< 1 Chronicles 27 >

1 Now the children of Israel after their number, [to wit], the chief fathers and captains of thousands and hundreds, and their officers that served the king in any matter of the courses, which came in and went out month by month throughout all the months of the year, of every course [were] twenty and four thousand.
Hii ni orodha ya familia za viongozi wa Israeli, wakuu wa maelfu na mamia, pamoja na maafisa wa jeshi walio mtumikia mfalme kwa namna tofauti. Kila kikosi cha jeshi kilitumika mwenzi hadi mwezi kwa mwaka mzima. Kila kikosi kilikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
2 Over the first course for the first month [was] Jashobeam the son of Zabdiel: and in his course [were] twenty and four thousand.
Kwa mwezi wa kwanza wa kikosi alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
3 Of the children of Perez [was] the chief of all the captains of the host for the first month.
Alikuwa miongoni mwa uzao wa Perezi na mhusika wa maafisa wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
4 And over the course of the second month [was] Dodai an Ahohite, and of his course [was] Mikloth also the ruler: in his course likewise [were] twenty and four thousand.
Juu ya kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai, wa ukoo wa uliotoka kwa Ahoa. Mikilothi alikuwa wa pili kwa cheo. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
5 The third captain of the host for the third month [was] Benaiah the son of Jehoiada, a chief priest: and in his course [were] twenty and four thousand.
Mkuu wa jeshi wa mwezi wa tatu alikuwa Benaia mwana wa Yehoiada, kuhani na kiongozi. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
6 This [is that] Benaiah, [who was] mighty [among] the thirty, and above the thirty: and in his course [was] Ammizabad his son.
Huyu ni Benaia aliye kuwa kiongozi wa wale thelathini na juu ya wale thelathini. Amizabadi mwanae alikuwa katika kikosi chake.
7 The fourth [captain] for the fourth month [was] Asahel the brother of Joab, and Zebadiah his son after him: and in his course [were] twenty and four thousand.
Mkuu kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli kaka wa Yoabu. Zebadia mwanae akawa mkuu baada yake. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
8 The fifth captain for the fifth month [was] Shamhuth the Izrahite: and in his course [were] twenty and four thousand.
Mkuu kwa mwezi wa tano alikuwa Shamihuthi, mzao wa Izra. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
9 The sixth [captain] for the sixth month [was] Ira the son of Ikkesh the Tekoite: and in his course [were] twenty and four thousand.
Mkuu kwa mwezi wa sita alikuwa Ira mwana wa Ikeshi, kutoka Tekoa. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
10 The seventh [captain] for the seventh month [was] Helez the Pelonite, of the children of Ephraim: and in his course [were] twenty and four thousand.
Mkuu kwa mwezi wa saba alikuwa Helezi Mpeloni, kutoka watu wa Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
11 The eighth [captain] for the eighth month [was] Sibbecai the Hushathite, of the Zarhites: and in his course [were] twenty and four thousand.
Mkuu kwa mwezi wa nane alikuwa Sibekai Mhushathi, kutoka ukoo ulitoka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
12 The ninth [captain] for the ninth month [was] Abi-ezer the Anetothite, of the Benjamites: and in his course [were] twenty and four thousand.
Mkuu kwa mwezi wa tisa alikuwa Abi Ezeri Manathothi, kutoka kwa kabila la Benjamini. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
13 The tenth [captain] for the tenth month [was] Maharai the Netophathite, of the Zarhites: and in his course [were] twenty and four thousand.
Mkuu kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai kutoka mji wa Netofa, kutoka ukoo ulio toka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
14 The eleventh [captain] for the eleventh month [was] Benaiah the Pirathonite, of the children of Ephraim: and in his course [were] twenty and four thousand.
Mkuu kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaia kutoka mji wa Pirathoni, kutoka kabila la Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
15 The twelfth [captain] for the twelfth month [was] Heldai the Netophathite, of Othniel: and in his course [were] twenty and four thousand.
Mkuu kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Helidai kutoka mji wa Netopafa, kutoka ukoo uliotoka kwa Othinieli. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
16 Furthermore over the tribes of Israel: the ruler of the Reubenites [was] Eliezer the son of Zichri: of the Simeonites, Shephatiah the son of Maachah:
Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli: Kwa kabila la Rubeni, Eliezeri mwana wa Zikri alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Simeoni, Shefatia mwana wa Maka alikuwa kiongozi.
17 Of the Levites, Hashabiah the son of Kemuel: of the Aaronites, Zadok:
Kwa kabila la Lawi, Hashinia mwana wa Kemueli alikuwa kiongozi, na Zadoki aliongoza uzao wa Aruni.
18 Of Judah, Elihu, [one] of the brethren of David: of Issachar, Omri the son of Michael:
Kwa kabila la Yuda, Elihu, mmoja wa kaka zake Daudi, alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Isakari, Omri mwana wa Mikaeli alikuwa kiongozi.
