< 1 Samuel 15 >

1 Samuel said to Saul, "Jehovah sent me to anoint you to be king over his people, over Israel. Now therefore listen to the voice of the words of Jehovah.
Samweli akamwambia Sauli, “Mimi ndiye ambaye Bwana alinituma nikutie mafuta uwe mfalme juu ya watu wake Israeli, basi sasa sikiliza ujumbe kutoka kwa Bwana.
2 Thus says Jehovah of hosts, 'I will punish Amalek for what he did to Israel, how he set himself against him in the way, when he came up out of Egypt.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nitawaadhibu Waamaleki kwa kile walichowatendea Israeli walipowavizia wakati walipanda kutoka Misri.
3 Now go and strike Amalek, and utterly destroy all that they have, and do not spare them; but kill both man and woman, infant and nursing baby, ox and sheep, camel and donkey.'"
Basi sasa nenda ukawashambulie Waamaleki na kuwaangamiza kabisa pamoja na kila kitu kilicho mali yao. Usiwahurumie; waue wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao, ngʼombe na kondoo, ngamia na punda.’”
4 Saul summoned the people, and numbered them in Telaim, two hundred thousand footmen, and ten thousand men of Judah.
Ndipo Sauli akawaita watu na kuwapanga huko Telaimu, askari wa miguu 200,000 pamoja na watu 10,000 kutoka Yuda.
5 Saul came to the city of Amalek, and lay in wait in the valley.
Sauli akaenda katika mji wa Amaleki na kuwavizia bondeni.
6 Saul said to the Kenites, "Go, depart, go down from among the Amalekites, lest I sweep you away with them; for you showed kindness to all the children of Israel, when they came up out of Egypt." So the Kenites departed from among the Amalekites.
Kisha akawaambia Wakeni, “Ondokeni, waacheni Waamaleki ili nisije nikawaangamiza ninyi pamoja nao, kwa kuwa ninyi mliwatendea mema Waisraeli wote wakati walipanda kutoka Misri.” Basi Wakeni wakaondoka, wakawaacha Waamaleki.
7 Saul struck the Amalekites, from Havilah as you go to Shur, that is before Egypt.
Ndipo Sauli akawashambulia Waamaleki toka Havila mpaka Shuri, hadi mashariki ya Misri.
8 He took Agag the king of the Amalekites alive, and utterly destroyed all the people with the edge of the sword.
Akamchukua Agagi, mfalme wa Waamaleki akiwa hai, nao watu wake wote akawaangamiza kabisa kwa upanga.
9 But Saul and the people spared Agag, and the best of the sheep, and the cattle, and the fat ones and the lambs, and all that was good, and wouldn't utterly destroy them; but everything that was despised and rejected, that they utterly destroyed.
Lakini Sauli na hilo jeshi wakamhifadhi hai Agagi na kondoo na ngʼombe walio wazuri, mafahali na wana-kondoo walionona kila kitu kilichokuwa kizuri. Hivi vitu hawakuwa radhi kuviangamiza kabisa, bali kila kitu kilichodharauliwa na kilicho dhaifu wakakiangamiza kabisa.
10 Then the word of Jehovah came to Samuel, saying,
Kisha neno la Bwana likamjia Samweli kusema:
11 "It grieves me that I have made Saul king; for he has turned back from following me, and has not carried out my commandments." And Samuel was angry; and he cried to Jehovah all night.
“Ninasikitika kwamba nimemfanya Sauli kuwa mfalme, kwa sababu ameacha kunifuata mimi na hakutimiza maagizo yangu.” Samweli akafadhaika, naye akamlilia Bwana usiku ule wote.
12 And Samuel rose early to meet Saul in the morning; and it was told Samuel, saying, "Saul came to Carmel, and look, he set up a monument for himself, and turned, and passed on, and went down to Gilgal." And Samuel came to Saul, and look, he was offering up a burnt offering to Jehovah, the best of the spoils which he had brought from Amalek.
