< Psalms 73 >

1 Truly God is good to Israel, even to such as are of a clean heart.
Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
2 But as for me, my feet were almost gone; my steps had well nigh slipped.
Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
3 For I was envious at the foolish, when I saw the prosperity of the wicked.
kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
4 For there are no bands in their death: but their strength is firm.
Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
5 They are not in trouble as other men; neither are they plagued like other men.
Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
6 Therefore pride compasses them about as a chain; violence covers them as a garment.
Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
7 Their eyes stand out with fatness: they have more than heart could wish.
Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
8 They are corrupt, and speak wickedly concerning oppression: they speak loftily.
Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
9 They set their mouth against the heavens, and their tongue walks through the earth.
Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
10 Therefore his people return here: and waters of a full cup are wrung out to them.
Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
11 And they say, How does God know? and is there knowledge in the most High?
Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
12 Behold, these are the ungodly, who prosper in the world; they increase in riches.
Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
13 Verily I have cleansed my heart in vain, and washed my hands in innocence.
Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
14 For all the day long have I been plagued, and chastened every morning.
Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
15 If I say, I will speak thus; behold, I should offend against the generation of your children.
Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
16 When I thought to know this, it was too painful for me;
Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
17 Until I went into the sanctuary of God; then understood I their end.
Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
18 Surely you did set them in slippery places: you casted them down into destruction.
Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
19 How are they brought into desolation, as in a moment! they are utterly consumed with terrors.
Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
20 As a dream when one awakes; so, O Lord, when you awake, you shall despise their image.
Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
21 Thus my heart was grieved, and I was pricked in my reins.
Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
22 So foolish was I, and ignorant: I was as a beast before you.
Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
23 Nevertheless I am continually with you: you have held me by my right hand.
Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
24 You shall guide me with your counsel, and afterward receive me to glory.
Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
25 Whom have I in heaven but you? and there is none upon earth that I desire beside you.
Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
26 My flesh and my heart fails: but God is the strength of my heart, and my portion for ever.
Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
27 For, lo, they that are far from you shall perish: you have destroyed all them that go a whoring from you.
Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 But it is good for me to draw near to God: I have put my trust in the Lord GOD, that I may declare all your works.
Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.

< Psalms 73 >