< Matthew 25 >

1 "Then will the kingdom of heaven be likened to ten maidens who took their lamps and went out to meet the bridegroom and the bride.
“Wakati huo, Ufalme wa mbinguni utafanana na wasichana kumi waliochukua taa zao, wakaenda kumlaki bwana arusi.
2 "And five of them were foolish, and five were wise.
Watano miongoni mwao walikuwa wapumbavu na watano walikuwa wenye busara.
3 "The foolish took their lamps, but took no oil with them;
Wale wapumbavu walichukua taa zao, lakini hawakuchukua akiba ya mafuta.
4 "but the wise took oil in their flasks with their lamps.
Lakini wale wenye busara walichukua mafuta katika chupa pamoja na taa zao.
5 "Now because the bridegroom tarried, they all fell to nodding and went on sleeping.
Kwa kuwa bwana arusi alikawia kuja, wale wanawali wote wote walisinzia, wakalala.
6 "But at midnight there arose a cry, "‘Behold, the bridegroom! Go out to meet him!’
Usiku wa manane kukawa na kelele: Haya, haya! Bwana arusi anakuja; nendeni kumlaki.
7 "Then all those maidens rose and trimmed their lamps;
Hapo wale wanawali wote wakaamka, wakazitayarisha taa zao.
8 "and the foolish said to the wise, "‘Give us some of your oil, for our lamps are going out.’
Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara: Tupeni mafuta yenu kidogo maana taa zetu zinazimika.
9 "‘Not so, answered the wise, ‘for there may not be enough for you and for us. Go to the shops, rather, and buy some for yourselves.’
Lakini wale wenye busara wakawaambia, Hayatatutosha sisi na ninyi! Afadhali mwende dukani mkajinunulie wenyewe!
10 "And while they were going away to buy, the bridegroom came; and those who were ready went in with him to the wedding-feast. And the door was shut.
Basi, wale wanawali wapumbavu walipokwenda kununua mafuta, bwana arusi akafika, na wale wanawali waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye katika jumba la arusi, kisha mlango ukafungwa.
11 "Afterwards the other maidens came and cried, "‘Lord, Lord, open unto us!’
Baadaye wale wanawali wengine wakaja, wakaita: Bwana, bwana, tufungulie!
12 "‘In solemn truth I tell you,’ he replied, ‘I know you not.’
Lakini yeye akawajibu, Nawaambieni kweli, siwajui ninyi.”
13 "Be watchful then, for you know neither the day nor the hour.
Kisha Yesu akasema, “Kesheni basi, kwa maana hamjui siku wala saa.
14 "For it is like a man going into another country, who summoned his slaves, and committed his property to their care.
“Itakuwa kama mtu mmoja aliyetaka kusafiri ng'ambo: aliwaita watumishi wake, akawakabidhi mali yake.
15 "To one he gave five talents, to another two, and to another, one - to each according to his individual ability - and then set out on his travels.
Alimpa kila mmoja kadiri ya uwezo wake: mmoja sarafu tano za fedha ziitwazo talanta, mwingine talanta mbili na mwingine talanta moja, kisha akasafiri.
16 "At once the man who had received the five talents went out and traded with them, and made five talents more.
Mara yule aliyekabidhiwa talanta tano akafanya kazi nazo akapata faida talanta tano.
17 "In the same way the one who got two talents made another two.
Hali kadhalika na yule aliyekabidhiwa talanta mbili akapata faida talanta mbili.
18 "But he who had received the one talent went off, and dug a hole in the ground, and hid his master’s money.
Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaenda akachimba shimo ardhini, akaificha fedha ya bwana wake.
19 "After a long time the master of those slaves came, and demanded a reckoning with them.
“Baada ya muda mrefu, yule bwana alirudi, akaanza kukagua hesabu ya matumizi na mapato ya fedha yake.
20 "The man who had received the five talents came, bringing five more, and said. "‘Master, five talents you entrusted to me; see, I have gained five more.’
Mtumishi aliyekabidhiwa talanta tano akaja amechukua zile talanta tano faida, akamwambia, Bwana, ulinikabidhi talanta tano, hapa pana talanta tano zaidi faida niliyopata.
21 "‘Well done, good and faithful slave,’ replied his master; ‘You have been faithful over many things. Enter into your master’s joy.’
Bwana wake akamwambia, Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.
22 "The second, who had received the two talents, came up and said. "‘Master, it was two talents that you entrusted to me; see, I have gained two more.’
“Mtumishi aliyekabidhiwa talanta mbili akaja, akatoa talanta mbili faida, akisema, Bwana, ulinikabidhi talanta mbili. Chukua talanta mbili zaidi faida niliyopata.
23 "‘Well done, good and faithful slave,’ his master replied, ‘You have been faithful over many things; enter into your master’s joy.’
Bwana wake akamwambia, Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo, nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.
24 "Then the man who had received the one talent came up and said. "‘Master, I knew you were a hard man, reaping where you had not sown, and gathering where you had not scattered;
“Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaja, akasema, Bwana, najua wewe ni mtu mgumu; wewe huvuna pale ambapo hukupanda, na kukusanya pale ambapo hukutawanya.
