< Luke 16 >

1 To his disciples he said. "There was a certain rich man who had a steward, and this steward was accused to him of wasting his property.
Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Palikuwa na tajiri mmoja na msimamizi wake. Ilisemekana kwamba huyo msimamizi alikuwa anatumia vibaya mali ya tajiri yake.
2 "He called to him to him and said. "‘What is this that I hear about you? Render an account of your stewardship; for you can no longer be steward.’
Hivyo huyo tajiri akamwita na kumuuliza, ‘Ni mambo gani haya ninayoyasikia kukuhusu? Toa taarifa ya usimamizi wako, kwa sababu huwezi kuendelea kuwa msimamizi.’
3 "Now the steward said to himself. ‘What shall I do, now that my master is taking away my stewardship? I am not strong enough to dig, to beg I am ashamed.
“Yule msimamizi akawaza moyoni mwake, ‘Nitafanya nini sasa? Bwana wangu ananiondoa katika kazi yangu. Sina nguvu za kulima, nami ninaona aibu kuombaomba.
4 "‘I know what I will do, so that when I am put out of my stewardship, they may receive me into their houses.’
Najua nitakalofanya ili nikiachishwa kazi yangu hapa, watu wanikaribishe nyumbani kwao.’
5 "So he called to him each of his master’s debtors and said to the first, ‘How much money do you owe my master?’
“Kwa hiyo akawaita wadeni wote wa bwana wake, mmoja mmoja. Akamuuliza wa kwanza, ‘Deni lako kwa bwana wangu ni kiasi gani?’
6 "‘A hundred measures of oil,’ he answered. "He said to him, ‘Take your bill and sit down quickly and write fifty."
“Akajibu, ‘Galoni 800za mafuta ya mizeituni.’ “Msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati ya deni lako, ibadilishe upesi, uandike galoni 400.’
7 "To a second he said, ‘How much do you owe?’ "The man answered, ‘A hundred measures of wheat.’ "‘Here is you bill,’ he said, ‘change it to eighty measures.’
“Kisha akamuuliza wa pili, ‘Wewe deni lako ni kiasi gani?’ “Akajibu, ‘Vipimo 1,000vya ngano.’ “Yule msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati yako, andika vipimo 800!’
8 "And the master praised the unjust steward because he had acted shrewdly; for the sons of this world are in relation to their own generation wiser than the sons of the light. (aiōn g165)
“Yule bwana akamsifu yule msimamizi dhalimu kwa jinsi alivyotumia ujanja. Kwa maana watu wa dunia hii wana ujanja zaidi wanapojishughulisha na mambo ya dunia kuliko watu wa nuru. (aiōn g165)
9 "And to you I say, Use mammon, dishonest as it is, to make yourselves friends, so that when it shall fail they will welcome you to the eternal tabernacles. (aiōnios g166)
Nawaambia, tumieni mali ya kidunia kujipatia marafiki, ili itakapokwisha, mkaribishwe katika makao ya milele. (aiōnios g166)
10 "The man who is faithful in a very little is faithful also in much, and he who is unjust in a very little, is unjust also as much.
“Yeyote aliye mwaminifu katika mambo madogo, pia ni mwaminifu hata katika mambo makubwa, naye mtu ambaye si mwaminifu katika mambo madogo pia si mwaminifu katika mambo makubwa.
11 "If therefore you have not been faithful in the unrighteous mammon, who will trust to you the true riches?
Ikiwa hamkuwa waaminifu katika mali ya kidunia, ni nani atakayewaaminia mali ya kweli?
12 "And if you are not faithful with what belongs to another, who will give you what is your own?
Nanyi kama hamkuwa waaminifu na mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?
13 "No one can be a household servants to two masters; for either he will hate the one and love the other, or he will cling to the one and despise the other. You cannot be the slave of God and of Mammon."
“Hakuna mtumishi awezaye kuwatumikia mabwana wawili. Kwa kuwa atamchukia huyu na kumpenda yule mwingine, au atashikamana sana na huyu na kumdharau yule mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu pamoja na Mali.”
14 Now the Pharisees who loved money listened to all this and they jeered at him.
Mafarisayo, waliokuwa wapenda fedha, waliyasikia hayo yote na wakamcheka kwa dharau.
15 He said to them. "You are those that justify themselves in the eyes of men; but God knows you hearts; for that which is lofty in the eyes of men is abomination in the eyes of God.
Yesu akawaambia, “Ninyi mnajionyesha kuwa wenye haki mbele za wanadamu, lakini Mungu anaijua mioyo yenu. Kwa maana vile vitu ambavyo wanadamu wanavithamini sana, kwa Mungu ni machukizo.