19 Of Zebulun, Ishmaiah the son of Obadiah: of Naphtali, Jerimoth the son of Azriel:
Kwa kabila la Zebuluni, Ishimaia mwana wa Obadia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Naftali, Yeremothi mwana wa Azirieli alikuwa kiongozi.
20 Of the children of Ephraim, Hoshea the son of Azaziah: of the half tribe of Manasseh, Joel the son of Pedaiah:
Kwa kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Azazia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Manase, Yoeli mwana wa Pedaia alikuwa kiongozi.
21 Of the half [tribe] of Manasseh in Gilead, Iddo the son of Zechariah: of Benjamin, Jaasiel the son of Abner:
Kwa nusu kabila la Manase lililo Gileadi, Ido mwana wa Zekaria alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Benjamini, Yaasieli mwana wa Abneri alikuwa kiongozi.
22 Of Dan, Azareel the son of Jeroham. These [were] the princes of the tribes of Israel.
Kwa kabila la Dani, Azareli mwana wa Yerohamu alikuwa kiongozi. Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli.
23 But David took not the number of them from twenty years old and under: because the LORD had said he would increase Israel like to the stars of the heavens.
Daudi hakuwa hesabu wenye umri wa miaka ishirini au chini zaidi, kwasababu Yahweh alihaidi kuongeza Israeli kama nyota za mbinguni.
24 Joab the son of Zeruiah began to number, but he finished not, because there fell wrath for it against Israel; neither was the number put in the account of the chronicles of king David.
Yoabu mwana wa Zeruia alianza kuhesabu wanaume, lakini hakumaliza. Gadhabu iliangukia Israeli kwa hili. Hii idadi haikuandikwa kwenye nyakati za mfalme Daudi.
25 And over the king’s treasures [was] Azmaveth the son of Adiel: and over the storehouses in the fields, in the cities, and in the villages, and in the castles, [was] Jehonathan the son of Uzziah:
Azimavethi mwana wa Adieli alikuwa mhusika wa hazina za mfalme. Yonathani mwana wa Uzia alikuwa juu ya nyumba za ghala katika mashamba, kwenye miji, na vijijini, na kwenye minara iliyo imarishwa.
26 And over them that did the work of the field for tillage of the ground [was] Ezri the son of Chelub:
Ezri mwana wa Kelubi alikuwa juu ya mashamba, hao walio lima ardhi.
27 And over the vineyards [was] Shimei the Ramathite: over the increase of the vineyards for the wine cellars [was] Zabdi the Shiphmite:
Shimei kutoka Rama alikuwa juu ya mashamba ya mizabibu, na Zabdi kutoka Shefamu alikuwa juu ya mizabibu na mhifadhi wa mvinyo.
28 And over the olive trees and the sycomore trees that [were] in the low plains [was] Baal-hanan the Gederite: and over the cellars of oil [was] Joash:
Mwangalizi wa miti mizeituni na miti ya mikuyu iliyo kuwa bondeni alikuwa Baali Hanani kutoka Gederi, na juu ya nyumba za ghala za mafuta alikuwa Yoashi.
29 And over the herds that fed in Sharon [was] Shitrai the Sharonite: and over the herds [that were] in the valleys [was] Shaphat the son of Adlai:
Juu ya mifugo iliyo kuwa inalishwa huko Sharoni alikuwa Shitrai kutoka Sharoni, na juu ya mifugo iliyo kuwa mabondeni alikuwa Shafati mwana wa Adlai.
30 Over the camels also [was] Obil the Ishmaelite: and over the asses [was] Jehdeiah the Meronothite:
Msimamizi wa ngamia alikuwa Obili Mishimaeli, na juu ya punda wakike alikuwa Yehideia kutoka Meronothi. Juu ya mifugo alikuwa Yazizi Mhagri.
31 And over the flocks [was] Jaziz the Hagerite. All these [were] the rulers of the substance which [was] king David’s.
Hawa wote walikuwa wasimamizi wa mali za Mfalme Daudi.
32 Also Jonathan David’s uncle was a counsellor, a wise man, and a scribe: and Jehiel the son of Hachmoni [was] with the king’s sons:
Yonathani, mjomba wake Daudi alikuwa mshauri, sababu alikuwa na busara na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakimoni aliwajali watoto wa mfalme.
33 And Ahithophel [was] the king’s counsellor: and Hushai the Archite [was] the king’s companion:
Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme, na Hushai kutoka watu wa Waariki alikuwa mshauri wake wa siri.
34 And after Ahithophel [was] Jehoiada the son of Benaiah, and Abiathar: and the general of the king’s army [was] Joab.
Nafasi ya Ahithofeli ilichukuliwa na Yehoiada mwana wa Benaia, na Abiathari. Yoabu alikuwa mkuu wa jeshi la mfalme.

< 1 Chronicles 27 >