< 1 Samuel 30 >

1 It happened, when David and his men had come to Ziklag on the third day, that Amalek had made a raid on the Negev, and on Ziklag, and had struck Ziklag, and burned it with fire,
Daudi na watu wake wakafika Siklagi siku ya tatu. Basi Waamaleki walikuwa wamevamia Negebu na Siklagi. Wakawa wameshambulia mji wa Siklagi na kuuteketeza kwa moto,
2 and had taken captive the women and all who were in it, both small and great. They did not kill any, but carried them off, and went their way.
nao wakawa wamewachukua mateka wanawake pamoja na wote waliokuwamo humo, vijana na wazee. Hawakuua yeyote, bali waliwachukua wakaenda zao.
3 When David and his men came to the city, look, it was burned with fire; and their wives, and their sons, and their daughters, were taken captive.
Daudi na watu wake walipofika Siklagi, wakakuta mji umeangamizwa kwa moto na wake zao pamoja na wana wao na binti zao wamechukuliwa mateka.
4 Then David and the people who were with him lifted up their voice and wept, until they had no more power to weep.
Hivyo Daudi na watu wake wakapiga yowe mpaka wakaishiwa na nguvu za kulia.
5 David's two wives were taken captive, Ahinoam the Jezreelite and Abigail the wife of Nabal the Carmelite.
Wake wawili wa Daudi walikuwa wametekwa: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
6 David was greatly distressed; for the people spoke of stoning him, because the soul of all the people was grieved, every man for his sons and for his daughters: but David strengthened himself in the LORD his God.
Daudi alihuzunika sana kwa sababu watu walikuwa wakisemezana juu ya kumpiga kwa mawe. Kila mmoja alikuwa na uchungu rohoni kwa sababu ya wanawe na binti zake. Lakini Daudi akajitia nguvu katika Bwana, Mungu wake.
7 David said to Abiathar the priest, the son of Ahimelech, "Please bring me here the ephod." Abiathar brought the ephod to David.
Kisha Daudi akamwambia kuhani Abiathari mwana wa Ahimeleki, “Niletee kisibau.” Abiathari akamletea,
8 David inquired of the LORD, saying, "If I pursue after this troop, shall I overtake them?" He answered him, "Pursue; for you shall surely overtake them, and shall without fail recover all."
naye Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nifuatie kundi hili la wavamizi? Je, nitawapata?” Bwana akajibu, “Wafuatie. Hakika utawapata na utafanikiwa kuwaokoa.”
9 So David went, he and the six hundred men who were with him, and came to the Wadi Besor, where those who were left behind stayed.
Daudi pamoja na watu wake 600 wakafika kwenye Bonde la Besori, mahali ambapo wengine waliachwa nyuma,
10 But David pursued, he and four hundred men; for two hundred stayed behind, who were so faint that they couldn't cross the Wadi Besor.
kwa kuwa watu 200 walikuwa wamechoka sana kuweza kuvuka hilo bonde. Lakini Daudi pamoja na watu 400 wakaendelea kufuatia.
11 They found an Egyptian in the field, and brought him to David, and gave him bread, and he ate; and they gave him water to drink.
Wakamkuta Mmisri katika shamba fulani, nao wakamleta kwa Daudi. Wakampa huyo Mmisri maji ya kunywa na chakula;
12 They gave him a piece of a cake of figs, and two clusters of raisins. When he had eaten, his spirit came again to him; for he had eaten no bread, nor drunk any water, three days and three nights.
kipande cha andazi la tini na andazi la zabibu zilizokaushwa. Akala naye akapata nguvu, kwa kuwa hakuwa amekula chakula chochote wala kunywa maji kwa siku tatu usiku na mchana.
13 David asked him, "To whom do you belong? Where are you from?" He said, "I am a young man of Egypt, servant to an Amalekite; and my master left me, because three days ago I fell sick.
Daudi akamuuliza, “Wewe ni wa nani, na umetoka wapi?” Akajibu, “Mimi ni Mmisri, mtumwa wa Mwamaleki. Bwana wangu alinitelekeza nilipougua siku tatu zilizopita.
14 We made a raid on the Negev of the Kerethites, and on that which belongs to Judah, and on the Negev of Caleb; and we burned Ziklag with fire."
Tulivamia Negebu ya Wakerethi, na nchi ya Yuda, na Negebu ya Kalebu. Nasi tulichoma moto Siklagi.”
15 David said to him, "Will you bring me down to this troop?" He said, "Swear to me by God that you will neither kill me, nor deliver me up into the hands of my master, and I will bring you down to this troop." And he swore to him.
Daudi akamuuliza, “Je, unaweza kuniongoza kufikia kundi hili la uvamizi?” Akajibu, “Niapie mbele ya Mungu kwamba hutaniua wala kunikabidhi mikononi mwa bwana wangu, nami nitakupeleka hadi waliko.”
