< Luke 4 >

1 Yeshua, full of the Rukha d'Qudsha, returned from the Yurdinan, and was led by the Rukha into the wilderness
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2 for forty days, being tempted by the devil. He ate nothing in those days. When they were completed, he was hungry.
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 The devil said to him, "If you are the Son of God, command this stone to become bread."
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 Yeshua answered him, saying, "It is written, 'Humankind cannot live by bread alone.'"
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 And leading him up to a high mountain, the devil showed him all the kingdoms of the world in a moment of time.
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 The devil said to him, "I will give you all this authority, and their glory, for it has been delivered to me; and I give it to whomever I want.
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 If you therefore will worship before me, it will all be yours."
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 Yeshua answered and said to him, "It is written, 'You are to worship the Lord your God, and serve him only.'"
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 He led him to Urishlim, and set him on the pinnacle of the temple, and said to him, "If you are the Son of God, cast yourself down from here,
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 for it is written, 'He will put his angels in charge of you, to guard you;'
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 and, 'On their hands they will bear you up, lest perhaps you dash your foot against a stone.'"
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 And Yeshua, answering, said to him, "It is said, 'Do not test the Lord your God.'"
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 When the devil had completed every temptation, he departed from him until another time.
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 Yeshua returned in the power of the Rukha into Galila, and news about him spread through all the surrounding area.
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 He taught in their synagogues, being praised by all.
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 He came to Natsrath, where he had been brought up. He entered, as was his custom, into the synagogue on the Sabbath day, and stood up to read.
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17 The scroll of the prophet Eshaya was handed to him, and unrolling the scroll, he found the place where it was written,
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 "The Rukha of the Lord is upon me, because he has anointed me to preach good news to the poor. He has sent me to heal the brokenhearted, to proclaim liberty to the captives, recovering of sight to the blind, to deliver those who are crushed,
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19 and to proclaim the acceptable year of the Lord."
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 He closed the scroll, gave it back to the attendant, and sat down. The eyes of all in the synagogue were fastened on him.
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 He began to tell them, "Today, this Scripture has been fulfilled in your hearing."
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 All testified about him, and wondered at the gracious words which proceeded out of his mouth, and they said, "Is not this Yauseph's son?"
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 He said to them, "Doubtless you will tell me this parable, 'Physician, heal yourself. Whatever we have heard done at Kepharnakhum, do also here in your hometown.'"
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 He said, "Truly I tell you, no prophet is acceptable in his hometown.
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 But truly I tell you, there were many widows in Israyel in the days of Eliya, when the sky was shut up three years and six months, when a great famine came over all the land.
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 Eliya was sent to none of them, except to Tsarpath, in the land of Tsaidan, to a woman who was a widow.
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 There were many lepers in Israyel in the time of Elaysha the prophet, yet not one of them was cleansed, except Naaman, the Armaya."
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 They were all filled with wrath in the synagogue, as they heard these things.
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 They rose up, threw him out of the city, and led him to the brow of the hill that their city was built on, that they might throw him off the cliff.
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 But he, passing through the midst of them, went his way.
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 He came down to Kepharnakhum, a city of Galila. He was teaching them on the Sabbath day,
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 and they were astonished at his teaching, for his word was with authority.
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 In the synagogue there was a man who had a spirit of an unclean demon, and he shouted with a loud voice,
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
34 saying, "Ah. What have we to do with you, Yeshua, Natsraya? Have you come to destroy us? I know you who you are — the Holy One of God."
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 Yeshua rebuked him, saying, "Be silent, and come out of him." When the demon had thrown him down in their midst, he came out of him, having done him no harm.
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 Amazement came on all, and they spoke together, one with another, saying, "What is this word? For with authority and power he commands the unclean spirits, and they come out."
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 News about him went out into every place of the surrounding region.
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 He rose up from the synagogue, and entered into Shimon's house. Now Shimon's mother-in-law was suffering from a high fever, and they appealed to him about her.
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 He stood over her, and rebuked the fever; and it left her. Immediately she rose up and served them.
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 When the sun was setting, all those who had any sick with various diseases brought them to him; and he laid his hands on every one of them, and healed them.
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 Demons also came out from many, crying out, and saying, "You are the Son of God." But he rebuked them and did not allow them to speak, because they knew that he was the Meshikha.
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 When it was day, he departed and went into an uninhabited place, and the crowds looked for him, and came to him, and held on to him, so that he would not go away from them.
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 But he said to them, "I must proclaim the good news of the Kingdom of God to the other cities also. For this reason I have been sent."
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 And he was preaching in the synagogues of Galila.
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< Luke 4 >