< Psalms 64 >

1 Hear my voice, O God, in my prayer: preserve my life from fear of the enemy.
Sikia sauti yangu, Mungu, usikilize malalamiko yangu; unilinde dhidi ya hofu ya adui zangu.
2 Hide me from the secret counsel of the wicked; from the insurrection of the workers of iniquity:
Unifiche dhidi ya mipango ya siri ya wafanyao maovu, unifiche dhidi ya watendao vurugu ya udhalimu.
3 Who sharpen their tongue like a sword, and bend their bows to shoot their arrows, even bitter words:
Wao wamenoa ndimi zao kama panga; wamelenga mishale yao, maneno machungu,
4 That they may shoot in secret at the perfect: suddenly do they shoot at him, and fear not.
ili kwamba waweze kupiga kutoka mahali pa siri kwenda kwa mtu asiye na hatia; wampige yeye kwa ghafla nao wasihofu lolote.
5 They encourage themselves in an evil matter: they commune of laying snares privately; they say, Who shall see them?
Wao wanahamasishana wenyewe katika kupanga uovu; wanashauriana pamoja wao binafsi ili kuweka mitego; nao husema, “Ni nani atakayetuona?”
6 They search out iniquities; they accomplish a diligent search: both the inward thought of every one of them, and the heart, is deep.
Wanabuni mipango ya dhambi; “Tumemaliza,” wanasema, “ni mpango makini.” Mawazo ya ndani na mioyo ya watu ni ya kina.
7 But God shall shoot at them with an arrow; suddenly shall they be wounded.
Lakini Mungu atawapiga wao; ghafla watajeruhiwa kwa mishale yake.
8 So they shall make their own tongue to fall upon themselves: all that see them shall flee away.
Watafanywa kuwa mashakani, kwa kuwa ndimi zao wenyewe ziko kinyume nao; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao.
9 And all men shall fear, and shall declare the work of God; for they shall wisely consider of his doing.
Watu wote wataogopa na kutangaza matendo ya Mungu. Kwa hekima watafikiria kuhusu kile yeye ametenda.
10 The righteous shall be glad in the LORD, and shall trust in him; and all the upright in heart shall glory.
Wenye haki watakuwa na furaha kuhusu Yahwe nao watakimbilia kwake; wote wenye haki moyoni watajivuna katika yeye.

< Psalms 64 >