< Daniel 6 >

1 It pleased Daryavesh to set over the kingdom one hundred twenty satraps, who should be throughout the whole kingdom;
Ilimpendeza Dario kuteua wakuu 120 kutawala katika ufalme wake wote,
2 and over them three administrators, of whom Daniel was one; that these satraps might give account to them, and that the king might not suffer loss.
pamoja na wasimamizi watatu juu yao, ambao mmoja wao alikuwa Danieli. Wakuu walitoa hesabu kwa hao wasimamizi ili mfalme asipate hasara.
3 Then this Daniel was distinguished above the administrators and the satraps, because an extraordinary spirit was in him; and the king thought to set him over the whole realm.
Basi Danieli alijidhihirisha, miongoni mwa wasimamizi na wakuu kwa sifa zake za kipekee hata mfalme akapanga kumweka juu ya ufalme wote.
4 Then the administrators and the satraps sought to find a charge against Daniel regarding the kingdom; but they could find no charge or fault, because he was faithful. Neither was there any error or fault found in him.
Walipofahamu hilo, wakuu na wasimamizi wakajaribu kutafuta sababu za kumshtaki Danieli kuhusu usimamizi wake wa shughuli za serikali, lakini hawakuweza kufanikiwa. Hawakuweza kupata kosa kwake, kwa sababu alikuwa mwaminifu, wala hakupatikana na upotovu au uzembe.
5 Then these men said, "We will not find any charge against this Daniel, except we find it against him concerning the law of his God."
Mwishoni watu hawa walisema, “Kamwe hatutapata msingi wa mashtaka dhidi ya huyu Danieli isipokuwa iwe inahusiana na sheria ya Mungu wake.”
6 Then these administrators and satraps assembled together to the king, and said this to him, "King Daryavesh, live forever.
Basi wasimamizi na wakuu wakaingia kwa mfalme kama kikundi wakasema, “Ee Mfalme Dario, uishi milele!
7 All the administrators of the kingdom, the deputies and the satraps, the counselors and the governors, have consulted together to establish a royal statute, and to make a strong decree, that whoever shall ask a petition of any god or man for thirty days, except of you, O king, he shall be cast into the den of lions.
Wasimamizi wa ufalme, wasaidizi, wakuu, washauri na watawala wote wamekubaliana kwamba mfalme atoe sheria na kukazia amri kuwa yeyote atakayetoa dua kwa mungu au mwanadamu yeyote katika muda huu wa siku thelathini zijazo, isipokuwa kwako wewe, ee mfalme, atupwe ndani ya tundu la simba.
8 Now, O king, establish the decree, and sign the writing, that it not be changed, according to the law of the Medes and Persians, which cannot be changed."
Sasa, ee mfalme, toa amri na uiandike ili isiweze kubadilishwa: kulingana na sheria za Wamedi na Waajemi, ambazo haziwezi kubatilishwa.”
9 Therefore king Daryavesh signed the writing and the decree.
Hivyo Mfalme Dario akaiweka amri hiyo katika maandishi.
10 When Daniel knew that the writing was signed, he went into his house (now his windows were open in his chamber toward Jerusalem) and he kneeled on his knees three times a day, and prayed, and gave thanks before his God, as he did before.
Basi Danieli alipofahamu kuwa amri ile imetangazwa, alikwenda nyumbani kwenye chumba chake cha ghorofani ambako madirisha yalifunguka kuelekea Yerusalemu. Akapiga magoti na kuomba mara tatu kwa siku, akimshukuru Mungu wake kama alivyokuwa akifanya mwanzoni.
11 Then these men assembled together, and found Daniel making petition and petition before his God.
Ndipo watu hawa wakaenda kama kikundi na kumkuta Danieli akiomba na kumsihi Mungu kwa ajili ya msaada.
12 Then they came near, and spoke before the king concerning the king's decree. "Haven't you signed a decree, that every man who shall make petition to any god or man within thirty days, except to you, O king, shall be cast into the den of lions?" The king answered, "The thing is true, according to the law of the Medes and Persians, which cannot be changed."
Basi wakaenda kwa mfalme na kusema naye kuhusu amri ya mfalme: “Je, hukutangaza amri kwamba kwa muda huu wa siku thelathini zijazo mtu yeyote ambaye atamwomba mungu au mwanadamu yeyote isipokuwa wewe, ee mfalme, angetupwa ndani ya tundu la simba?” Mfalme akajibu, “Amri ndivyo ilivyo, kulingana na sheria za Wamedi na Waajemi, ambazo haziwezi kubatilishwa.”
13 Then they answered and said before the king, "That Daniel, who is of the children of the captivity of Judah, doesn't regard you, O king, nor the decree that you have signed, but makes his petition three times a day."
Ndipo wakamwambia mfalme, “Danieli, ambaye ni mmoja wa mahamisho kutoka Yuda, hakuheshimu, ee mfalme, wala hajali amri uliyoiweka kwa maandishi. Bado anaomba mara tatu kwa siku.”
14 Then the king, when he heard these words, was very displeased, and set his heart on Daniel to deliver him. And he labored until the going down of the sun to rescue him.
