< Psalms 108 >

1 O god, my heart is fixed; I will sing and give praise, even with my glory.
Ee Mungu, moyo wangu u thabiti; nitaimba, naam, nitaimba sifa pia kwa moyo mkuu.
2 Awake, psaltery and harp: I myself will awake early.
Amka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
3 I will praise you, O LORD, among the people: and I will sing praises unto you among the nations.
Nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya watu; nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
4 For your mercy is great above the heavens: and your truth reachs unto the clouds.
Kwa maana uaminifu wa agano lako ni mkuu juu ya mbingu; na uaminifu wako wafika mawinguni.
5 Be you exalted, O God, above the heavens: and your glory above all the earth;
Ee Mungu, uinuliwe, juu ya mbingu, na utukufu wako utukuke juu ya nchi.
6 That your beloved may be delivered: save with your right hand, and answer me.
Ili kwamba wale uwapendao waokolewe, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
7 God has spoken in his holiness; I will rejoice, I will divide Shechem, and mete out the valley of Succoth.
Mungu ameongea katika utakatifu wake; “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na nitalipima bonde la Sukothi.
8 Gilead is mine; Manasseh is mine; Ephraim also is the strength of mine head; Judah is my lawgiver;
Gileadi ni yangu, na manase ni yangu; Ephraimu ni nguvu ya kichwa changu; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
9 Moab is my pot for washing; over Edom will I cast out my shoe; over Philistia will I triumph.
Moabu ni bakuli langu la kunawia; nitatupa kiatu changu juu ya Edomu; nitapaza sauti katika ushindi kwa ajili ya Filisti.
10 Who will bring me into the strong city? who will lead me into Edom?
Ni nani atakaye nipeleka kwenye mji imara? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?”
11 Will not you, O God, who have cast us off? and will not you, O God, go forth with our hosts?
Ee Mungu, sio wewe uliyetukataa? Hauendi vitani na jeshi letu.
12 Give us help from trouble: for vain is the help of man.
Utupe msaada dhidi ya adui yetu, maana msaada wa wanadamu ni bure.
13 Through God we shall do valiantly: for he it is that shall tread down our enemies.
Tutashinda kwa msaada wa Mungu; atawakanyaga kwa adui zetu.

< Psalms 108 >