< Proverbs 6 >

1 My son, if you be guarantor for your friend, if you have stricken your hand with a stranger,
Mwanangu, kama utaweka pesa zako kuwa dhamana kwa mkopo wa jirani yako; kama ukitoa ahadi yako katika mkopo wa mtu usiyemjua,
2 You are snared with the words of your mouth, you are taken with the words of your mouth.
basi umejiwekea mtego mwenyewe na umenaswa kwa maneno ya kinywa chako.
3 Do this now, my son, and deliver yourself, when you are come into the hand of your friend; go, humble yourself, and make sure your friend.
Mwanagu, ukinaswa kwa maneno yako mwenyewe, fanya haya ili kujiokoa, kwa kuwa umeangukia kwenye mikono ya jirani yako; nenda unyenyekee na ufanye shauri mbele ya jirani yako.
4 Give not sleep to your eyes, nor slumber to your eyelids.
Usiruhusu usingizi katika macho yako wala kope za macho yako kusinzia.
5 Deliver yourself as a roe from the hand of the hunter, and as a bird from the hand of the fowler.
Jiokoe mwenyewe kama swala kutoka katika mkono wa mwindaji, kama ndege kutoka katika mkono wa mwinda ndege.
6 Go to the ant, you sluggard; consider her ways, and be wise:
Wewe mtu mvivu, mwangalie mchwa, zitafakari njia zake ili kupata busara.
7 Which having no guide, overseer, or ruler,
Hana akida, afisa au mtawala,
8 Provides her food in the summer, and gathers her food in the harvest.
lakini huandaa chakula chake wakati wa joto na wakati wa mavuno huweka hazina ili kula baadaye.
9 How long will you sleep, O sluggard? when will you arise out of your sleep?
Ewe mtu mvivu, utalala hata lini? Wakati gani utainuka usingizini?”
10 Yet a little sleep, a little slumber, a little folding of the hands to sleep:
Lala kidogo, sizia kidogo, kunja mikono kupumzika kidogo” -
11 So shall your poverty come as one that travels, and your lack as an armed man.
ndipo umasikini wako utakapokujia kama mporaji na uhitaji wako kama askari wa vita.
12 A naughty person, a wicked man, walks with a perverse mouth.
Mtu asiyefaa-mtu mwovu- huishi kwa kauli za udanganyifu wake,
13 He winks with his eyes, he speaks with his feet, he teaches with his fingers;
akipepesa macho yake, akiashilia kwa miguu yake na kusonta kwa videle vyake.
14 Perverseness is in his heart, he devises mischief continually; he sows discord.
Hufanya njama za uovu kwa hila ya moyo wake; daima huchochea faraka.
15 Therefore shall his calamity come suddenly; suddenly shall he be broken without remedy.
Kwa hiyo msiba wake utamkumba kwa ghafula, punde atavunjika vibaya wala hatapona.
16 These six things does the LORD hate: yea, seven are an abomination unto him:
Kuna vitu sita ambavyo Yehova huvichukia, saba ambavyo ni chukizo kwake.
17 A proud look, a lying tongue, and hands that shed innocent blood,
Macho ya mtu mwenye kiburi, ulimi wa uongo, mikono inayomwaga damu ya watu maasumu,
18 An heart that devises wicked imaginations, feet that be swift in running to mischief,
moyo unaobuni njama mbaya, miguu inayokimbilia maovu upesi,
19 A false witness that speaks lies, and he that sows discord among brethren.
shahidi asemaye uongo na apandaye faraka kati ya ndugu.
20 My son, keep your father's commandment, and forsake not the law of your mother:
Mwanangu, itii amri ya baba yako na wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
21 Bind them continually upon your heart, and tie them about your neck.
Uyafunge katika moyo wako siku zote; yafunge kwenye shingo yako.
22 When you go, it shall lead you; when you sleep, it shall keep you; and when you awake, it shall talk with you.
utembeapo, yatakuongoza; ulalapo yatakulinda, na uamkapo yatakufundisha.
23 For the commandment is a lamp; and the law is light; and reproofs of instruction are the way of life:
Maana amri ni taa, na mafundisho ni nuru; kinga za kuadilisha za njia ya uzima.
24 To keep you from the evil woman, from the flattery of the tongue of a strange woman.
Yanakulinda dhidi ya mwanamke malaya, dhidi ya maneno laini ya uzinzi.
25 Lust not after her beauty in your heart; neither let her take you with her eyelids.
Moyoni mwako usiutamani uzuri wake wala usitekwe katika kope zake.
26 For by means of a whorish woman a man is brought to a piece of bread: and the adultress will hunt for the precious life.
Kulala na malaya inaweza kugharimu bei ya kipande cha mkate, lakini mke wa mtu mwingine inagharimu uzima wako wote.
27 Can a man take fire in his bosom, and his clothes not be burned?
Je mtu anaweza kubeba moto katika kifua chake bila kuuguza mavazi yake?
28 Can one go upon hot coals, and his feet not be burned?
Je mtu anaweza kutembea juu ya makaa bila kuchomwa miguu yake?
29 So he that goes in to his neighbour's wife; whosoever touches her shall not be innocent.
Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa jirani yake; yule alalaye na huyo mke hatakosa adhabu.
30 Men do not despise a thief, if he steal to satisfy his soul when he is hungry;
Watu hawawezi kumdharau mwizi kama anaiba ili kukidhi hitaji lake la njaa.
31 But if he be found, he shall restore sevenfold; he shall give all the substance of his house.
Walakini akimatwa, atalipa mara saba ya kile alichoiba; lazima atoe kila kitu cha thamani katika nyumba yake.
32 But whoso commits adultery with a woman lacks understanding: he that does it destroys his own soul.
Mtu anayefanya uzinzi hana akili; hufanya hiyo kwa uharibifu wake mwenyewe.
33 A wound and dishonour shall he get; and his reproach shall not be wiped away.
Anasitahili aibu na majeraha na fedheha yake haiwezi kuondolewa.
34 For jealousy is the rage of a man: therefore he will not spare in the day of vengeance.
Maana vivu humghadhibisha mtu; hatakuwa na huruma wakati wa kulipa kisasi chake.
35 He will not regard any ransom; neither will he rest content, though you give many gifts.
Ujapompa zawadi nyingi, hatakubali mbadala wa kusuruhishwa wala kulipwa.

< Proverbs 6 >