< Luke 19 >

1 So he entered Jericho and was passing through the town.
Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2 There was a man there, called Zaccheus, who was a chief of the tax- gatherers, and was wealthy.
Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 And he kept trying to see what sort of a man Jesus was; but he could not see because he was short.
Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4 So he ran on before him and climbed up into a sycamore tree to see him; for he was about to pass that way.
Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5 As soon as Jesus came to the place, he looked up and said to him, "Come down quickly, Zaccheus, for today I must stay at your house."
Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
6 He made haste to climb down, and receive him joyfully.
Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7 When they all saw it, they began to complain, saying "He has gone in to lodge with a man who is a sinner."
Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
8 But Zaccheus stood up and said to the Lord, "I give half my property to the poor, Lord, and if I have defrauded any man of anything I am restoring it to him fourfold."
Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
9 "Today is salvation come to this house," said Jesus "since Zaccheus here is a son of Abraham.
Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10 "For the Son of man is come to seek and to save the lost."
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
11 As they were listening to his words he added this parable, because he was near Jerusalem and they thought that the kingdom of God was immediately to appear.
Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12 So he said. "A certain nobleman went abroad to receive for himself royal power and to return.
Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13 "And he summoned ten slaves of his, and gave them ten pounds, and said to them, "‘Trade with these until I come.’
Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14 "But this fellow citizens hated him, and sent a deputation after him to say, ‘We do not wish this man to become our king.’
Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15 "And upon his return after he had secured the royal power, he ordered the slaves to whom he had given the money to be called in, so that he might know what they had gained by trading.
“Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16 "And the first came before him, saying, ‘Master, your pound has made ten pounds.’
Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17 "And he said to him, ‘Well done, good slave! Because you have been faithful in a very little, have authority over ten cities.’
Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18 "And the second came and said, ‘Master, your pound has made five pounds.’
Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19 "Then he said to him also, ‘You shall be over five cities.’
Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20 "And the next came to him and said, ‘Here master is your pound which I was keeping safe in a napkin.
“Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21 "‘For I was afraid of you, because you are a hard man. You take what you did not sow.’
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22 "He said to him, "‘By your own words I will Judge you, you wicked slave. You knew, did you, that I was a hard man taking up what I did not lay down, reaping what I did not sow.
Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23 "‘Then why did you not put my money into the bank, so that at my coming I might I might have gotten it back with interest?’
Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24 "Then to those who stood by, he said, ‘Take the pounds from him and give it to him who has ten pounds.’
Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25 "‘Master,’ they said to him, ‘he already has ten pounds.’
Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26 "‘I tell you that to every one who has it shall be given; and from him who has not shall be taken away even what he has.
Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 "‘Howbeit these enemies of mine who were not willing for me to become their King, bring them here, and slay them in my presence.’"
Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
28 When he had so spoken he went on before, going up to Jerusalem.
Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29 When he was come near Bethphage and Bethany at the mount called The Olive Orchard,
Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 he sent two of his disciples saying. "Go into the village in the front, and on entering it you will find an ass’s colt tied, on which no one has ever ridden.
akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31 "Untie it and bring it here. And if any one asks you, ‘Why are you untying the colt?’ Simply say, ‘The Master needs it.’"
Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
32 Then those who were sent out and found it as he had told them.
Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33 For as they were untying the colt, the owners said to them, "Why are you untying the colt?"
Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34 They answered, "The Master needs it."
Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 So they led it to Jesus, and, after throwing their outer garments on the colt, they placed Jesus on it.
Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36 So he rode on, while they kept throwing their garments in the way.
Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 And when now he was coming near Jerusalem, and descending the Mount of Olives, the whole multitude of the disciples began to rejoice, and to praise God with a loud voice for the almighty works they had seen.
Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38 They cried, "Blessed is the King who comes in the name of the Lord! Peace in Heaven and glory in the Highest"
wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39 And some of the Pharisees said to them out of the crowd, "Teacher reprove your disciples!"
Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
40 "I tell you," he answered, "that if these should hold their peace, the very stones would cry out."
Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
41 And when he came into view of the city, as he approached it he broke into loud weeping,
Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42 exclaiming. "Oh that at this time you knew, yes, even you, on what your peace depends! But now it is hidden from your eyes.
akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 "The time will come for you when your enemies will throw ramparts around you, and encompass you, and shut you in on every side, and raze you to the ground,
Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44 "you and your children within you. And they will not leave in you one stone upon the another. Because you knew not the time of your visitation."
Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
45 Then Jesus went into the Temple and began to drive out dealers,
Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46 saying, "It is written, "The house of God shall be called a house of prayer, but you have made it a den of robbers."
akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
47 Day after day he continued to teach in the Temple. The high priests and scribes tried to have him put to death, so did the rulers of the people.
Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48 But they could not find how to do it, for the people all hung upon him, listening to him.
lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

< Luke 19 >