< Ezekiel 43 >

1 Afterward he brought me to the gate, even the gate that looks toward the east.
Kisha yule mtu akanileta kwenye lango linaloelekea upande wa mashariki,
2 Look, the glory of the God of Israel came from the way of the east: and his voice was like the sound of many waters; and the earth shined with his glory.
nami nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka upande wa mashariki. Sauti yake ilikuwa kama ya ngurumo ya maji yaendayo kasi, nayo nchi ikangʼaa kwa utukufu wake.
3 It was according to the appearance of the vision which I saw, even according to the vision that I saw when I came to destroy the city; and the visions were like the vision that I saw by the river Chebar; and I fell on my face.
Maono niliyoyaona yalikuwa kama maono yale niliyokuwa nimeyaona wakati Mungu alipokuja kuangamiza mji na kama maono niliyokuwa nimeyaona kando ya Mto wa Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
4 The glory of Jehovah came into the house by the way of the gate whose prospect is toward the east.
Utukufu wa Bwana ukaingia hekaluni kwa kupitia lango linaloelekea upande wa mashariki.
5 The Spirit took me up, and brought me into the inner court; and look, the glory of Jehovah filled the house.
Kisha Roho akanichukua na kunileta katika ule ua wa ndani, nao utukufu wa Bwana ulilijaza Hekalu.
6 I heard one speaking to me out of the house; and a man stood by me.
Wakati yule mtu akiwa amesimama kando yangu, nilisikia mtu mmoja akisema nami kutoka ndani ya Hekalu.
7 He said to me, "Son of man, this is the place of my throne, and the place of the soles of my feet, where I will dwell in the midst of the children of Israel forever. The house of Israel shall no more defile my holy name, neither they, nor their kings, by their prostitution, and by the dead bodies of their kings in their high places;
Akasema, “Mwanadamu, hapa ni mahali pa kiti changu cha enzi na mahali pa kuweka nyayo za miguu yangu. Hapa ndipo nitakapoishi miongoni mwa Waisraeli milele. Kamwe nyumba ya Israeli hawatalinajisi tena Jina langu takatifu, yaani, wao wala wafalme wao, kwa ukahaba wao na kwa sanamu zao zisizokuwa na uhai za wafalme wao katika mahali pao pa juu pa kuabudia miungu.
8 in their setting of their threshold by my threshold, and their doorpost beside my doorpost, and there was but the wall between me and them; and they have defiled my holy name by their abominations which they have committed: therefore I have consumed them in my anger.
Walipoweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu na miimo yao ya milango karibu na miimo yangu, pakiwa na ukuta tu kati yangu na wao, walilinajisi Jina langu takatifu kwa matendo yao ya machukizo. Kwa sababu hiyo niliwaangamiza kwa hasira yangu.
9 Now let them put away their prostitution, and the dead bodies of their kings, far from me; and I will dwell in their midst forever.
Basi sasa na waweke mbali nami ukahaba wao na sanamu za wafalme wao zisizo na uhai, nami nitakaa miongoni mwao milele.
10 "You, son of man, show the house to the house of Israel, that they may be ashamed of their iniquities; and let them measure the pattern.
“Mwanadamu, elezea hilo Hekalu kwa watu wa Israeli, ili wapate kuona aibu kwa ajili ya dhambi zao. Wao na wapime hicho kielelezo.
11 If they be ashamed of all that they have done, make known to them the form of the house, and its fashion, and its exits, and its entrances, and all its forms, and all its ordinances, and all its forms, and all its laws; and write it in their sight; that they may keep the whole form of it, and all its ordinances, and do them.
Wakishaona aibu kwa ajili ya yale yote waliyotenda, wafahamishe kielelezo cha hilo Hekalu, yaani mpangilio wake, maingilio yake ya kutoka na kuingia, kielelezo chake chote, na masharti yake yote na sheria zake zote. Yaandike haya mbele yao ili wapate kuwa waaminifu kwa hicho kielelezo chake na kufuata masharti yake yote.
12 "This is the law of the house: on the top of the mountain the whole limit around it shall be most holy. Look, this is the law of the house.
“Hii ndiyo sheria ya Hekalu: Eneo lote linalozunguka Hekalu juu ya mlima litakuwa takatifu kuliko yote. Hii ndiyo sheria ya Hekalu.
13 "These are the measurements of the altar by units of length (each unit is the standard eighteen inches plus three inches): the bottom shall be twenty-one inches, and the breadth twenty-one inches, and its border around its edge nine inches. And this shall be the height of the altar:
“Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa dhiraa ndefu, yaani, dhiraa moja na nyanda nne: Tako lake liwe na kina cha hiyo dhiraa moja na upana wa hiyo dhiraa moja, ikiwa na ukingo wa shibiri moja kuizunguka pembeni. Hiki kitakuwa ndicho kimo cha madhabahu:
14 from the bottom on the ground to the lower ledge shall be three feet five inches, and the breadth twenty-one inches; and from the lesser ledge to the greater ledge shall be six feet eleven inches, and the breadth twenty-one inches.
