< Psalms 64 >

1 For the end, a Psalm of David. Hear my prayer, O God, when I make my petition to you; deliver my soul from fear of the enemy.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
2 You have sheltered me from the conspiracy of them that do wickedly; from the multitude of them that work iniquity;
Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
3 who have sharpened their tongues as a sword; they have bent their bow maliciously;
Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
4 to shoot in secret at the blameless; they will shoot him suddenly, and will not fear.
Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
5 They have set up for themselves an evil matter, they have given counsel to hide snares; they have said, Who shall see them?
Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
6 They have searched out iniquity; they have wearied themselves with searching diligently, a man shall approach and the heart is deep,
Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
7 and God shall be exalted, their wounds were [caused by] the weapon of the foolish children,
Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
8 and their tongues have set him at nothing, all that saw them were troubled;
Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
9 and every man was alarmed, and they related the works of God, and understood his deeds.
Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
10 The righteous shall rejoice in the Lord, and hope on him, and all the upright in heart shall be praised.
Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!

< Psalms 64 >