< Psalms 75 >

1 Unto you, O God, do we give thanks, unto you do we give thanks: for that your name is near your wondrous works declare.
Tunatoa shukrani kwako, Mungu; tunatoa shukrani, maana wewe unaufunua uwepo wako; watu huzungumza kuhusu kazi zako za ajabu.
2 When I shall receive the congregation I will judge uprightly.
Kwa wakati maalum nitahukumu kwa haki.
3 The earth and all the inhabitants thereof are dissolved: I bear up the pillars of it. (Selah)
Ingawa nchi na wenyeji wote watatikisika katika hofu, ninaifanyia nchi nguzo za kutosha. (Selah)
4 I said unto the fools, Deal not foolishly: and to the wicked, Lift not up the horn:
Nilisema kwa wenye kiburi, “Msiwe wenye kiburi,” na kwa waovu, “Msiinue mapembe.
5 Lift not up your horn on high: speak not with a stiff neck.
Msiinue mapembe yenu kwenye marefu; wala msizungumze kwa shingo ya kiburi.”
6 For promotion comes neither from the east, nor from the west, nor from the south.
Sio kutoka mashariki au magharibi, na wala sio kutoka jangwani ambako kuinuliwa kunakuja.
7 But God is the judge: he puts down one, and sets up another.
Bali Mungu ni muhumkumu; humshusha huyu na kumuinua huyu.
8 For in the hand of the LORD there is a cup, and the wine is red; it is full of mixture; and he pours out of the same: but the dregs thereof, all the wicked of the earth shall wring them out, and drink them.
Kwa kuwa Yahwe kashikilia mkononi mwake kikombe cha mvinyo wenye povu, ambao umechanganywa na vilolezo, naye huimimina. Hakika waovu wote wa duniani watakunywa mvinyo hadi tone la mwisho.
9 But I will declare for ever; I will sing praises to the God of Jacob.
Bali mimi nitaendelea kusema yale ambayo umeyatenda; nami nitamwimbia sifa Mungu wa Yakobo.
10 All the horns of the wicked also will I cut off; but the horns of the righteous shall be exalted.
Yeye husema, “Nitayakata mapembe yote ya waovu, lakini mapembe ya wenye haki yatainuliwa.”

< Psalms 75 >