Kimo cha msingi kuanzia usawa wa ardhi mpaka kwenye mfereji sehemu ya chini kimo chake ni dhiraa mbili na upana wake ni dhiraa moja na kuanzia kwenye ukingo mdogo hadi kwenye ukingo mpana kimo chake ni dhiraa nne na upana wake ni dhiraa moja.
15 The upper altar shall be six feet eleven inches; and four horns project upward from the altar hearth.
Pale pawashwapo moto madhabahuni kimo chake kitakuwa dhiraa nne, na pembe nne zinazoelekeza juu kutoka pale pawashwapo moto.
16 The altar hearth shall be twenty-four feet one inch long by twenty-four feet one inch broad, square in the four sides of it.
Pale pawashwapo moto pa madhabahu ni mraba, urefu wake ni dhiraa kumi na mbili na upana wa dhiraa kumi na mbili.
17 The ledge shall be twenty-four feet one inch long by twenty-four feet one inch broad in the four sides of it; and the border about it shall be ten and a half inches; and its bottom shall be twenty-one inches around; and its steps shall look toward the east."
Pia sehemu ya juu ni mraba, urefu wake dhiraa kumi na nne na upana wa dhiraa kumi na nne, ikiwa na ukingo wa nusu dhiraa na mfereji kuizunguka madhabahu. Ngazi za kupandia madhabahuni zitaelekea upande wa mashariki.”
18 He said to me, "Son of man, thus says Jehovah: These are the ordinances of the altar in the day when they shall make it, to offer burnt offerings thereon, and to sprinkle blood thereon.
Kisha akaniambia, “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Haya ndiyo yatakayokuwa masharti ya kutoa dhabihu za kuteketezwa na kunyunyiza damu juu ya madhabahu itakapokuwa imejengwa.
19 You shall give to the priests the Levites who are of the offspring of Zadok, who are near to me, to minister to me, says Jehovah, a young bull for a sin offering.
Utatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi kwa makuhani, ambao ni Walawi, wa jamaa ya Sadoki, ndio watakaonikaribia kuhudumu mbele zangu, asema Bwana Mwenyezi.
20 You shall take of its blood, and put it on the four horns of it, and on the four corners of the ledge, and on the border all around: thus you shall cleanse it and make atonement for it.
Itakupasa kuchukua baadhi ya hiyo damu ya mnyama huyo na kuiweka juu ya hizo pembe nne za madhabahu na juu ya ncha zake nne za sehemu ya juu kuzunguka ukingo wote, ili kuitakasa madhabahu na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
21 You shall also take the bull of the sin offering, and it shall be burnt in the appointed place of the house, outside of the sanctuary.
Itakupasa kumchukua huyo fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi na kumteketeza mahali palipoagizwa katika eneo la Hekalu nje ya mahali Patakatifu.
22 "On the second day you shall offer a male goat without blemish for a sin offering; and they shall cleanse the altar, as they cleansed it with the bull.
“Siku ya pili yake utamtoa beberu asiye na dosari kwa ajili ya sadaka ya dhambi, nayo madhabahu itatakaswa kama ilivyotakaswa kwa yule fahali.
23 When you have finished cleansing it, you shall offer a young bull without blemish, and a ram out of the flock without blemish.
Utakapokuwa umemaliza kazi ya kuitakasa, utamtoa fahali mchanga pamoja na kondoo dume toka kwenye kundi, wote wawe hawana dosari.
24 You shall bring them near to Jehovah, and the priests shall cast salt on them, and they shall offer them up for a burnt offering to Jehovah.
Utawatoa mbele za Bwana, nao makuhani watanyunyizia chumvi juu yao na kuwatoa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
25 "Seven days you shall prepare every day a goat for a sin offering: they shall also prepare a young bull, and a ram out of the flock, without blemish.
“Kwa siku saba itakupasa kutoa beberu kila siku kwa ajili ya sadaka ya dhambi, pia itakupasa kutoa fahali mchanga na kondoo dume kutoka zizini, wote wawe hawana dosari.
26 Seven days shall they make atonement for the altar and purify it; so shall they consecrate it.
Kwa siku saba itawapasa kufanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuitakasa na hivyo ndivyo watakavyoiweka wakfu.
27 When they have accomplished the days, it shall be that on the eighth day, and forward, the priests shall make your burnt offerings on the altar, and your peace offerings; and I will accept you, says Jehovah."
Mwishoni mwa hizi siku saba, kuanzia siku ya nane na kuendelea, itawapasa makuhani kutoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za amani juu ya madhabahu. Kisha nitawakubali ninyi, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ezekiel 43 >