< Psalms 135 >

1 Alleluia. Praise you the name of the Lord; praise the Lord, [you his] servants,
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 who stand in the house of the Lord, in the courts of the house of our God.
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Praise you the Lord; for the Lord is good: sing praises to his name; for [it is] good.
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 For the Lord has chosen Jacob for himself, [and] Israel for his peculiar treasure.
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 For I know that the Lord is great, and our Lord is above all gods;
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 all that the Lord willed, he did in heaven, and on the earth, in the sea, and in all deeps.
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 Who brings up clouds from the extremity of the earth: he has made lightnings for the rain: he brings winds out of his treasures.
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 Who struck the firstborn of Egypt, both of man and beast.
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 He sent signs and wonders into the midst of you, O Egypt, on Pharao, and on all his servants.
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 Who struck many nations, and killed mighty kings;
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 Seon king of the Amorites, and Og king of Basan, and all the kingdoms of Chanaan:
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 and gave their land [for] an inheritance, an inheritance to Israel his people.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 O Lord, your name [endures] for ever, and your memorial to all generations.
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 For the Lord shall judge his people, and comfort himself concerning his servants.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 The idols of the heathen are silver and gold, the works of men's hands.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 They have a mouth, but they can’t speak; they have eyes, but they can’t see;
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 they have ears, but they can’t hear; for there is no breath in their mouth.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 Let those who make them be made like to them; and all those who trust in them.
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 O house of Israel, bless you the Lord: O house of Aaron, bless you the Lord:
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 O house of Levi, bless you the Lord: you that fear the Lord, bless the Lord.
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Blessed in Sion be the Lord, who dwells in Jerusalem.
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Psalms 135 >