< Deuteronomy 6 >

1 Now this is the commandment, the statutes, and the ordinances, which the LORD your God commanded to teach you, that you might do them in the land where you go over to possess it;
Haya ndiyo maagizo, amri na sheria ambazo Bwana Mungu wenu aliniagiza niwafundishe ninyi ili mpate kuyashika katika nchi ambayo ninyi mnavuka Yordani kuimiliki,
2 that you might fear the LORD your God, to keep all his statutes and his commandments, which I command you, you, and your son, and your son's son, all the days of your life; and that your days may be prolonged.
ili kwamba ninyi, watoto wenu na watoto wao baada yao wamche Bwana Mungu wenu siku zote kwa kushika amri na maagizo yake yote ninayowapa, ili mweze kuyafurahia maisha marefu.
3 Hear therefore, Israel, and observe to do it; that it may be well with you, and that you may increase mightily, as the LORD, the God of your fathers, has promised to you, in a land flowing with milk and honey.
Sikia, ee Israeli, nawe uwe mwangalifu kutii ili upate kufanikiwa na kuongezeka sana katika nchi itiririkayo maziwa na asali, kama Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaahidi ninyi.
4 Hear, Israel: the LORD is our God, the LORD is one.
Sikia, ee Israeli: Bwana Mungu wako, Bwana ni mmoja.
5 And you shall love the LORD your God with all your heart, and with all your soul, and with all your might.
Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote.
6 These words, which I command you this day, shall be on your heart;
Amri hizi ninazokupa leo zitakuwa katika moyo wako.
7 and you shall teach them diligently to your children, and shall talk of them when you sit in your house, and when you walk by the way, and when you lie down, and when you rise up.
Wafundishe watoto wako kwa bidii. Nena kuhusu amri hizi uketipo nyumbani na wakati utembeapo njiani, ulalapo na uamkapo.
8 You shall bind them for a sign on your hand, and they shall be for symbols between your eyes.
Zifunge kama alama juu ya mkono wako, na uzifunge juu ya paji la uso wako.
9 You shall write them on the door posts of your house, and on your gates.
Ziandike kwenye miimo ya milango ya nyumba yako na juu ya malango yako.
10 It shall be, when the LORD your God shall bring you into the land which he swore to your fathers, to Abraham, to Isaac, and to Jacob, to give you, great and goodly cities, which you did not build,
Wakati Bwana Mungu wako atakapokuleta katika nchi aliyowaapia baba zako, Abrahamu, Isaki na Yakobo, kukupa wewe, nchi kubwa, ina miji inayopendeza ambayo hukuijenga,
11 and houses full of all good things, which you did not fill, and cisterns dug out, which you did not dig, vineyards and olive trees, which you did not plant, and you shall eat and be full;
nyumba zilizojaa vitu vizuri vya aina nyingi ambavyo hukuvijaza, visima ambavyo hukuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hukupanda wewe, basi, utakapokula na kushiba,
12 then beware lest you forget the LORD, who brought you forth out of the land of Egypt, out of the house of bondage.
jihadhari usije ukamwacha Bwana, aliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
13 You shall fear the LORD your God; and you shall serve him only, and you shall cling to him, and take oaths by his name.
Utamcha Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake na kuapa kwa jina lake.
14 You shall not go after other gods, of the gods of the peoples who are around you;
Usifuate miungu mingine, miungu ya mataifa yanayokuzunguka;
15 for the LORD your God in the midst of you is a jealous God; lest the anger of the LORD your God be kindled against you, and he destroy you from off the face of the earth.
kwa kuwa Bwana Mungu wako, ambaye yuko katikati yako, ni Mungu mwenye wivu na hasira yake itawaka dhidi yako, naye atakuangamiza kutoka uso wa nchi.
16 Do not test the LORD your God, as you tested him at Massah.
Usimjaribu Bwana Mungu wako kama ulivyofanya huko Masa.
17 You shall diligently keep the commandments of the LORD your God, and his testimonies, and his statutes, which he has commanded you.
Utayashika maagizo ya Bwana Mungu wako kwa bidii, na masharti na amri alizokupa.
18 You shall do that which is right and good in the sight of the LORD; that it may be well with you, and that you may go in and possess the good land which the LORD swore to your fathers,
Fanya lililo haki na jema mbele za Bwana, ili upate kufanikiwa, uweze kuingia na kuimiliki nchi nzuri ambayo Bwana aliahidi kwa kiapo kwa baba zako,
19 to thrust out all your enemies from before you, as the LORD has spoken.
kuwafukuza kwa nguvu adui zako mbele yako kama Bwana alivyosema.
20 When your son asks you in time to come, saying, "What do the testimonies, the statutes, and the ordinances, which the LORD our God has commanded you mean?"
Siku zijazo, mtoto wako atakapokuuliza, “Ni nini maana ya masharti haya, amri na sheria hizi ambazo Bwana Mungu wako alikuagiza wewe?”
21 then you shall tell your son, "We were Pharaoh's bondservants in Egypt: and the LORD brought us out of Egypt with a mighty hand;
Mwambie: “Tulikuwa watumwa wa Farao huko Misri, lakini Bwana alitutoa sisi kutoka Misri kwa mkono wenye nguvu.
22 and the LORD showed great and awesome signs and wonders on Egypt, on Pharaoh, and on all his house, before our eyes;
Bwana akapeleka mbele yetu ishara za miujiza na maajabu makubwa na ya kutisha mno juu ya Misri na Farao pamoja na nyumba yake yote.
23 and he brought us out from there, that he might bring us in, to give us the land which he swore to our fathers.
Lakini Mungu akatutoa huko, akatuleta na kutupa nchi hii ambayo aliwaahidi baba zetu kwa kiapo.
24 The LORD commanded us to do all these statutes, to fear the LORD our God, for our good always, that he might preserve us alive, as at this day.
Bwana akatuagiza tutii amri hizi zote na kumcha Bwana Mungu wetu, ili tupate kustawi na kuendelea kuwa hai kama ilivyo leo.
25 It shall be righteousness to us, if we observe to do all this commandment before the LORD our God, as he has commanded us."
Kama tukizitii kwa bidii amri hizi zote mbele za Bwana Mungu wetu, kama alivyotuamuru sisi, hiyo itakuwa haki yetu.”

< Deuteronomy 6 >