< Genesis 16 >

1 Now Sarai, Abram's wife, bore him no children, but she had an Egyptian servant whose name was Hagar.
Basi Sarai, mkewe Abramu, alikuwa hajamzalia watoto. Lakini alikuwa na mtumishi wa kike Mmisri jina lake Hagari,
2 Sarai said to Abram, "Look now, God has prevented me from bearing. Please go in to my servant. It may be that I will obtain children by her." Abram listened to the voice of Sarai.
hivyo Sarai akamwambia Abramu, “Bwana amenizuilia kupata watoto. Nenda, ukakutane kimwili na mtumishi wangu wa kike, huenda nitaweza kupata watoto kupitia kwake.” Abramu akakubaliana na lile Sarai alilosema.
3 So Sarai, Abram's wife, took Hagar the Egyptian, her servant, after Abram had lived ten years in the land of Canaan, and gave her to Abram her husband to be his wife.
Hivyo baada ya Abramu kuishi katika nchi ya Kanaani miaka kumi, Sarai akamchukua mtumishi wake wa kike wa Kimisri, Hagari na kumpa mumewe awe mke wake.
4 He slept with Hagar, and she conceived. When she saw that she had conceived, her mistress was despised in her eyes.
Akakutana kimwili na Hagari, naye akapata mimba. Hagari alipojua kuwa ana mimba, alianza kumdharau Sarai.
5 Sarai said to Abram, "This wrong is your fault. I gave my servant into your bosom, and when she saw that she had conceived, she despised me. God judge between me and you."
Ndipo Sarai akamwambia Abramu, “Unawajibika na manyanyaso ninayoyapata. Nilimweka mtumishi wangu mikononi mwako, sasa kwa vile anajua kwamba ana mimba, ananidharau mimi. Bwana na aamue kati yako na mimi.”
6 But Abram said to Sarai, "Look, your servant is in your hand. Do to her whatever is good in your sight." Sarai dealt harshly with her, so she fled from her presence.
Abramu akamwambia, “Mtumishi wako yuko mikononi mwako. Mtendee lolote unalofikiri ni bora zaidi.” Ndipo Sarai akamtesa Hagari, hivyo akamtoroka.
7 And the angel of God found her by a spring of water in the desert, by the spring on the way to Shur.
Malaika wa Bwana akamkuta Hagari karibu na chemchemi huko jangwani; ilikuwa chemchemi ile iliyokuwa kando ya barabara iendayo Shuri.
8 And he said, "Hagar, servant of Sarai, where did you come from, and where are you going?" And she said, "I am running away from the presence of my mistress Sarai."
Malaika akamwambia, “Hagari, mtumishi wa Sarai, umetokea wapi, na unakwenda wapi?” Akamjibu, “Ninamkimbia bibi yangu Sarai.”
9 The angel of Jehovah said to her, "Return to your mistress, and submit yourself to her authority."
Ndipo malaika wa Bwana akamwambia, “Rudi kwa bibi yako ukajishushe chini yake.”
10 The angel of Jehovah said to her, "I will greatly multiply your descendants, so that they will be too numerous to count."
Malaika akaendelea akasema, “Nitazidisha wazao wako, hivi kwamba watakuwa wengi mno wasiohesabika.”
11 Then the angel of God said to her, "Look, you are with child, and will bear a son. You are to name him Ishmael, because God has heard your affliction.
Pia malaika wa Bwana akamwambia: “Wewe sasa una mimba nawe utamzaa mwana. Utamwita jina lake Ishmaeli, kwa sababu Bwana amesikia juu ya huzuni yako.
12 He will be like a wild donkey among men. His hand will be against every man, and every man's hand against him. And he will live away from all of his brothers."
Atakuwa punda-mwitu katikati ya wanadamu, mkono wake utakuwa dhidi ya kila mtu na mkono wa kila mtu dhidi yake, naye ataishi kwa uhasama na ndugu zake wote.”
13 And she called his name, the one who spoke to her, "You are El Roi," for she said, "Here I have seen the one who sees me."
Hagari akampa Bwana aliyezungumza naye jina hili: “Wewe ndiwe Mungu unionaye mimi,” kwa maana alisema, “Sasa nimemwona yeye anayeniona mimi.”
14 Therefore the well was called Beer Lahai Roi. Look, it is between Kadesh and Bered.
Ndiyo sababu kisima kile kikaitwa Beer-Lahai-Roi, ambacho bado kipo huko hata leo kati ya Kadeshi na Beredi.
15 Hagar bore a son for Abram. Abram called the name of his son, whom Hagar bore, Ishmael.
Hivyo Hagari akamzalia Abramu mwana, naye Abramu akamwita huyo mwana Hagari aliyemzalia, Ishmaeli.
16 Abram was eighty-six years old when Hagar bore Ishmael to Abram.
Abramu alikuwa na umri wa miaka themanini na sita wakati Hagari alipomzalia Ishmaeli.

< Genesis 16 >