Asubuhi na mapema Samweli akaamka kwenda kukutana na Sauli, lakini akaambiwa, “Sauli amekwenda Karmeli. Huko amesimamisha mnara kwa heshima yake mwenyewe naye ameendelea na kuteremkia Gilgali.”
13 And Samuel came to Saul; and Saul said to him, "You are blessed by Jehovah. I have performed the commandment of Jehovah."
Samweli alipomfikia, Sauli akamwambia, “Bwana akubariki! Nimetimiza yale Bwana aliniagiza.”
14 Samuel said, "Then what does this bleating of the sheep in my ears, and the lowing of the cattle which I hear mean?"
Lakini Samweli akasema, “Nini basi huu mlio wa kondoo masikioni mwangu? Huu mlio wa ngʼombe ninaousikia ni kitu gani?”
15 And Saul said, "I have brought them from Amalek; for the people spared the best of the sheep and the cattle to sacrifice to Jehovah your God, and I have utterly destroyed the rest."
Sauli akajibu, “Askari wamewaleta kutoka kwa Waamaleki, waliwaacha wale kondoo na ngʼombe wazuri ili kuwatoa dhabihu kwa Bwana, Mungu wako, lakini tuliwaangamiza kabisa wengine wote.”
16 Then Samuel said to Saul, "Stay, and I will tell you what Jehovah has said to me last night." He said to him, "Say on."
Samweli akamwambia Sauli, “Ngoja! Nami nitakuambia lile Bwana aliloniambia usiku huu.” Sauli akajibu, “Niambie.”
17 Samuel said, "Though you were little in your own sight, weren't you made the head of the tribes of Israel? Jehovah anointed you king over Israel;
Samweli akamwambia, “Ingawa zamani ulijiona mdogo machoni pako mwenyewe, Je, hukuwa kiongozi wa kabila za Israeli? Bwana alikutia mafuta kuwa mfalme juu ya Israeli.
18 and Jehovah sent you on a journey, and said to you, 'Go, and utterly destroy the sinners the Amalekites, and fight against them until you have destroyed them.'
Naye akakutuma kwa kazi maalum, akisema, ‘Nenda ukaangamize kabisa wale watu waovu, wale Waamaleki, upigane nao vita mpaka utakapowaangamiza kabisa.’
19 Why then did you not obey the voice of Jehovah, but took the spoils, and did that which was evil in the sight of Jehovah?"
Kwa nini hukumtii Bwana? Kwa nini ulivamia nyara na kufanya uovu machoni pa Bwana?”
20 Saul said to Samuel, "But I have obeyed the voice of Jehovah, and have gone the way which Jehovah sent me, and have brought Agag the king of Amalek, and have utterly destroyed the Amalekites.
Sauli akasema, “Lakini nilimtii Bwana. Nilikamilisha ile kazi ambayo Bwana alinituma. Niliwaangamiza Waamaleki kabisa na kumleta Agagi mfalme wao.
21 But the people took of the spoil, sheep and cattle, the chief of the devoted things, to sacrifice to Jehovah your God in Gilgal."
Askari walichukua kondoo na ngʼombe kutoka kwenye nyara, zile ambazo ni nzuri sana zimewekwa wakfu kwa Mungu, ili zitolewe dhabihu kwa Bwana Mungu wako huko Gilgali.”
22 Samuel said, "Has Jehovah as great delight in burnt offerings and sacrifices, as in obeying the voice of Jehovah? Look, to obey is better than sacrifice, and to listen than the fat of rams.
Lakini Samweli akajibu: “Je, Bwana anafurahia sadaka za kuteketezwa na dhabihu kama vile kuitii sauti ya Bwana? Kutii ni bora zaidi kuliko dhabihu, nako kusikia ni bora kuliko mafuta ya kondoo dume.
23 For rebellion is as the sin of witchcraft, and stubbornness is as idolatry and teraphim. Because you have rejected the word of Jehovah, he has also rejected you from being king."
