< Psalms 138 >

1 I will praise you with my whole heart: before the gods will I sing praise unto you.
Nitakushukuru kwa moyo wangu wote; mbele ya miungu nitakuimbia sifa.
2 I will worship toward your holy temple, and praise your name for your loving kindness and for your truth: for you have magnified your word above all your name.
Nitasujundu mbele ya hekalu lako takatifu na kulishukuru jina lako kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na kwa uaminifu wako. Umelifanya muhimu zaidi neno lako na jina lako kuliko kitu chochote.
3 In the day when I cried you answered me, and strengthened me with strength in my soul.
Siku ile niliyo kuita, ulinijibu; ulinitia moyo na kuitia nguvu nafsi yangu.
4 All the kings of the earth shall praise you, O LORD, when they hear the words of your mouth.
Wafalme wote wa nchi watakushukuru wewe, Yahwe, maana watasikia maneno kutoka kinywani mwako.
5 Yea, they shall sing in the ways of the LORD: for great is the glory of the LORD.
Hakika, wataimba kuhusu matendo ya Yahwe, kwa kuwa utukufu wa Yahwe ni mkuu.
6 Though the LORD be high, yet has he respect unto the lowly: but the proud he knows far off.
Maana ingawa Yahwe yuko juu, lakini anawajali wanyenyekevu, lakini hawatambui wenye majivuno.
7 Though I walk in the midst of trouble, you will revive me: you shall stretch forth your hand against the wrath of mine enemies, and your right hand shall save me.
Nijapopita katikati ya hatari, wewe utauhifadhi uhai wangu; utanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, na mkono wako wa kuume utaniokoa.
8 The LORD will perfect that which concerns me: your mercy, O LORD, endures for ever: forsake not the works of your own hands.
Yahwe yuko pamoja nami hadi mwisho; uaminifu wa agano lako, Yahwe, wadumu milele. Usiwaache wale ambao mikono yako imewaumba.

< Psalms 138 >