< Esias 13 >

1 THE VISION WHICH ESAIAS SON OF AMOS SAW AGAINST BABYLON.
Neno kuhusu Babeli ambalo Isaya mwana wa Amozi aliliona:
2 Lift up a standard on the mountain of the plain, exalt the voice to them, beckon with the hand, open [the gates], you rulers.
Twekeni bendera juu ya mlima usio na kitu, wapazieni sauti, wapungieni mkono waingie katika malango ya wenye heshima.
3 I give command, and I bring them: giants are coming to fulfil my wrath, rejoicing at the same time and insulting.
Nimewaamuru watakatifu wangu; nimewaita mashujaa wangu waitimize hasira yangu: wale wanaoshangilia ushindi wangu.
4 A voice of many nations on the mountains, [even] like [to that] of many nations; a voice of kings and nations gathered together: the Lord of hosts has given command to a warlike nation,
Sikilizeni kelele juu ya milima, kama ile ya umati mkubwa wa watu! Sikilizeni, makelele katikati ya falme, kama mataifa yanayokusanyika pamoja! Bwana Mwenye Nguvu Zote anakusanya jeshi kwa ajili ya vita.
5 to come from a land afar off, from the utmost foundation of heaven; the Lord and his warriors [are coming] to destroy all the world.
Wanakuja kutoka nchi za mbali sana, kutoka miisho ya mbingu, Bwana na silaha za ghadhabu yake, kuangamiza nchi yote.
6 Howl you, for the day of the Lord is near, and destruction from God shall arrive.
Ombolezeni, kwa maana siku ya Bwana i karibu, itakuja kama uharibifu kutoka kwa Mwenyezi.
7 Therefore every hand shall become powerless, and every soul of man shall be dismayed.
Kwa sababu ya hili, mikono yote italegea, moyo wa kila mtu utayeyuka.
8 The elders shall be troubled, and pangs shall seize them, as of a woman in travail: and they shall mourn one to another, and shall be amazed, and shall change their countenance as a flame.
Hofu itawakamata, uchungu na maumivu makali yatawashika, watagaagaa kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa. Watatazamana kwa hofu kila mtu na mwenzake, nyuso zao zikiwaka kama moto.
9 For behold! the day of the Lord is coming which can’t be escaped, [a day] of wrath and anger, to make the world desolate, and to destroy sinners out of it.
Tazameni, siku ya Bwana inakuja, siku katili, yenye ghadhabu na hasira kali, kuifanya nchi kuwa ukiwa na kuwaangamiza wenye dhambi waliomo ndani yake.
10 For the stars of heaven, and Orion, and all the host of heaven, shall not give their light; and it shall be dark at sunrise, and the moon shall not give her light.
Nyota za mbinguni na makundi ya nyota havitatoa mwanga wake. Jua linalochomoza litatiwa giza na mwezi hautatoa nuru yake.
11 And I will command evils for the whole world, and [will visit] their sins on the ungodly: and I will destroy the pride of transgressors, and will bring low the pride of the haughty.
Nitauadhibu ulimwengu kwa ajili ya uovu wake, waovu kwa ajili ya dhambi zao. Nitakomesha majivuno ya wenye kiburi, na nitakishusha kiburi cha watu wakatili.
12 And they that are left shall be more precious than gold tried in the fire; and a man shall be more precious than the stone that is in Suphir.
Nitawafanya wanadamu kuwa adimu kuliko dhahabu safi, watakuwa wachache sana kuliko dhahabu ya Ofiri.
13 For the heaven shall be enraged, and the earth shall be shaken from her foundation, because of the fierce anger of the Lord of hosts, in the day in which his wrath shall come on.
Kwa hiyo nitazifanya mbingu zitetemeke, nayo dunia itatikisika kutoka mahali pake katika ghadhabu ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika siku ya hasira yake iwakayo.
14 And they that are left shall be as a fleeing fawn, and as a stray sheep, and there shall be none to gather [them]: so that a man shall turn back to his people, and a man shall flee to his own land.
Kama swala awindwaye, kama kondoo wasio na mchungaji, kila mmoja atarudi kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja atakimbilia nchi yake ya kuzaliwa.
15 For whoever shall be taken shall be overcome; and they that are gathered together shall fall by the sword.
Yeyote atakayetekwa atapasuliwa tumbo, wote watakaokamatwa watauawa kwa upanga.
16 And they shall dash their children before their eyes; and they shall spoil their houses, and shall take their wives.
Watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande mbele ya macho yao; nyumba zao zitatekwa na wake zao watatendwa jeuri.
17 Behold, I will stir up against you the Medes, who do not regard silver, neither have they need of gold.
Tazama, nitawachochea Wamedi dhidi yao, ambao hawajali fedha wala hawafurahii dhahabu.
18 They shall break the bows of the young men; and they shall have no mercy on your children; nor shall their eyes spare your children.
Mishale yao itawaangusha vijana, hawatakuwa na huruma kwa watoto wachanga wala hawataangalia watoto kwa huruma.
19 And Babylon, which is called glorious by the king of the Chaldeans, shall be as [when] God overthrew Sodoma, and Gomorrha.
Babeli, johari ya falme, utukufu wa kiburi cha Wababeli, itaangushwa na Mungu kama Sodoma na Gomora.
20 It shall never be inhabited, neither shall any enter into it for many generations: neither shall the Arabians pass through it; nor shall shepherds at all rest in it.
Hautakaliwa na watu kamwe wala watu hawataishi humo kwa vizazi vyote. Hakuna Mwarabu atakayepiga hema lake huko, hakuna mchungaji atakayepumzisha makundi yake huko.
21 But wild beasts shall rest there; and the houses shall be filled with howling; and monsters shall rest there, and devils shall dance there, and satyrs shall dwell there; and hedgehogs shall make their nests in their houses. It will come soon, and will not wait.
Lakini viumbe wa jangwani watalala huko, mbweha watajaza nyumba zake, bundi wataishi humo nao mbuzi-mwitu watarukaruka humo.
Fisi watalia ndani ya ngome zake, mbweha ndani ya majumba yake ya kifahari. Wakati wake umewadia, na siku zake hazitaongezwa.

< Esias 13 >