< Psalms 73 >

1 A Psalm for Asaph. How good is God to Israel, to the upright in heart!
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 But my feet were almost overthrown; my goings very nearly slipped.
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 For I was jealous of the transgressors, beholding the tranquility of sinners.
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 For there is no sign of reluctance in their death: and [they have] firmness under their affliction.
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5 They are not in the troubles of [other] men; and they shall not be scourged with [other] men.
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 Therefore pride has possessed them; they have clothed themselves with their injustice and ungodliness.
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7 Their injustice shall go forth as out of fatness: they have fulfilled their intention.
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8 They have taken counsel and spoken in wickedness: they have uttered unrighteousness loftily.
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9 They have set their mouth against heaven, and their tongue has gone through upon the earth.
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10 Therefore shall my people return hither: and full days shall be found with them.
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11 And they said, How does God know? and is there knowledge in the Most High?
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12 Behold, these [are] the sinners, and they that prosper always: they have possessed wealth.
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
13 And I said, Verily in vain have I justified my heart, and washed my hands in innocency.
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14 For I was plagued all the day, and my reproof [was] every morning.
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15 If I said, I will speak thus; behold, I [should] have broken covenant with the generation of your children.
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16 And I undertook to understand this, [but] it is too hard for me,
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17 until I go into the sanctuary of God; [and so] understand the latter end.
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18 Surely you have appointed [judgments] to them because of their crafty dealings: you have cast them down when they were lifted up.
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19 How have they become desolate! suddenly they have failed: they have perished because of their iniquity.
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20 As the dream of one awakening, O Lord, in your city you will despise their image.
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
21 For my heart has rejoiced, and my reins have been gladdened.
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22 But I [was] vile and knew not: I became brutish before you.
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23 Yet I am continually with you: you have holden my right hand.
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24 You have guided me by your counsel, and you have taken me to yourself with glory.
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25 For what have I in heaven [but you]? and what have I desired upon the earth beside you?
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26 My heart and my flesh have failed: [but] God [is the strength] of my heart, and God is my portion for ever.
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27 For, behold, they that remove themselves far from you shall perish: you have destroyed every one that goes a whoring from you.
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 But it is good for me to cleave close to God, to put my trust in the Lord; that I may proclaim all your praises in the gates of the daughter of Sion.
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.

< Psalms 73 >