< Psalms 49 >

1 Hear this, all you people; give ear, all you inhabitants of the world:
Sikieni hili, ninyi watu wote; tegeni masikio, ninyi wenyeji wa dunia,
2 Both low and high, rich and poor, together.
wote walio chini na walio juu, tajiri na masikini wote pamoja.
3 My mouth shall speak of wisdom; and the meditation of my heart shall be of understanding.
Mdomo wangu utazungumza hekima na tafakari ya moyo wangu itakuwa ya uelewa.
4 I will incline mine ear to a parable: I will open my dark saying upon the harp.
Nitaelekeza sikio langu kwenye mfano; nitaanza mfano wangu kwa kinubi.
5 Wherefore should I fear in the days of evil, when the iniquity of my heels shall compass me about?
Kwa nini nilazimike kuziogopa siku za uovu, wakati uovu umenizunguka kwenye visigino vyangu?
6 They that trust in their wealth, and boast themselves in the multitude of their riches;
Kwa nini niwaogope wale wanao amini katika mali zao na kujivuna kuhusu utajiri wao?
7 None of them can by any means redeem his brother, nor give to God a ransom for him:
Ni hakika kuwa hakuna yeyote atakaye muokoa ndugu yake au kumpa Mungu pesa kwa ajili yake,
8 (For the redemption of their soul is precious, and it ceases for ever: )
Kwa maana ukombozi wa uhai wa mtu ni gharama kubwa, na hakuna awezaye kulipa kile tunacho daiwa.
9 That he should still live for ever, and not see corruption.
Hakuna yeyote atakaye ishi milele ili mwili wake usioze.
10 For he sees that wise men die, likewise the fool and the brutish person perish, and leave their wealth to others.
Maana yeye ataona uozo. Watu wenye hekima hufa; wajinga pia huangamia na kuacha mali zao kwa wengine.
11 Their inward thought is, that their houses shall continue for ever, and their dwelling places to all generations; they call their lands after their own names.
Mawazo yao ya ndani ni kuwa familia zao zitaishi milele, na mahali waishipo, kwa vizazi vyote; wanaita ardhi zao kwa majina yao wenyewe.
12 Nevertheless man being in honour abides not: he is like the beasts that perish.
Lakini mtu, kuwa na mali, haimaanishi atabaki hai; kama wanyama walioangamia.
13 This their way is their folly: yet their posterity approve their sayings. (Selah)
Hii ni hatma ya wafanyao ujinga baada ya kufa, .................
14 Like sheep they are laid in the grave; death shall feed on them; and the upright shall have dominion over them in the morning; and their beauty shall consume in the grave from their dwelling. (Sheol h7585)
Kama kondoo wamechaguliwa kwa ajili ya kuzimu na kifo kitakuwa mchungaji wao. Nao watatawaliwa na wenye haki ifikapo asubuhi, na miili yao italiwa kuzimuni, wakiwa hawana afasi ya kuishi kwa ajili yao. (Sheol h7585)
15 But God will redeem my soul from the power of the grave: for he shall receive me. (Selah) (Sheol h7585)
Bali Mungu ataufufua uhai wangu kutoka katika nguvu ya kuzimu; naye atanipokea. (Selah) (Sheol h7585)
16 Be not you afraid when one is made rich, when the glory of his house is increased;
Msifadhaike mtu awapo tajiri, utukufu wa nyumba yake uongezekapo.
17 For when he dies he shall carry nothing away: his glory shall not descend after him.
Maana atakapo kufa hataondoka na chochote; utukufu wake hautamfuata yeye.
18 Though while he lived he blessed his soul: and men will praise you, when you do well to yourself.
Yeye huifurahisha nafsi yake awapo hai na watu hukusifu wewe uishipo maisha yako mwenyewe-
19 He shall go to the generation of his fathers; they shall never see light.
naye atakwenda kwenye ukoo wa baba zake naye kamwe hataiona nuru tena.
20 Man that is in honour, and understands not, is like the beasts that perish.
Yule ambaye ana mali lakini hana ufahamu ni kama wanyama, ambao wataangamia.

< Psalms 49 >