< Genesis 16 >

1 Now Sarai, Abram's wife, bore him no children, but she had an Egyptian servant whose name was Hagar.
Kisha Sarai mke wa Abram, alikuwa hajamzalia mtoto, lakini alikuwa na mtumishi wa kike, Mmisri ambaye jina lake aliitwa Hajiri.
2 Sarai said to Abram, "Look now, God has prevented me from bearing. Please go in to my servant. It may be that I will obtain children by her." Abram listened to the voice of Sarai.
Kwa hiyo Sarai akamwambia Abram, “Tazama, Yahwe hajanifanya mimi kuwa na watoto. Nenda na ulale na mtumishi wangu. Ili kwamba niweze kupata watoto kupitia yeye.” Abram akasikiliza sauti ya Sarai.
3 So Sarai, Abram's wife, took Hagar the Egyptian, her servant, after Abram had lived ten years in the land of Canaan, and gave her to Abram her husband to be his wife.
Ilikuwa baada ya Abram kuishi miaka kumi katika nchi ya Kanaani ndipo Sarai, mke wa Abram, alimtoa Hajiri yule mmisri mtumishi wake kwa mume wake awe kama mke wake.
4 He slept with Hagar, and she conceived. When she saw that she had conceived, her mistress was despised in her eyes.
Kwa hiyo akawa na mahusiano na Hajiri, na akabeba mimba. Na alipoona kuwa amebeba mimba, akamdharau bibi yake.
5 Sarai said to Abram, "This wrong is your fault. I gave my servant into your bosom, and when she saw that she had conceived, she despised me. God judge between me and you."
Kisha Sarai akamwambia Abram, “Jambo hili baya kwangu ni kwa sababu yako. Nilimtoa mtumishi wangu wa kike katika kumbatio lako. Na alipoona kuwa amebeba mimba, nilidharaulika machoni pake. Na sasa acha Yahwe aamuwe kati yangu na wewe.”
6 But Abram said to Sarai, "Look, your servant is in your hand. Do to her whatever is good in your sight." Sarai dealt harshly with her, so she fled from her presence.
Lakini Abram akamwambia Sarai, “Tazama, hapa, mtumishi wako yuko katika uwezo wako, fanya unachofikiri ni kizuri sana kwake.” Kwa hiyo Sarai akakabiliana naye kwa ukatili, na akatoroka.
7 And the angel of God found her by a spring of water in the desert, by the spring on the way to Shur.
Malaika wa Yahwe akamkuta karibu na chemichemi ya maji katika jangwa, chemichemi iliyo katika njia kuelekea Shuri.
8 And he said, "Hagar, servant of Sarai, where did you come from, and where are you going?" And she said, "I am running away from the presence of my mistress Sarai."
Akasema, Hajiri, mtumishi wa Sarai, umetoka wapi na unakwenda wapi?” Na akasema, ninamtoroka bibi yangu Sarai.”
9 The angel of Jehovah said to her, "Return to your mistress, and submit yourself to her authority."
Malaika wa Yahwe akamwambia, “Rudi kwa bibi yako, na unyenyekee chini ya mamlaka yake.”
10 The angel of Jehovah said to her, "I will greatly multiply your descendants, so that they will be too numerous to count."
Kisha Malaika wa Yahwe akamwambia, “Nitazidisha uzao wako maradufu, kiasi kwamba watakuwa wengi wasioweza kuhesabika.”
11 Then the angel of God said to her, "Look, you are with child, and will bear a son. You are to name him Ishmael, because God has heard your affliction.
Malaika wa Yahwe pia akamwambia, “Tazama, wewe unamimba, na utazaa mtoto kiume, na utamwita jina lake Ishmaeli, kwasabab Yahwe amesikia mateso yako.
12 He will be like a wild donkey among men. His hand will be against every man, and every man's hand against him. And he will live away from all of his brothers."
Atakuwa punda mwitu wa mtu. Atakuwa adui dhidi ya kila mtu, na kila mtu atakuwa adui yake, na ataishi kando na ndugu zake wote.”
13 And she called his name, the one who spoke to her, "You are El Roi," for she said, "Here I have seen the one who sees me."
Kisha akamwita jina hili Yahwe aliye zungumza naye, “Wewe ni Mungu unionaye mimi,” kwa kuwa alisema, “je ninaendelea kweli kuona, hata baada ya kuwa ameniona?”
14 Therefore the well was called Beer Lahai Roi. Look, it is between Kadesh and Bered.
Kwa hiyo kisima kiliitwa Beerlahairori; Tazama, kiko kati ya Kadeshi na Beredi.
15 Hagar bore a son for Abram. Abram called the name of his son, whom Hagar bore, Ishmael.
Hajiri akamzalia Abram mwana wa kiume, na Abram akamwita mwanawe, ambaye Hajiri amemzaa jina, Ishmaeli.
16 Abram was eighty-six years old when Hagar bore Ishmael to Abram.
Abram alikuwa na umri wa miaka themanini na sita wakati Hajiri alipomzaa Ishmaeli kwa Abram.

< Genesis 16 >