Wakati mfalme aliposikia hili, akahuzunika mno. Akakusudia kumwokoa Danieli, hivyo akafanya kila jitihada ya kumwokoa hadi jua likatua.
15 Then these men assembled together to the king, and said to the king, "Know, O king, that it is a law of the Medes and Persians, that no decree nor statute which the king establishes may be changed."
Ndipo wale watu wakamwendea mfalme kama kikundi na kumwambia, “Ee mfalme, kumbuka kwamba kulingana na sheria ya Wamedi na Waajemi, hakuna amri wala sheria ambayo mfalme ameitoa inayoweza kubadilishwa.”
16 Then the king commanded, and they brought Daniel, and cast him into the den of lions. Now the king spoke and said to Daniel, "Your God whom you serve continually, he will deliver you."
Basi mfalme akatoa amri, nao wakamleta Danieli, na wakamtupa ndani ya tundu la simba. Mfalme akamwambia Danieli, “Mungu wako unayemtumikia daima na akuokoe!”
17 A stone was brought, and placed on the opening of the den; and the king sealed it with his own signet, and with the signet of his lords; that nothing might be changed concerning Daniel.
Jiwe likaletwa na kuwekwa kwenye mdomo wa tundu, naye mfalme akalitia muhuri kwa pete yake mwenyewe pamoja na kwa pete za wakuu wake, ili hali ya Danieli isiweze kubadilishwa.
18 Then the king went to his palace, and passed the night fasting; neither were instruments of music brought before him. And his sleep fled from him.
Kisha mfalme akarudi kwenye jumba lake la kifalme, naye usiku kucha hakula chakula wala kutumia viburudisho alivyoletewa. Lakini hakuweza kulala.
19 Then the king arose very early in the morning, and went in haste to the den of lions.
Asubuhi na mapema, mfalme akaondoka na kuharakisha kwenda kwenye tundu la simba.
20 When he came near to the den to Daniel, he cried with a lamentable voice. The king spoke and said to Daniel, "Daniel, servant of the living God. Is your God, whom you serve continually, able to deliver you from the lions?"
Wakati alipokaribia lile tundu, akamwita Danieli kwa sauti ya uchungu, “Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai! Je, Mungu wako unayemtumikia daima, ameweza kukuokoa kwa simba?”
21 Then said Daniel to the king, "O king, live forever.
Danieli akajibu, “Ee mfalme, uishi milele!
22 My God has sent his angel, and has shut the lions' mouths, and they have not hurt me; because before him innocence was found in me; and also before you, O king, have I done no wrong."
Mungu wangu alimtuma malaika wake, naye akafunga vinywa vya hawa simba. Hawajanidhuru, kwa sababu nilionekana sina hatia mbele zake. Wala kamwe sijafanya jambo lolote baya mbele yako, ee mfalme.”
23 Then was the king exceedingly glad, and commanded that they should take Daniel up out of the den. So Daniel was taken up out of the den, and no manner of hurt was found on him, because he had trusted in his God.
Mfalme akafurahi mno, naye akatoa amri Danieli atolewe kutoka kwa lile tundu. Danieli alipotolewa kutoka kwa lile tundu, hakukutwa na jeraha lolote, kwa sababu alikuwa amemtumaini Mungu wake.
24 The king commanded, and they brought those men who had accused Daniel, and they cast them into the den of lions, them, their children, and their wives; and the lions overpowered them, and broke all their bones in pieces, before they came to the bottom of the den.
Kwa amri ya mfalme, wale watu waliokuwa wamemshtaki Danieli kwa uongo waliletwa na kutupwa ndani ya lile tundu la simba, pamoja na wake zao na watoto wao. Nao kabla hawajafika chini kwenye sakafu ya lile tundu, simba wakawakamata na kusaga mifupa yao yote.
25 Then king Daryavesh wrote to all the peoples, nations, and languages, who dwell in all the earth: "Peace be multiplied to you.
Kisha Mfalme Dario akawaandikia kabila zote za watu, mataifa, na watu wa kila lugha katika nchi yote: “Ninyi na mstawi sana!
26 I make a decree, that in all the dominion of my kingdom men tremble and fear before the God of Daniel; for he is the living God, and steadfast forever. His kingdom shall not be destroyed; and his dominion shall be to the end.
“Natoa amri hii, kwamba katika kila sehemu ya ufalme wangu, lazima watu wamwogope na kumheshimu Mungu wa Danieli. “Kwa maana yeye ni Mungu aliye hai, naye hudumu milele, ufalme wake hautaangamizwa, nao utawala wake hauna mwisho.
27 He delivers and rescues, and he works signs and wonders in heaven and in earth, who has delivered Daniel from the power of the lions."
Huponya na kuokoa; hufanya ishara na maajabu mbinguni na duniani. Amemwokoa Danieli kutoka nguvu za simba.”
28 So this Daniel prospered in the reign of Daryavesh, and in the reign of Koresh the Persian.
Hivyo Danieli akastawi wakati wa utawala wa Dario, na utawala wa Koreshi Mwajemi.

< Daniel 6 >