< Numbers 13 >

1 And the LORD spoke unto Moses, saying,
Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia, “tuma watu waende kuipeleleza nchi ya Kanani, ambayo nimewapa wana wa Israeli.
2 Send you men, that they may search the land of Canaan, which I give unto the children of Israel: of every tribe of their fathers shall all of you send a man, every one a ruler among them.
Tuma mwanamume mmoja kutoka kila jamaa ya kabila. Kila mwanamume awe kiongozi katika kabila lake.”
3 And Moses by the commandment of the LORD sent them from the wilderness of Paran: all those men were heads of the children of Israel.
Musa akawatuma kutoka jangwa la Parani, ili watii amri ya BWANA. Watu wote hao walikuwa viongozi wa watu wa Israeli.
4 And these were their names: of the tribe of Reuben, Shammua the son of Zaccur.
Majina yao yalikuwa haya yafuatayo: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;
5 Of the tribe of Simeon, Shaphat the son of Hori.
Kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;
6 Of the tribe of Judah, Caleb the son of Jephunneh.
Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;
7 Of the tribe of Issachar, Igal the son of Joseph.
Kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yusufu,
8 Of the tribe of Ephraim, Oshea the son of Nun.
Kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
9 Of the tribe of Benjamin, Palti the son of Raphu.
Kutoka kabila la Benjamini, Paliti mwana wa Rafu;
10 Of the tribe of Zebulun, Gaddiel the son of Sodi.
kutoka kabila ya Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi;
11 Of the tribe of Joseph, namely, of the tribe of Manasseh, Gaddi the son of Susi.
kutoka kabila la Yusufu (hiyo inamaanisha kutoka kabila la Manase), Gadi mwana wa Susi;
12 Of the tribe of Dan, Ammiel the son of Gemalli.
kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemalili;
13 Of the tribe of Asher, Sethur the son of Michael.
kutoka kabila Asheri, Setu mwana wa Mikaili;
14 Of the tribe of Naphtali, Nahbi the son of Vophsi.
kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Vofisi;
15 Of the tribe of Gad, Geuel the son of Machi.
kutoka kabila la Gadi, Geuli mwana wa Machi.
16 These are the names of the men which Moses sent to spy out the land. And Moses called Oshea the son of Nun Jehoshua.
Haya ndiyo majina ya wanaume ambao Musa aliwatuma kwenda kuipelelza ile nchi. Musa akamwita Hoshea mwana wa Nuni kwa jina la Joshua.
17 And Moses sent them to spy out the land of Canaan, and said unto them, Get you up this way southward, and go up into the mountain:
Musa akawatuma kwenda kuipeleleza ile nchi ya Kanani. Naye akawaambia, “Mkaanzie Negebu hadi mahali pa milima.
18 And see the land, what it is, and the people that dwells therein, whether they be strong or weak, few or many;
Kaipelelezeni nchi kujua ni nchi ya namna gani. Wachunguzeni watu wake, kama ni watu wenye nguvu au dhaifu, kama ni wachache au ni wengi.
19 And what the land is that they dwell in, whether it be good or bad; and what cities they be that they dwell in, whether in tents, or in strong holds;
Chunguzeni nchi hiyo wanayoishi ni nchi ya namna gani. Ni nzuri au mbaya? Miji yao ikoje? Je iko kama kambi au ni miji yenye ngome?
20 And what the land is, whether it be fat or lean, whether there be wood therein, or not. And be all of you of good courage, and bring of the fruit of the land. Now the time was the time of the first-fruits grapes.
Chunguzeni ni nchi ya namna gani, kama ni njema kwa mazao au la kama kuna miti au hapana. Mwe hodari mkalete sampuli za mazao ya nchi,” Sasa ni muda wa msimu wa malimbuko ya mizabibu.
21 So they went up, and searched the land from the wilderness of Zin unto Rehob, as men come to Hamath.
Kwa hiyo wale wanaume wakaenda kuipeleleza ile nchi kutoka jangwa la Sini mpaka Rehobi, karibu na Lebo Hamati.
