< Psalms 83 >

1 Keep not you silence, O God: hold not your peace, and be not still, O God.
Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
2 For, lo, your enemies make a tumult: and they that hate you have lifted up the head.
Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
3 They have taken crafty counsel against your people, and consulted against your hidden ones.
Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
4 They have said, Come, and let us cut them off from being a nation; that the name of Israel may be no more in remembrance.
“Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
5 For they have consulted together with one consent: they are confederate against you:
Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
6 The tabernacles of Edom, and the Ishmaelites; of Moab, and the Hagarenes;
Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
7 Gebal, and Ammon, and Amalek; the Philistines with the inhabitants of Tyre;
Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
8 Assur also is joined with them: they have helped the children of Lot. (Selah)
Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
9 Do unto them as unto the Midianites; as to Sisera, as to Jabin, at the brook of Kison:
Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
10 Which perished at Endor: they became as dung for the earth.
Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
11 Make their nobles like Oreb, and like Zeeb: yea, all their princes as Zebah, and as Zalmunna:
Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
12 Who said, Let us take to ourselves the houses of God in possession.
Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
13 O my God, make them like a wheel; as the stubble before the wind.
Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
14 As the fire burns a wood, and as the flame sets the mountains on fire;
Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
15 So persecute them with your tempest, and make them afraid with your storm.
Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
16 Fill their faces with shame; that they may seek your name, O LORD.
Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
17 Let them be confounded and troubled for ever; yea, let them be put to shame, and perish:
Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
18 That men may know that you, whose name alone is JEHOVAH, are the most high over all the earth.
Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.

< Psalms 83 >