25 "so I was afraid; I went away and buried your talent in the earth. There, you have what belongs to you!’
Niliogopa, nikaificha fedha yako katika ardhi. Chukua basi mali yako.
26 "‘You wicked and lazy slave,’ said his master. ‘You say you knew that I reap where I have not sowed, and gather where I have not scattered?
“Bwana wake akamwambia, Wewe ni mtumishi mwovu na mvivu! Unajua kuwa mimi huvuna mahali ambapo sikupanda, na hukusanya pale ambapo sikutawanya.
27 "‘Then you ought to have deposited my money with the bankers, and at my coming I should have received back my property with interest.
Ilikupasa basi, kuiweka fedha yangu katika benki, nami ningelichukua mtaji wangu na faida yake!
28 "‘So take away the talent from him, and give it to the man who has ten talents.
Basi, mnyang'anyeni hiyo fedha mkampe yule mwenye talanta kumi.
29 "‘(For to every one who has, it shall be given, and he shall have abundance; but from him who has not shall be taken away even what he has.)
Maana, aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
30 "‘But cast out the worthless slave into the outer darkness; there will be the weeping and the gnashing of teeth.’
Na kuhusu huyu mtumishi asiye na faida, mtupeni nje gizani! Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.
31 "But when the Son of man comes in his glory, and all the angels with him, then will he take his seat on the throne of his glory;
“Wakati Mwana wa Mtu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote wakiwa pamoja naye, hapo ataketi juu ya kiti chake cha enzi kitukufu,
32 "and all the nations will be gathered in his presence. And he will separate them one from another, as a shepherd divides his sheep from the goats;
na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu kama mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi.
33 "and he will place the sheep on his right hand, and the goats on his left.
Atawaweka kondoo upande wake wa kulia na mbuzi upande wake wa kushoto.
34 "Then he, the King will say to those on his right hand. "‘Come, my Father’s blessed ones, inherit the kingdom prepared for you from the foundation of the world.
“Kisha Mfalme atawaambia wale walio upande wake wa kulia, Njoni enyi mliobarikiwa na Baba yangu; pokeeni Ufalme mliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
35 "‘For I was hungry, and you gave me food; I was thirsty, and you gave me drink; I was a stranger, and you took me in;
Maana nilikuwa na njaa nanyi mkanipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi mkanipa maji; nilikuwa mgeni nanyi mkanikaribisha;
36 "‘I was naked, and you clothed me; I was sick, and you visited me; I was in prison, and you came to see me.’
nilikuwa uchi, mkanivika; nilikuwa mgonjwa nanyi mkaja kunitazama; nilikuwa gerezani nanyi mkaja kunitembelea.
37 "Then shall the righteous answer him, saying. ‘Master, when did we see you hungry and feed you; or thirsty and give you drink?
Hapo, hao watu wema watamjibu mfalme Bwana, ni lini tulikuona mwenye njaa nasi tukakupa chakula, au ukiwa na kiu nasi tukakunywesha maji?
38 "‘When did we see you a stranger and take you in; or naked and clothe you?
Ni lini tulikuona ukiwa mgeni nasi tukakukaribisha, au bila nguo nasi tukakuvika?
39 "‘When did we see you sick or in prison, and come to see you?’
Ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa au mfungwa nasi tukaja kukutazama?
40 "‘In solemn truth I tell you,’ the King will answer them, ‘that inasmuch as you have done it unto one of the least of these, my brothers, you have done it unto me.’
Mfalme atawajibu, Kweli nawaambieni, kila kitu mlichomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu wadogo, mlinitendea mimi.
41 "Then he will say to those also at his left hand. ‘Depart from me, accursed ones, into the eternal fire prepared for the devil and his angels; (aiōnios g166)
“Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, Ondokeni mbele yangu enyi mliolaaniwa! Nendeni katika moto wa milele aliotayarishiwa Ibilisi na malaika wake. (aiōnios g166)
42 "for I was hungry, and you gave me no food; I was thirsty, and you gave me no drink;
Maana nilikuwa na njaa nanyi hamkunipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi hamkunipa maji.
43 "I was a stranger, and you took me not in; naked, and you clothed me not; sick, or in prison, and you visited me not.’
Nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha; nilikuwa mgonjwa na mfungwa nanyi hamkuja kunitazama.
44 "Then will they also answer, ‘Master, when did we ever see you hungry, or thirsty, or a stranger, or naked, or sick, or in prison, and did not minister to you?’
“Hapo nao watajibu, Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, ukiwa mgeni au bila nguo, ukiwa mgonjwa au mfungwa, nasi hatukuja kukuhudumia?
45 "But he will reply, ‘In solemn truth I tell you that inasmuch as you did not do it unto one of these least, you did not do it unto me.’
Naye atawajibu, Nawaambieni kweli, kila mlipokataa kumtendea mambo haya mmojawapo wa hawa wadogo, mlikataa kunitendea mimi.
46 "And these will go away into eternal punishment; but the righteous into eternal life." (aiōnios g166)
Basi, hawa watakwenda kwenye adhabu ya milele, lakini wale waadilifu watakwenda kwenye uzima wa milele.” (aiōnios g166)

< Matthew 25 >