22 And they ascended by the south, and came unto Hebron; where Ahiman, Sheshai, and Talmai, the children of Anak, were. (Now Hebron was built seven years before Zoan in Egypt.)
Walienda kutoka Negebu nao wakafika Hebroni. Ahimani, Sheshai, na Talmai, Uzao wa Anaki nao walikuweko, Sasa Hebroni ilikuwa imejengwa miaka saba iliyokuwa imepita kabla ya Zoani wa Misri.
23 And they came unto the brook of Eshcol, and cut down from thence a branch with one cluster of grapes, and they bare it between two upon a staff; and they brought of the pomegranates, and of the figs.
Nao walipofika katika bonde la Eshikoli, walikata matawi ya mizabibu lenye kishada cha zabibu. Na makundi mawili ya wapelelezi wakakibeba kwenye mti. Pia wakaleta makomamanga na mtini.
24 The place was called the brook Eshcol, because of the cluster of grapes which the children of Israel cut down from thence.
Mahali pale paliitwa Eshikoli, kwa sababu ya kishada cha mizabibu ambacho wana wa Israeli walikata kule.
25 And they returned from searching of the land after forty days.
Baada ya siku arobaini, wakarudi kutoka kuipeleleza nchi.
26 And they went and came to Moses, and to Aaron, and to all the congregation of the children of Israel, unto the wilderness of Paran, to Kadesh; and brought back word unto them, and unto all the congregation, and showed them the fruit of the land.
Wakaja kwa Musa, Haruni na kwa watu wote wa Israeli katka jangwa la Parani, kule Kadeshi. Wakaleta taarifa kwao na kwa Waisraeli wote, na kuwaonyesha matunda ya nchi ile.
27 And they told him, and said, We came unto the land where you sent us, and surely it flows with milk and honey; and this is the fruit of it.
Wakamwambia Musa, “Tulifika katika ile nchi uliyotutuma. Kwa hakika ni nchi ya kutiririka maziwa na asali. Na baadhi ya matunda yake ni haya hapa.
28 Nevertheless the people be strong that dwell in the land, and the cities are walled, and very great: and moreover we saw the children of Anak there.
Hata hivyo, watu wanaoishi huko ni wenye nguvu. Miji yao ni mikubwa tena ina maboma. Pia tuliwaona wana wa Anaki huko.
29 The Amalekites dwell in the land of the south: and the Hittites, and the Jebusites, and the Amorites, dwell in the mountains: and the Canaanites dwell by the sea, and by the coast of Jordan.
Waamaleki wanaishi Negebu. Wahiti, Wayebusi, na Waamori nao wanaishi katika milima ya hiyo nchi. Wakanaani wanaishi kando ya bahari na mto Yorodani.”
30 And Caleb stilled the people before Moses, and said, Let us go up at once, and possess it; for we are well able to overcome it.
Kisha Kalebu akawatuliza watu waliokuwa mbele ya Musa, akasema, “Twendeni tukaiteke nyara hiyo nchi, kwa kuwa tuna uhakika wa kuikamata.”
31 But the men that went up with him said, We be not able to go up against the people; for they are stronger than we.
Lakini wale watu waliokuwa wameenda naye walisema, “Hatutaweza kuwashinda hao watu kwa kuwa wao ni hodari kuliko sisi.”
32 And they brought up an evil report of the land which they had searched unto the children of Israel, saying, The land, through which we have gone to search it, is a land that eats up the inhabitants thereof; and all the people that we saw in it are men of a great stature.
Kwa hiyo wakasambaza taarifa za kukatisha tamaa kwa Wana wa Israeli juu ya nchi ile waliyoipeleleza. Walisema, “Ile nchi tuliyoiona ni nchi inayowala watu wake. Watu wote tuliowaona ni watu warefu.
33 And there we saw the giants, the sons of Anak, which come of the giants: and we were in our own sight as grasshoppers, and so we were in their sight.
Kule tuliiona majitu, wana wa uzao wa Anaki, ambao nii uzao wa majitu. Sisi tulionekana kama panzi machoni mwao tulipojilingsnisha nao, hivyo ndivyo tulivyoonekana machoni mwao pia.”

< Numbers 13 >