< Galatians 1 >

1 Paul, an apostle (not from humans, nor through humans, but through Jesus Christ, and God the Father, who raised him from the dead),
Mimi ni Paulo mtume. Mimi sio mtume kutoka kwa wanadamu wala kupitia kwa mwanadamu, lakini kupitia kwa Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua kutoka kwa wafu.
2 and all the brothers who are with me, to the churches of Galatia:
Pamoja na ndugu wote na mimi, ninayaandikia makanisa ya Galatia.
3 Grace to you and peace from God our Father, and the Lord Jesus Christ,
Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo,
4 who gave himself for our sins, that he might deliver us out of this present evil age, according to the will of our God and Father— (aiōn g165)
aliyejitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu ili kwamba atukomboe na nyakati hizi za uovu, kutokana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba. (aiōn g165)
5 to whom be the glory forever and ever. Amen. (aiōn g165)
Kwake uwe utukufu milele na milele. (aiōn g165)
6 I am astonished that you are so quickly deserting him who called you by the grace of Christ to a different Good News;
Ninashangaa kwamba mnageukia haraka kwenye injili nyingine. Ninashangaa kwamba mnageukia mbali kutoka kwake yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo.
7 and there is not another Good News. Only there are some who trouble you, and want to pervert the Good News of Christ.
Hakuna injili nyingine, lakini kuna baadhi ya watu wanao wasababishieni nyinyi matatizo na kutaka kubadilisha injili ya Kristo.
8 But even though we, or an angel from heaven, should preach to you a Good News other than that which we preached to you, let him be cursed.
Lakini hata kama ni sisi au malaika kutoka mbinguni atatangaza kwenu injili tofauti na ile tuliyoitangaza kwenu, na alaaniwe.
9 As we have said before, so I now say again: if anyone preaches to you a Good News other than that which you received, let him be cursed.
Kama tulivyo sema mwanzoni, na sasa nasema tena, “Kama kuna mtu atawatangazia kwenu injili tofauti na mliyoipokea, na alaaniwe.”
10 For am I now seeking the favor of people, or of God? Or am I striving to please people? For if I were still pleasing people, I would not be a servant of Christ.
Kwani sasa hivi ninatafuta uthibitisho wa watu au Mungu? Ninatafuta kuwafurahisha wanadamu? Kama ninaendelea kujaribu kuwafurahisha wanadamu, mimi sio mtumishi wa Kristo.
11 But I make known to you, brothers, concerning the Good News which was preached by me, that it is not of human origin.
Ndugu, ninataka ninyi mjue kwamba injili niliyoitangaza haitokani na wanadamu.
12 For neither did I receive it from a human, nor was I taught it, but it came to me through revelation of Jesus Christ.
Sikuipokea kutoka kwa mtu, wala sikufundishwa. Badala yake, ilikuwa ni kwa ufunuo wa Yesu Kristo kwangu.
13 For you have heard of my former way of life in Judaism, how I severely persecuted the church of God, and tried to destroy it.
Mmekwisha sikia juu ya maisha yangu ya nyuma katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyokuwa nikilitesa kwa ukali kanisa la Mungu zaidi ya kipimo na kuliteketeza.
14 I advanced in Judaism beyond many of my own age among my countrymen, being more exceedingly zealous for the traditions of my fathers.
Nilikuwa nimeendelea katika Dini ya Kiyahudi zaidi ya ndugu zangu wengi Wayahudi. Nilikuwa na bidii sana katika tamaduni za baba zangu.
15 But when God, who had set me apart from my mother's womb and called me through his grace, was pleased
Lakini Mungu alipendezwa kunichagua mimi kutoka tumboni mwa mama. Aliniita mimi kupitia neema yake
16 to reveal his Son to me, that I might preach him among those who are not Jewish, I did not immediately confer with flesh and blood,
kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu, ili kwamba nimtangaze yeye miongoni mwa watu wa mataifa. Wala sikutafuta ushauri wa mwili na damu
17 nor did I go up to Jerusalem to those who were apostles before me, but I went away into Arabia. Then I returned to Damascus.
na sikupanda kwenda Yerusalem kwa wale waliokuwa mitume kabla yangu. Badala yake nilienda Uarabuni na baadae kurudi Damesiki.
18 Then after three years I went up to Jerusalem to see Cephas and get information from him, and stayed with him fifteen days.
Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kumtembelea Kefa, nikakaa naye kwa siku kumi na tano.
19 But of the other apostles I saw no one, except James, the Lord's brother.
Lakini sikuona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndungu yake na Bwana.
20 Now about the things which I write to you, look, before God, I'm not lying.
Tazama, mbele za Mungu, sidanganyi kwa kile niandikacho kwenu.
21 Then I came to the regions of Syria and Cilicia.
Kisha nilikwenda mikoa ya Shamu na Kilikia.
22 I was still unknown by face to the churches of Judea which were in Christ,
Sikuwa najulikana kwa macho kwa makanisa ya Uyahudi yale yaliyokuwa katika Kristo,
23 but they only heard: "He who once persecuted us now preaches the faith that he once tried to destroy."
lakini walikuwa wakisikia tu, “Yeye aliyekuwa akitutesa sasa anatangaza imani aliyokuwa akiiharibu.”
24 And they glorified God because of me.
Walikuwa wakimtukuza Mungu kwa ajili yangu.

< Galatians 1 >