila mtu akaenda zake;

< Yochanan 7 >