< Psalms 73 >

1 Truly God is good to Israel, even to such as are of a clean heart.
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 But as for me, my feet were almost gone; my steps had well nigh slipped.
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 For I was envious at the foolish, when I saw the prosperity of the wicked.
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 For there are no bands in their death: but their strength is firm.
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5 They are not in trouble as other men; neither are they plagued like other men.
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 Therefore pride compasses them about as a chain; violence covers them as a garment.
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7 Their eyes stand out with fatness: they have more than heart could wish.
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8 They are corrupt, and speak wickedly concerning oppression: they speak loftily.
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9 They set their mouth against the heavens, and their tongue walks through the earth.
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10 Therefore his people return here: and waters of a full cup are wrung out to them.
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11 And they say, How does God know? and is there knowledge in the most High?
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12 Behold, these are the ungodly, who prosper in the world; they increase in riches.
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
13 Verily I have cleansed my heart in vain, and washed my hands in innocence.
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14 For all the day long have I been plagued, and chastened every morning.
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15 If I say, I will speak thus; behold, I should offend against the generation of your children.
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16 When I thought to know this, it was too painful for me;
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17 Until I went into the sanctuary of God; then understood I their end.
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18 Surely you did set them in slippery places: you casted them down into destruction.
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19 How are they brought into desolation, as in a moment! they are utterly consumed with terrors.
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20 As a dream when one awakes; so, O Lord, when you awake, you shall despise their image.
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
21 Thus my heart was grieved, and I was pricked in my reins.
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22 So foolish was I, and ignorant: I was as a beast before you.
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23 Nevertheless I am continually with you: you have held me by my right hand.
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24 You shall guide me with your counsel, and afterward receive me to glory.
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25 Whom have I in heaven but you? and there is none upon earth that I desire beside you.
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26 My flesh and my heart fails: but God is the strength of my heart, and my portion for ever.
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27 For, lo, they that are far from you shall perish: you have destroyed all them that go a whoring from you.
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 But it is good for me to draw near to God: I have put my trust in the Lord GOD, that I may declare all your works.
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.

< Psalms 73 >