< Psalms 2 >

1 Why do the heathen rage, and the people imagine a vain thing?
Kwa nini mataifa wanafanya dhoruba, kwa nini watu wanafanya njama ambazo zitafeli?
2 The kings of the earth set themselves, and the rulers take counsel together, against the LORD, and against his anointed, saying,
Wafalme wa nchi kwa pamoja hushikilia misimamo yao na watawala kwa pamoja hufanya njama kinyume na Yahwe na kinyume na Masihi, wakisema,
3 Let us break their bands asunder, and cast away their cords from us.
“Ngoja tuzikate pingu walizo tufingia sisi na kuzitupa pingu zao.”
4 He that sits in the heavens shall laugh: the LORD shall have them in derision.
Yeye aketie katika mbingu atacheka kwa dharau mbele yao; Bwana atawadhihaki wao.
5 Then shall he speak unto them in his wrath, and vex them in his sore displeasure.
Kisha ataongea nao katika hasira yake na kuwaogofya kwa gadhabu yake, akisema,
6 Yet have I set my king upon my holy hill of Zion.
“Mimi mwenyewe nilimpaka mafuta mfalme wa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 I will declare the decree: the LORD has said unto me, You are my Son; this day have I begotten you.
Nami nitatangaza amri ya Yahwe. Yeye aliniambia, “wewe ni mwanangu! Leo hii nimekuwa baba yako.
8 Ask of me, and I shall give you the heathen for your inheritance, and the uttermost parts of the earth for your possession.
Uniombe, nami nitakupa wewe taifa kwa ajili ya urithi na mikoa ya nchi iliyo bora kwa ajili ya umiliki wako.
9 You shall break them with a rod of iron; you shall dash them in pieces like a potter's vessel.
Wewe utawavunja wao kwa fimbo ya chuma; kama vile mtungi wa mfinyanzi, wewe utawavunja wao vipande vipande.”
10 Be wise now therefore, O all of you kings: be instructed, all of you judges of the earth.
Hivyo sasa, ninyi wafalme; mchukue tahadhari; mjirekebishe.
11 Serve the LORD with fear, and rejoice with trembling.
Mwabuduni Yahwe kwa hofu na mfurahi mkitetemeka.
12 Kiss the Son, lest he be angry, and all of you perish from the way, when his wrath is kindled but a little. Blessed are all they that put their trust in him.
Mumbusu mwana vinginevyo atawakasirikia, na mtakufa pale pale hasira yake ikiwaka. Ni jinsi gani wamebarikiwa wale wote watafutao usalama ndani yake.

< Psalms 2 >