< Michaeas 6 >

1 Hear now a word: the Lord God has said; Arise, plead with the mountains, and let the hills hear your voice.
Sasa sikilizeni kile ambacho Yahwe asemacho, “Inuka na ueleze kesi yako mbele ya milima; acha milima isikie sauti yako.
2 Hear you, O mountains, the controversy of the Lord, and [you] valleys [even] the foundations of the earth: for the Lord [has] a controversy with his people, and will plead with Israel.
Sikilizeni madai ya Yahwe, enyi milima, na ninyi misingi mivumilivu ya dunia. Kwa kuwa Yahwe anavumilia pamoja na watu wake, na atapigana katika mahakama juu ya Israeli.”
3 O my people, what have I done to you? or wherein have I grieved you? or wherein have I troubled you? answer me.
Watu wangu, nimefanya nini kwenu? nimewachosha mara ngapi? shuhudieni dhidi yangu!
4 For I brought tee up out of the land of Egypt, and redeemed you out of the house of bondage, and sent before you Moses, and Aaron, and Mariam.
Kwa kuwa niliwaleta kutoka nchi ya Msiri na kuwaokoa kutoka kwenye nyumba ya utumwa. Nawatuma Musa, Aruni, na Mariamu kwako.
5 O my people, remember now, what counsel Balac king of Moab took against you, and what Balaam the son of Beor answered him, from the reeds to Galgal; that the righteousness of the Lord might be known.
Watu wangu, kumbukeni ambavyo Balaki mfalme wa Moabu alivyotunga, na vile ambavyo Balamu mwana wa Beori alivyomjibu kama ulipokuwa ukienda kutoka kwa Gilgali, hivyo mnaweza kujua matendo ya haki ya Yahwe.”
6 Wherewithal shall I reach the Lord, [and] lay hold of my God most high? shall I reach him by whole burnt offerings, by calves of a year old?
Je nilete nini kwa Yahwe, ninapoenda kumwinamia Mungu aliye juu? Je ninaweza kuja kwake na sadaka za kuteketeza, pamoja na ndama wenye mwaka mmoja?
7 Will the Lord accept thousands of rams, or ten thousands of fat goats? should I give my firstborn for ungodliness, the fruit of my body for the sin of my soul?
Je Yahwe atapendezwa na maelfu ya kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa ajili ya kosa langu, tunda la mwili wangu kwa ajili ya dhambi yangu mwenyewe?
8 Has it [not] been told you, O man, what [is] good? or what does the Lord require of you, but to do justice, and love mercy, and be ready to walk with the Lord your God?
Amekwambia, mtu, kile kilicho bora, na kile ambacho Yahwe atakacho kutoka kwako: Kutenda haki, kupenda ukarimu, na kutembea kwa unyenyekevu pamoja na Mungu wako.
9 The Lord's voice shall be proclaimed in the city, and he shall save those that fear his name: hear, O tribe; and who shall order the city?
Sauti ya Yahwe inatangaza kwenye mji-hata sasa hekima hukukiri jina lako: “Kaa tayari kwa ajili ya fimbo, na kwa yule aliyeiweka.
10 [Is there] not fire, and the house of the wicked heaping up wicked treasures, and [that] with the pride of unrighteousness?
Kuna utajiri katika nyumba za waovu, na kipimo cha uongo hilo ni chukizo mno.
11 Shall the wicked be justified by the balanced, or deceitful weights in the bag,
Ningeweza kumfikira mtu kuwa hana hatia kama anatumia kipimo cha ulaghai, pamoja na mfuko wa kipimo wa udanganyifu?
12 whereby they have accumulated their ungodly wealth, and they that dwell in the city have uttered falsehoods, and their tongue has been exalted in their mouth?
Matajiri wamejaa uharibifu, makazi yao yamesema uongo, na ulimi wao katika midomo yao unaudanganyifu.
13 Therefore will I begin to strike you; I will destroy you in your sins.
Kwa hiyo nimekupiga kwa pigo linaloumiza, nimekufanya gofu kwa sababu ya dhambi zako.
14 You shall eat, and shall not be satisfied; and there shall be darkness upon you; and he shall depart from [you], and you shall not escape; and all that shall escape shall be delivered over to the sword.
Utakula lakini hutatosheka; utupu wako utabakia ndani yako. Utatunza mizigo mbali lakini hutahifadhi, na kile unachokihifadhi nitakitoa kwa upanga.
15 You shall sow, but you shall not reap; you shall press the olive, but you shall not anoint yourself with oil; and [shall make] wine, but you shall drink no wine: and the ordinances of my people shall be utterly abolished.
Utapanda lakini huatavuna; utazikusanya zaituni lakini hutajipaka mafuta; utasindika zabibu lakini hutakunywa divai.
16 For you have kept the statues of Zambri, and [done] all the works of the house of Achaab; and you have walked in their ways, that I might deliver you to utter destruction, and those that inhabit the city to hissing: and you shall bear the reproach of nations.
Kanuni zilizotengenezwa na Omri zimetunzwa, na matendo yote ya nyumba ya Ahabu. Mnatembea kwa ushauri wao. Hivyo nitakufanya wewe, mji, gofu, na makazi yako jambo la zomeo, na matabeba dharau kama watu wangu.”

< Michaeas 6 >