< Ephesians 5 >

1 Be therefore imitators of God, as beloved children.
Kwa hiyo muwe watu wa kumfuata Mungu, kama watoto wake wapendwao.
2 And walk in love, even as Messiah also loved us, and gave himself up for us, an offering and a sacrifice to God for a sweet-smelling fragrance.
Mtembee katika pendo, vilevile kama Kristo alivyotupenda sisi, alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu. Yeye alikuwa sadaka na dhabihu, kuwa harufu nzuri ya kumfurahisha Mungu.
3 But sexual immorality, and all uncleanness, or covetousness, let it not even be mentioned among you, as becomes saints;
Zinaa au uchafu wowote na tamaa mbaya lazima visitajwe kati yenu, kama inavyotakiwa kwa waaminio,
4 nor filthiness, nor foolish talking, nor jesting, which are not appropriate; but rather giving of thanks.
wala machukizo yasitajwe, mazungumzo ya kipumbavu, au mizaha ya udhalilishaji, ambayo siyo sawa, badala yake iwepo shukrani.
5 Know this for sure, that no sexually immoral or impure or greedy person, that is, an idolater, has any inheritance in the Kingdom of Messiah and God.
Mnaweza kuwa na uhakika ya kwamba kuna zinaa, uchafu, wala atamaniye, huyo nimwabudu sanamu, hana urithi wowote katika ufalme wa Kristo na Mungu.
6 Let no one deceive you with empty words. For because of these things, the wrath of God comes on the children of disobedience.
Mtu yote asikudanganye kwa maneno matupu, kwa sababu ya mambo haya hasira ya Mungu inakuja juu ya wana wasiotii.
7 Therefore do not be partakers with them.
Hivyo usishiriki pamoja nao.
8 For you were once darkness, but are now light in the Lord. Walk as children of light,
Kwa kuwa ninyi mwanzo mlikuwa giza, lakini sasa mmekuwa nuru katika Bwana. Hivyo tembeeni kama watoto wa nuru.
9 for the fruit of the light is in all goodness and righteousness and truth,
Kwa kuwa matunda ya nuru yanajumuisha uzuri wote, haki na ukweli.
10 proving what is well pleasing to the Lord.
Tafuta kile kinacho furahisha kwa Bwana.
11 Have no fellowship with the unfruitful works of darkness, but rather even reprove them.
Usiwepo ushiriki katika kazi za giza zisizo na matunda, badala yake ziweke wazi.
12 For the things which are done by them in secret, it is a shame even to speak of.
Kwa sababu mambo yanayofanywa na wao sirini ni aibu sana hata kuyaelezea.
13 But all things, when they are reproved, are revealed by the light, for everything that reveals is light.
Mambo yote, yanapofichuliwa na nuru, huwa wazi,
14 Therefore he says, "Awake, you who sleep, and rise from the dead, and Messiah will shine on you."
kwa kuwa Kila kitu kilichofichuliwa kinakuwa nuruni. Hivyo husema hivi, “Amka, wewe uliyelala, na inuka kutoka wafu na Kristo atang'aa juu yako.”
15 Therefore watch carefully how you walk, not as unwise, but as wise;
Hivyo iweni makini jinsi mtembeavyo, siyo kama watu wasio werevu bali kama werevu.
16 redeeming the time, because the days are evil.
Ukomboeni muda kwa kuwa siku ni za uovu.
17 Therefore do not be foolish, but understand what the will of the Lord is.
Msiwe wajinga, badala yake, fahamuni nini mapenzi ya Bwana.
18 Do not get drunk with wine, which is debauchery, but be filled with the Spirit,
Msilewe kwa mvinyo, huongoza kwenye uharibifu, badala yake mjazwe na Roho Mtakatifu.
19 speaking to one another in psalms, hymns, and spiritual songs, singing and making music in your heart to the Lord;
Zungumzeni na kila mmoja wenu kwa zaburi, na sifa, na nyimbo za rohoni. Imbeni na sifuni kwa moyo kwa Bwana.
20 giving thanks always concerning all things in the name of our Lord Jesus (the) Messiah to God the Father;
Daima toa shukrani kwa mambo yote katika jina la Kristo Yesu Bwana wetu kwa Mungu Baba.
21 subjecting yourselves one to another in the fear of Messiah.
Jitoeni wenyewe kila mmoja kwa mwingine kwa heshima ya Kristo.
22 Wives, submit to your husbands as to the Lord.
Wake, jitoeni kwa waume zenu, kama kwa Bwana.
23 For the husband is the head of the wife, and Messiah also is the head of the church, being himself the savior of the body.
Kwa sababu mume ni kichwa cha mke, kama Kristo alivyo kichwa cha kanisa. Ni mwokozi wa mwili.
24 But as the church is subject to Messiah, so let the wives also be to their husbands in everything.
Lakini kama kanisa lilivyo chini ya Kristo, vilevile wake lazima wafanye hivyo kwa waume zao katika kila jambo.
25 Husbands, love your wives, even as Messiah also loved the church, and gave himself up for it;
Waume, wapendeni wake zenu kama vile Kristo alivyolipenda kanisa na akajitoa mwenyewe kwa ajili yake.
26 that he might sanctify it, having cleansed it by the washing of water with the word,
Alifanya hivyo ili liwe takatifu. Alilitakasa kwa kuliosha na maji katika neno.
27 that he might present the church to himself gloriously, not having spot or wrinkle or any such thing; but that it should be holy and without blemish.
Alifanya hivi ili kwamba aweze kujiwasilishia mwenyewe kanisa tukufu, pasipo na doa wala waa au kitu kifananacho na haya, badala yake ni takatifu lisilo na kosa.
28 Even so husbands also ought to love their own wives as their own bodies. He who loves his own wife loves himself.
Kwa njia ile ile, waume wanatakiwa kuwapenda wake zao kama miili yao. Yule ampendae mke wake anajipenda mwenyewe.
29 For no one ever hated his own flesh; but nourishes and cherishes it, even as Messiah also does the church;
Hakuna hata mmoja anayechukia mwili wake. Badala yake, huurutubisha na kuupenda, kama Kristo pia alivyolipenda kanisa.
30 because we are members of his body, of his flesh and of his bones.
Kwa kuwa sisi ni washiriki wa mwili wake.
31 "For this cause a man will leave his father and mother, and will be joined to his wife, and the two will become one flesh."
“Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na ataungana na mke wake, na hao wawili watakuwa mwili mmoja”.
32 This mystery is great, but I speak concerning Messiah and of the church.
huu ulikuwa umefichika. Lakini ninasema kuhusu Kristo na kanisa.
33 Nevertheless each of you must also love his own wife even as himself; and let the wife see that she respects her husband.
Walakini, kila mmoja wenu lazima ampende mke wake kama mwenyewe, na mke lazima amheshimu mumewe.

< Ephesians 5 >