< Numbers 34 >

1 And the LORD spoke unto Moses, saying,
BWANA akanena na Musa akasema,
2 Command the children of Israel, and say unto them, When all of you come into the land of Canaan; (this is the land that shall fall unto you for an inheritance, even the land of Canaan with the coasts thereof: )
“Waamuru watu wa Israeli na uwaambie, 'Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani, nchi ambayo itakuwa mali yenu, nchi ya Kanaani na mipaka yake, mpaka wenu wa kusini utaendelea kutoka nyika ya Sini hadi mpaka wa Edomu.
3 Then your south quarter shall be from the wilderness of Zin along by the coast of Edom, and your south border shall be the utmost coast of the salt sea eastward:
Mwisho wa mpaka wa kusini utakuwa mwisho wa bahari ya chumvi kuelekea mashariki.
4 And your border shall turn from the south to the ascent of Akrabbim, and pass on to Zin: and the going forth thereof shall be from the south to Kadeshbarnea, and shall go on to Hazaraddar, and pass on to Azmon:
Mpaka wenu utageukia kusini kutoka mlima kuelekea Akrabimu na kupitia nyika ya Sini. na kutokea huko utaelelkea kusini mwa Kadeshi Barinea na kuelekea Hazari Adari mpaka Azimoni.
5 And the border shall fetch a compass from Azmon unto the river of Egypt, and the activities out of it shall be at the sea.
Kutoka huko, mpaka utageuka kutoka Azimoni kuelekea kijito cha Misri na kukifuata mpaka baharini.
6 And as for the western border, all of you shall even have the great sea for a border: this shall be your west border.
Mpaka wa Magharibi utakuwa pwani ya bahari kuu. Huu ndio utakuwa mpaka wenuwa Magharibi.
7 And this shall be your north border: from the great sea all of you shall point out for you mount Hor:
Mpaka wenu wa kaskazini utaanzia kwenye bahari kuu hadi Mlima Hori,
8 From mount Hor all of you shall point out your border unto the entrance of Hamath; and the activities out of the border shall be to Zedad:
kisha kutoka Mlima Hori hadi Lebo Hamathi, kisha Zedadi.
9 And the border shall go on to Ziphron, and the activities out of it shall be at Hazarenan: this shall be your north border.
Mpaka utaendelea hadi Zifroni na kuishia Hazari Enani. Huu ndio utakuwa mpaka wenu wa kaskazini.
10 And all of you shall point out your east border from Hazarenan to Shepham:
Kisha mtaweka alama za mpaka wenu wa mashariki ambao utaanzia Hazari Enani kuelekea kusini Shefamu.
11 And the coast shall go down from Shepham to Riblah, on the east side of Ain; and the border shall descend, and shall reach unto the side of the sea of Chinnereth eastward:
Kisha mpaka wa kusini utaendelea kutoka Shefamu hadi Ribla, upande wa masharikia mwa Aini. Mpaka utaedelea upande huo wa mashariki hadi upande wa mashariki wa bahari ya Kinerethi.
12 And the border shall go down to Jordan, and the activities out of it shall be at the salt sea: this shall be your land with the coasts thereof round about.
Kisha mpaka utaendelea kuelekea kusini hadi mto Yorodani na hadi bahari ya chumvi. Hii ndiyo itakuwa nchi yenu, kwa kuifuata mipaka yake yote inayozunguka.'”
13 And Moses commanded the children of Israel, saying, This is the land which all of you shall inherit by lot, which the LORD commanded to give unto the nine tribes, and to the half tribe:
Kisha Musa akawaamuru watu wa Israeli akasema, “Hii ndiyo nchi ambayo mtaipokes kwa kura, ambayo BWANA ameamuru kuwapa wale makabila tisa na nusu.
14 For the tribe of the children of Reuben according to the house of their fathers, and the tribe of the children of Gad according to the house of their fathers, have received their inheritance; and half the tribe of Manasseh have received their inheritance:
Kabila ya uzao wa Reubeni, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na uzao wa kabila la Gadi, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na nusu ya Manase wamepata ardhi yao.
15 The two tribes and the half tribe have received their inheritance on this side Jordan near Jericho eastward, toward the sunrising.
Wale makabila mawili na nusu wameshapata mgawo wao ng'ambo ya mto Yorodani upande wa mashariki, kuelekea kule linakotokea jua.”
16 And the LORD spoke unto Moses, saying,
BWANA akanena na Musa akasema,
17 These are the names of the men which shall divide the land unto you: Eleazar the priest, and Joshua the son of Nun.
“Haya ndiyo majinaya watu watakaoigawa ardhi kwa ajili ya urithi wao: Eliazari kuhani na Joshua mwana wa Nuni.
18 And all of you shall take one prince of every tribe, to divide the land by inheritance.
Mtachagua kiongozi mmoja toka kila kabila ili kuigawa ardhi kwa koo zao.
19 And the names of the men are these: Of the tribe of Judah, Caleb the son of Jephunneh.
Haya ndiyo majina ya wanaume: Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.
20 And of the tribe of the children of Simeon, Shemuel the son of Ammihud.
Kutoka kwenye kabila la uzao wa Simeoni, Shemueli mwana wa Amihudi.
21 Of the tribe of Benjamin, Elidad the son of Chislon.
Kutoka kabila la Benjamini, Elidadi mwana wa Kisloni.
22 And the prince of the tribe of the children of Dan, Bukki the son of Jogli.
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Dani, Buki mwana wa Jogili.
23 The prince of the children of Joseph, for the tribe of the children of Manasseh, Hanniel the son of Ephod.
Kiongozi kutoka uzao wa Yusufu, kwenye kabila la Manase, Hannieli mwana wa Efodi.
24 And the prince of the tribe of the children of Ephraim, Kemuel the son of Shiphtan.
Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Efraimu, Kemueli mwana wa Shiftani.
25 And the prince of the tribe of the children of Zebulun, Elizaphan the son of Parnach.
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Zabuloni, Elizafani mwana wa Parinaki.
26 And the prince of the tribe of the children of Issachar, Paltiel the son of Azzan.
Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Isakari, Palitieli mwana wa Azzani.
27 And the prince of the tribe of the children of Asher, Ahihud the son of Shelomi.
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Asheri, Ahihudi mwana wa Shelomi.
28 And the prince of the tribe of the children of Naphtali, Pedahel the son of Ammihud.
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Naftali, Pedaheli mwana wa Amihudi.”
29 These are they whom the LORD commanded to divide the inheritance unto the children of Israel in the land of Canaan.
BWANA aliwaamuru wanaume hawa kuigawa nchi ya Kanaani na kuwapa kila kabla sehemu yao.

< Numbers 34 >