Kwa maana kuasi ni kama dhambi ya uaguzi, nao ukaidi ni kama uovu wa kuabudu sanamu. Kwa sababu umelikataa neno la Bwana, naye amekukataa wewe kuendelea kuwa mfalme.”
24 Saul said to Samuel, "I have sinned; for I have transgressed the commandment of Jehovah, and your words, because I feared the people, and obeyed their voice.
Ndipo Sauli akamwambia Samweli, “Nimetenda dhambi. Nimevunja amri ya Bwana na maagizo yako. Niliwaogopa watu na kwa hiyo nikafanya walivyotaka.
25 Now therefore, please pardon my sin, and turn again with me, that I may worship Jehovah."
Sasa ninakusihi usamehe dhambi yangu, nawe urudi pamoja nami, ili nipate kumwabudu Bwana.”
26 Samuel said to Saul, "I will not return with you; for you have rejected the word of Jehovah, and Jehovah has rejected you from being king over Israel."
Lakini Samweli akamwambia, “Sitarudi pamoja nawe. Umelikataa neno la Bwana, naye Bwana amekukataa wewe, usiendelee kuwa mfalme juu ya Israeli!”
27 As Samuel turned about to go away, he grabbed the skirt of his robe, and it tore.
Samweli alipogeuka ili aondoke, Sauli akangʼangʼania pindo la joho lake, nalo likararuka.
28 Samuel said to him, "Jehovah has torn the kingdom of Israel from you this day, and has given it to a neighbor of yours who is better than you.
Samweli akamwambia, “Bwana ameurarua ufalme wa Israeli kutoka kwako leo, naye ameutia kwa mmoja wa majirani zako, aliye bora kuliko wewe.
29 And also the Eternal One of Israel will not retract or change his mind; for he is not a man that he should change his mind."
Yeye aliye Utukufu wa Israeli hasemi uongo wala hana kigeugeu; kwa kuwa yeye si mwanadamu, hata abadili nia yake.”
30 Then he said, "I have sinned: yet please honor me now before the elders of my people, and before Israel, and come back with me, that I may worship Jehovah your God."
Sauli akajibu, “Nimetenda dhambi. Lakini tafadhali niheshimu mbele ya wazee wa watu wangu na mbele ya Israeli; rudi pamoja nami, ili nipate kumwabudu Bwana Mungu wako.”
31 So Samuel went back with Saul; and he worshiped Jehovah.
Hivyo Samweli akarudi pamoja na Sauli, naye Sauli akamwabudu Bwana.
32 Then Samuel said, "Bring here to me Agag the king of the Amalekites." And Agag came to him trembling. And Agag said, "Surely death is bitter."
Ndipo Samweli akasema, “Niletee Agagi mfalme wa Waamaleki.” Agagi akaja kwake kwa ujasiri, akifikiri, “Hakika uchungu wa mauti umepita.”
33 Samuel said, "As your sword has made women childless, so your mother will be childless among women." Samuel cut Agag in pieces before Jehovah in Gilgal.
Lakini Samweli akasema, “Kama upanga wako ulivyofanya wanawake kufiwa na watoto wao, ndivyo mama yako atakavyokuwa hana mtoto miongoni mwa wanawake.” Naye Samweli akamuua Agagi mbele za Bwana huko Gilgali.
34 Then Samuel went to Ramah; and Saul went up to his house to Gibeah of Saul.
Kisha Samweli akaenda Rama, lakini Sauli akapanda nyumbani kwake huko Gibea ya Sauli.
35 And Samuel did not see Saul again until the day of his death; for Samuel mourned for Saul. And Jehovah grieved that he had made Saul king over Israel.
Hadi siku Samweli alipofariki hakwenda kumwona Sauli tena, ingawa Samweli alimwombolezea. Naye Bwana alihuzunika kwamba alimfanya Sauli kuwa mfalme juu ya Israeli.

< 1 Samuel 15 >