16 When he had brought him down, look, they were spread around over all the ground, eating, drinking, and dancing, because of all the great spoil that they had taken out of the land of the Philistines, and out of the land of Judah.
Akamwongoza Daudi mpaka mahali walipokuwa, nao walikuwa wametawanyika eneo lote, wakila, wakinywa na wakifanya karamu kwa sababu ya nyara nyingi walizochukua kutoka nchi ya Wafilisti na kutoka Yuda.
17 David struck them from the twilight even to the evening of the next day and he put them to death. Not a man of them escaped from there, except four hundred young men, who rode on camels and fled.
Daudi akapigana nao kuanzia machweo ya jua hadi kesho yake jioni, na hakuna yeyote miongoni mwao aliyetoroka, isipokuwa vijana wanaume 400 waliopanda ngamia na kutoroka.
18 He recovered all that the Amalekites had taken; and David rescued his two wives.
Daudi akarudisha kila kitu Waamaleki walikuwa wamechukua, pamoja na wake zake wawili.
19 There was nothing lacking to them, neither small nor great, neither sons nor daughters, neither spoil, nor anything that they had taken to them. David brought back all.
Hakuna chochote kilichopotea: kijana au mzee, mvulana au msichana, nyara au kitu kingine chochote walichokuwa wamechukua. Daudi akarudisha kila kitu.
20 He took all the flocks and the herds, which they drove before those other livestock, and said, "This is David's spoil."
Akachukua makundi yote ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, nao watu wake wakawaswaga wanyama hao mbele ya wanyama wengine wa kufugwa, wakisema, “Hizi ni nyara za Daudi.”
21 David came to the two hundred men, who were so faint that they could not follow David, whom he also had made to stay at the Wadi Besor; and they went forth to meet David, and to meet the people who were with him. And when David came near to the people, he greeted them.
Kisha Daudi akafika kwa wale watu 200 waliokuwa wamechoka sana kumfuata na ambao waliachwa nyuma kwenye Bonde la Besori. Wakatoka kwenda kumlaki Daudi na wale watu aliokuwa nao. Daudi na watu wake walipowakaribia, akawasalimu.
22 Then every wicked and worthless one of the men who had gone with David answered, and they said, "Because they did not go with us, we will not give them anything of the spoil that we have recovered, except to each man his wife and his children. And let them take them, and depart."
Lakini watu wote waovu na wakorofi miongoni mwa wafuasi wa Daudi wakasema, “Kwa sababu hawakwenda pamoja nasi, hatutagawana nao nyara tulizorudisha. Lakini, kila mtu aweza kuchukua mkewe na watoto wake na kuondoka.”
23 Then David said, "You shall not do so after what the LORD has given to us, who has preserved us, and delivered into our hand the raiding party that came against us.
Daudi akajibu, “La hasha, ndugu zangu, kamwe hamwezi kufanya hivyo kwa kile ambacho Bwana ametupatia. Yeye ametulinda na kuweka mikononi mwetu majeshi yale yaliyokuja kupigana dhidi yetu.
24 So who will listen to you in this matter? For they are not inferior to you. For as his share is who goes down to the battle, so will his share be who remains with the supplies; they will share alike."
Ni nani atasikiliza yale mnayosema? Fungu la mtu aliyekaa na vyombo litakuwa sawa na la yule aliyekwenda vitani. Wote watashiriki sawa.”
25 It was so from that day forward, that he made it a statute and an ordinance for Israel to this day.
Daudi akafanya hili liwe amri na agizo kwa Israeli kutoka siku ile hata leo.
26 When David came to Ziklag, he sent of the spoil to the elders of Judah and to his friends, saying, "Look, a present for you of the spoil of the enemies of the LORD."
Daudi alipofika Siklagi, akatuma baadhi ya nyara kwa wazee wa Yuda, waliokuwa rafiki zake, akasema, “Tazama, hapa kuna zawadi kwa ajili yenu kutoka nyara za adui za Bwana.”
27 He sent it to those who were in Bethel, and to those who were in Ramath Negev, and to those who were in Jattir,
Akazituma kwa wale waliokuwa Betheli, Ramoth-Negebu na Yatiri;
28 and to those who were in Aroer, and to those who were in Siphmoth, and to those who were in Eshtemoa,
kwa wale walioko Aroeri, Sifmothi, Eshtemoa
29 and to those who were in Racal, and to those who were in the cities of the Jerahmeelites, and to those who were in the cities of the Kenizzites.
na Rakali; kwa wale waliokuwa katika miji ya Wayerameeli na ya Wakeni;
30 and to those who were in Hormah, and to those who were in Bor Ashan, and to those who were in Athach,
na kwa wale walioko Horma, Bori-Ashani, Athaki,
31 and to those who were in Hebron, and to all the places where David himself and his men used to stay.
na kwa wakazi wa Hebroni; na kwa wale waliokuwa mahali pengine pote ambako Daudi na watu wake walitembelea.

< 1 Samuel 30 >