16 "The Law and the Prophet lasted until John; since then the gospel of the kingdom of God is preached, and any one presses in.
“Sheria na Manabii vilihubiriwa mpaka kuja kwa Yohana Mbatizaji. Tangu wakati huo habari njema za Ufalme wa Mungu zinahubiriwa, na kila mmoja hujiingiza kwa nguvu.
17 "Yet it is easier for heaven and earth to pass away then for one title of the law to fail.
Lakini ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupita kuliko hata herufi moja kuondoka katika Sheria.
18 "Every man who divorces his wife and marries some one else, commits adultery; and he who marries one who is put away by her husband commits adultery.
“Mtu yeyote amwachaye mkewe na kumwoa mwanamke mwingine anazini, naye mwanaume amwoaye mwanamke aliyetalikiwa anazini.
19 "Now there was a certain rich man who was clothed in purple and fine linen, and made merry every day in splendor.
“Palikuwa na mtu mmoja tajiri aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, ambaye aliishi kwa anasa kila siku.
20 "And a certain beggar named Lazarus was thrown at his door.
Hapo penye mlango wake aliishi maskini mmoja, jina lake Lazaro, mwenye vidonda mwili mzima.
21 "He was full of sores, and longingly desired to be fed with the crumbs that fell from the rich man’s table. Yes! even the dogs came and licked his sores.
Huyo Lazaro alitamani kujishibisha kwa makombo yaliyoanguka kutoka mezani kwa yule tajiri. Hata mbwa walikuwa wakija na kuramba vidonda vyake.
22 "But in the course of time the beggar died; and he was carried by angels into Abraham’s bosom. The rich man also died, and was buried.
“Wakati ukafika yule maskini akafa, nao malaika wakamchukua akae pamoja na Abrahamu. Yule tajiri naye akafa na akazikwa.
23 "And as he was tormented in Hades, he lifted up his eyes and saw Abraham afar off and Lazarus in his bosom. (Hadēs g86)
Kule kuzimu alipokuwa akiteseka, alitazama juu, akamwona Abrahamu kwa mbali, naye Lazaro alikuwa karibu yake. (Hadēs g86)
24 "And he cried out and said, ‘Father Abraham have mercy on me; and send Lazarus to dip the tip of his finger in water and cool my tongue, for I am in anguish in this flame.’
Hivyo yule tajiri akamwita, ‘Baba Abrahamu, nihurumie na umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake ndani ya maji aupoze ulimi wangu, kwa sababu nina maumivu makuu kwenye moto huu.’
25 "‘Remember my son.’ said Abraham, ‘that you had in your lifetime all your good things, and in the same way Lazarus his evil things; but now here he is comforted, and you are in anguish.
“Lakini Abrahamu akamjibu, ‘Mwanangu, kumbuka kwamba wakati wa uhai wako ulipata mambo mazuri, lakini Lazaro alipata mambo mabaya. Lakini sasa anafarijiwa hapa na wewe uko katika maumivu makuu.
26 "But besides all this, between us and you there is a great chasm fixed, so that those who want to cross from here to you cannot, nor can those who would cross from you to us.’
Zaidi ya hayo, kati yetu na ninyi huko kumewekwa shimo kubwa, ili wale wanaotaka kutoka huku kuja huko wasiweze, wala mtu yeyote asiweze kuvuka kutoka huko kuja kwetu.’
27 "‘I beg you then, father,’ he said, ‘send him to my fathers house. For I have five brothers.
“Akasema, ‘Basi, nakuomba, umtume Lazaro aende nyumbani kwa baba yangu,
28 "‘Let him earnestly warn them, lest they too come to this place of torment.’
maana ninao ndugu watano. Awaonye, ili wasije nao wakafika mahali hapa pa mateso.’
29 "But Abraham said, ‘They have Moses and the Prophets, let them listen to them.’
“Abrahamu akamjibu, ‘Ndugu zako wana Maandiko ya Mose na Manabii, wawasikilize hao.’
30 "‘Nay, Father Abraham,’ he said ‘but if some one went to them from the dead they would repent.’
“Yule tajiri akasema, ‘Hapana, baba Abrahamu, lakini mtu kutoka kwa wafu akiwaendea, watatubu.’
31 "‘If they will not listen to Moses and the prophets,’ said Father Abraham, ‘neither will they be persuaded if one should rise from the dead.’"
“Abrahamu akamwambia, ‘Kama wasipowasikiliza Mose na Manabii, hawataweza kushawishika hata kama mtu akifufuka kutoka kwa wafu.’”

< Luke 16 >