< Psalms 129 >

1 Many a time have they afflicted me from my youth, may Israel now say:
Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
2 Many a time have they afflicted me from my youth: yet they have not prevailed against me.
wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
3 The plowers plowed upon my back: they made long their furrows.
Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
4 The LORD is righteous: he has cut asunder the cords of the wicked.
Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
5 Let them all be confounded and turned back that hate Zion.
Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
6 Let them be as the grass upon the housetops, which withers before it grows up:
Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
7 Wherewith the mower fills not his hand; nor he that binds sheaves his bosom.
kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
8 Neither do they which go by say, The blessing of the LORD be upon you: we bless you in the name of the LORD.
Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”

< Psalms 129 >