< 2 Kings 12 >

1 In the seventh year of Jehu began Jehoash to reign; and he reigned forty years in Jerusalem: and his mother's name was Zibiah of Beersheba.
Katika mwaka wa saba wa utawala wa Yehu, Yoashi alianza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka arobaini. Jina la mama yake aliitwa Sibia, kutoka Beer-Sheba.
2 Jehoash did that which was right in the eyes of Jehovah all his days in which Jehoiada the priest instructed him.
Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ambayo Yehoyada kuhani alikuwa akimwelekeza.
3 However the high places were not taken away; the people still sacrificed and burnt incense in the high places.
Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
4 Jehoash said to the priests, "All the money of the holy things that is brought into the house of Jehovah, in current money, the money of the persons for whom each man is rated, and all the money that it comes into any man's heart to bring into the house of Jehovah,
Yoashi akawaambia makuhani, “Kusanyeni fedha zote ambazo zitaletwa kama sadaka takatifu kwenye Hekalu la Bwana, yaani fedha zilizokusanywa kama kodi, fedha zilizopokelewa kutokana na nadhiri za watu binafsi, na fedha zilizoletwa kwa hiari hekaluni.
5 let the priests take it to them, every man from his acquaintance; and they shall repair the breaches of the house, wherever any breach shall be found."
Kila kuhani na apokee fedha kutoka kwa mmoja wa watunza hazina, nazo zitumike kukarabati uharibifu wowote unaoonekana katika Hekalu.”
6 But it was so, that in the three and twentieth year of king Jehoash the priests had not repaired the breaches of the house.
Lakini ikawa kufikia mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake Mfalme Yoashi, makuhani walikuwa bado hawajalikarabati Hekalu.
7 Then king Jehoash called for Jehoiada the priest, and for the other priests, and said to them, "Why do you not repair the breaches of the house? Now therefore take no more money from your treasurers, but deliver it for the breaches of the house."
Kwa hiyo Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na makuhani wengine, akawauliza, “Kwa nini hamtengenezi uharibifu uliofanyika hekaluni? Msichukue fedha zaidi kutoka kwa watunza hazina wenu kwa ajili ya matumizi yenu, lakini kuanzia sasa ni lazima fedha yote itumike kwa ajili ya kukarabati Hekalu.”
8 The priests consented that they should take no more money from the people, neither repair the breaches of the house.
Makuhani wakakubali kuwa hawatakusanya tena fedha kutoka kwa watu na kwamba hawatakarabati Hekalu wenyewe.
9 But Jehoiada the priest took a chest, and bored a hole in its lid, and set it beside the altar, on the right side as one comes into the house of Jehovah: and the priests who kept the threshold put in it all the money that was brought into the house of Jehovah.
Yehoyada kuhani akachukua kisanduku na akatoboa tundu kwenye kifuniko chake. Akakiweka kando ya madhabahu upande wa kulia unapoingia hekaluni mwa Bwana. Makuhani waliolinda ingilio wakaweka ndani ya kisanduku fedha zote ambazo zililetwa katika Hekalu la Bwana.
10 It was so, when they saw that there was much money in the chest, that the king's scribe and the high priest came up, and they put up in bags and counted the money that was found in the house of Jehovah.
Kila mara walipoona kuwa kuna kiasi kikubwa cha fedha ndani ya kisanduku, mwandishi wa mfalme na kuhani mkuu walikuja, wakazihesabu fedha hizo zilizoletwa katika Hekalu la Bwana, na kuziweka katika mifuko.
11 They gave the money that was weighed out into the hands of those who did the work, who had the oversight of the house of Jehovah: and they paid it out to the carpenters and the builders, who worked on the house of Jehovah,
Wakiisha kuthibitisha kiasi cha hizo fedha, waliwapa watu walioteuliwa kusimamia kazi katika Hekalu. Kwa fedha hizo, wakawalipa wale watu waliofanya kazi katika Hekalu la Bwana: yaani, maseremala na wajenzi,
12 and to the masons and the stone cutters, and for buying timber and cut stone to repair the breaches of the house of Jehovah, and for all that was laid out for the house to repair it.
waashi na wakata mawe. Walinunua mbao na mawe ya kuchongwa kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana, na kulipia gharama nyingine zote za kulitengeneza.
13 But there were not made for the house of Jehovah cups of silver, snuffers, basins, trumpets, any vessels of gold, or vessels of silver, of the money that was brought into the house of Jehovah;
Fedha zilizoletwa kwenye Hekalu hazikutumiwa kutengenezea masinia ya fedha, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, tarumbeta wala vyombo vingine vyovyote vya dhahabu au fedha kwa ajili ya Hekalu la Bwana;
14 for they gave that to those who did the work, and repaired therewith the house of Jehovah.
zililipwa kwa wafanyakazi, ambao walizitumia kwa kukarabati Hekalu.
15 Moreover they did not demand an accounting from the men into whose hand they delivered the money to give to those who did the work; for they dealt faithfully.
Wao hawakudai kupewa hesabu ya fedha kutoka kwa wale waliowapa ili kuwalipa wafanyakazi, kwa sababu walifanya kwa uaminifu wote.
16 The money for the trespass offerings, and the money for the sin offerings, was not brought into the house of Jehovah: it was the priests'.
Fedha zilizopatikana kutokana na sadaka za hatia na sadaka za dhambi hazikuletwa katika Hekalu la Bwana; zilikuwa mali ya makuhani.
17 Then Hazael king of Aram went up, and fought against Gath, and took it; and Hazael set his face to go up to Jerusalem.
Wakati huu Hazaeli mfalme wa Aramu akapanda kuishambulia Gathi, akaiteka. Kisha akageuka ili kuishambulia Yerusalemu.
18 Jehoash king of Judah took all the holy things that Jehoshaphat and Jehoram and Ahaziah, his fathers, kings of Judah, had dedicated, and his own holy things, and all the gold that was found in the treasures of the house of Jehovah, and of the king's house, and sent it to Hazael king of Aram: and he went away from Jerusalem.
Lakini Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vyombo vyote vitakatifu vilivyowekwa wakfu na baba zake, yaani Yehoshafati, Yehoramu na Ahazia, wafalme wa Yuda, zawadi ambazo yeye mwenyewe alikuwa ameziweka wakfu pamoja na dhahabu yote iliyokutwa katika hazina za Hekalu la Bwana na katika jumba la kifalme, akazipeleka kwa Hazaeli mfalme wa Aramu, ambaye hatimaye aliondoka Yerusalemu.
19 Now the rest of the acts of Joash, and all that he did, aren't they written in the book of the chronicles of the kings of Judah?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yoashi na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
20 His servants arose, and made a conspiracy, and struck Joash at the house of Millo, on the way that goes down to Silla.
Maafisa wake wakafanya shauri baya dhidi yake, nao wakamuulia Yoashi huko Beth-Milo, kwenye barabara iteremkayo kuelekea Sila.
21 For Jozabad the son of Shimeath, and Jehozabad the son of Shomer, his servants, struck him, and he died; and they buried him with his fathers in the City of David: and Amaziah his son reigned in his place.
Maafisa waliomuua walikuwa Yozabadi mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri. Akafa na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi. Naye Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Kings 12 >