< Luke 19 >

1 He entered and was passing through Jericho.
Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2 And look, there was a man named Zacchaeus. He was a chief tax collector, and he was rich.
Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 He was trying to see who Jesus was, and could not because of the crowd, because he was short.
Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4 He ran on ahead, and climbed up into a sycamore tree to see him, for he was to pass that way.
Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5 And as he came to the place, looking up, Jesus saw him, and said to him, "Zacchaeus, hurry and come down, for today I must stay at your house."
Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
6 He hurried, came down, and received him joyfully.
Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7 And when they saw it, they all murmured, saying, "He has gone in to lodge with a man who is a sinner."
Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
8 And Zacchaeus stood and said to the Lord, "Look, Lord, half of my goods I give to the poor. If I have wrongfully exacted anything of anyone, I restore four times as much."
Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
9 Jesus said to him, "Today, salvation has come to this house, because he also is a son of Abraham.
Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10 For the Son of Man came to seek and to save that which was lost."
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
11 As they heard these things, he went on and told a parable, because he was near Jerusalem, and they supposed that the kingdom of God would be revealed immediately.
Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12 He said therefore, "A certain nobleman went into a far country to receive for himself a kingdom, and to return.
Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13 He called ten servants of his, and gave them ten mina coins, and told them, 'Conduct business until I come.'
Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14 But his citizens hated him, and sent an envoy after him, saying, 'We do not want this man to reign over us.'
Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15 "It happened when he had come back again, having received the kingdom, that he commanded these servants, to whom he had given the money, to be called to him, that he might know what they had gained by conducting business.
“Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16 The first came before him, saying, 'Lord, your mina has made ten more minas.'
Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17 "And he said to him, 'Well done, good servant. Because you were faithful with very little, you will have authority over ten cities.'
Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18 "The second came, saying, 'Your mina, Lord, has made five minas.'
Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19 "So he said to him, 'And you are to be over five cities.'
Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20 Another came, saying, 'Lord, look, your mina, which I kept laid away in a handkerchief,
“Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21 for I feared you, because you are an exacting man. You take up that which you did not lay down, and reap that which you did not sow.'
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22 "He said to him, 'Out of your own mouth will I judge you, you wicked servant. You knew that I am an exacting man, taking up that which I did not lay down, and reaping that which I did not sow.
Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23 Then why did you not deposit my money in the bank, and at my coming, I might have earned interest on it?'
Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24 He said to those who stood by, 'Take the mina away from him, and give it to him who has the ten minas.'
Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25 "They said to him, 'Lord, he has ten minas.'
Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26 'For I tell you that to everyone who has, will more be given; but from him who does not have, even that which he has will be taken away.
Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 But bring those enemies of mine who did not want me to reign over them here, and kill them before me.'"
Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
28 Having said these things, he went on ahead, going up to Jerusalem.
Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29 It happened, when he drew near to Bethphage and Bethany, at the mountain that is called Olivet, he sent two of the disciples,
Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 saying, "Go your way into the village on the other side, in which, as you enter, you will find a colt tied, whereon no one ever yet sat. Untie it, and bring it.
akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31 If anyone asks you, 'Why are you untying it?' say to him: 'Because the Lord needs it.'"
Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
32 Those who were sent went away, and found things just as he had told them.
Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33 As they were untying the colt, its owners said to them, "Why are you untying the colt?"
Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34 They said, "Because the Lord needs it."
Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 They brought it to Jesus. They threw their cloaks on the colt, and set Jesus on them.
Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36 As he went, they spread their cloaks in the way.
Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 As he was now getting near, at the descent of the Mount of Olives, the whole crowd of the disciples began to rejoice and praise God with a loud voice for all the mighty works which they had seen,
Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38 saying, "Blessed is the King who comes in the name of the Lord. Peace in heaven, and glory in the highest."
wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39 Some of the Pharisees from the crowd said to him, "Teacher, rebuke your disciples."
Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
40 He answered them, "I tell you that if these were silent, the stones would cry out."
Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
41 When he drew near, he saw the city and wept over it,
Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42 saying, "If you, even you, had known today the things that make for peace. But now, they are hidden from your eyes.
akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 For the days will come on you, when your enemies will throw up a barricade against you, surround you, hem you in on every side,
Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44 and will dash you and your children within you to the ground. They will not leave in you one stone on another, because you did not know the time of your visitation."
Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
45 And he entered into the temple, and began to drive out those who were selling and buying in it,
Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46 saying to them, "It is written, 'And my house will be a house of prayer,' but you have made it a 'den of robbers'."
akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
47 He was teaching daily in the temple, but the chief priests and the scribes and the leaders among the people sought to destroy him.
Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48 They could not find what they might do, for all the people hung on to every word that he said.
lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

< Luke 19 >