< Leviticus 18 >

1 And the LORD spoke unto Moses, saying,
Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
2 Speak unto the children of Israel, and say unto them, I am the LORD your God.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
3 After the doings of the land of Egypt, wherein all of you dwelt, shall all of you not do: and after the doings of the land of Canaan, where I bring you, shall all of you not do: neither shall all of you walk in their ordinances.
Msitende mambo ambayo watu wa Misri huyatenda, mahali mlikokuwa mkiishi awali. Na ni lazima msitende mambo yale wanayoyatenda watu wa Kanaani, nchi ambayo ninawapeleka nyinyi. Msifuate desturi zao.
4 All of you shall do my judgments, and keep mine ordinances, to walk therein: I am the LORD your God.
Sheria zangu ndizo mtakazozitenda, na amri zangu ndizo mtakazozishika, kwa sababu Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
5 All of you shall therefore keep my statutes, and my judgments: which if a man do, he shall live in them: I am the LORD.
Kwa hiyo ni lazima mzitunze hukumu zangu na sheria zangu. Ikiwa mtu amezitii, ataishi kwa sababu ya hizo. Mimi Ndimi Yahweh.
6 None of you shall approach to any that is near of kin to him, to uncover their nakedness: I am the LORD.
Pasiwepo kwenu atakayelala na yeyote aliye na uhusiano wa karibu naye. Mimi ndimi Yahweh.
7 The nakedness of your father, or the nakedness of your mother, shall you not uncover: she is your mother; you shall not uncover her nakedness.
Usimfedheheshe baba yako kwa kulala na mama yako. Yeye ni mama yako! Haikupasi kumfedhehesha yeye.
8 The nakedness of your father's wife shall you not uncover: it is your father's nakedness.
Usilale na yeyote wa wake za baba yako; Usimfedheheshe namna hiyo baba yako.
9 The nakedness of your sister, the daughter of your father, or daughter of your mother, whether she be born at home, or born abroad, even their nakedness you shall not uncover.
Usilale na yeyote aliye mmoja miongoni mwa dada zako, ama ni binti ya baba yako au ni binti ya mama yako, ama aliyelelewa nyumbani mwenu au mbali nawe. Usilale na dada zako.
10 The nakedness of your son's daughter, or of your daughter's daughter, even their nakedness you shall not uncover: for theirs is your own nakedness.
Usilale na binti ya mwanao, au binti ya binti yako. Hiyo ingekuwa aibu yako mwenyewe.
11 The nakedness of your father's wife's daughter, begotten of your father, she is your sister, you shall not uncover her nakedness.
Usilale na binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa kwa baba yako, yeye ni dada yako, na usilale naye.
12 You shall not uncover the nakedness of your father's sister: she is your father's near kinswoman.
Usilale na dada ya baba yako. Yeye ni ndugu wa karibu kwa baba yako.
13 You shall not uncover the nakedness of your mother's sister: for she is your mother's near kinswoman.
Usilale na dada ya mama yako. Yeye ni ndugu wa mama yako.
14 You shall not uncover the nakedness of your father's brother, you shall not approach to his wife: she is your aunt.
Usimfedheheshe ndug wa baba yako kwa kulala na mke wake. Usimkaribie kwa kusudi hilo; yeye ni shangazi yako.
15 You shall not uncover the nakedness of your daughter in law: she is your son's wife; you shall not uncover her nakedness.
Usilale na binti- mkwe wako, Yeye ni mke wa mwanao; usilale naye.
16 You shall not uncover the nakedness of your brother's wife: it is your brother's nakedness.
Usilale na mke wa kaka yako; usije ukamfedhesha yeye katika njia hii.
17 You shall not uncover the nakedness of a woman and her daughter, neither shall you take her son's daughter, or her daughter's daughter, to uncover her nakedness; for they are her near kinswomen: it is wickedness.
Usilale na mwanamke kisha na binti yake, au binti wa mwanawe au binti wa binti yake. Hao ni ndugu zake wa karibu, na kulala nao lingekuwa ni uovu.
18 Neither shall you take a wife to her sister, to vex her, to uncover her nakedness, beside the other in her life time.
Usimwoe dada ya mke wako kuwa mke wako wa pili na kulala naye wakati bado mke wako wa kwanza angali hai.
19 Also you shall not approach unto a woman to uncover her nakedness, as long as she is put apart for her uncleanness.
Usilale na mwanamke wakati wake wa hedhi.
20 Moreover you shall not lie carnally with your neighbour's wife, to defile yourself with her.
Yeye ni najisi kwa wakati huo. Usilale na mke wa jilani yako na kujichafua mwenyewe kwake katika njia hii.
21 And you shall not let any of your seed pass through the fire to Molech, neither shall you profane the name of your God: I am the LORD.
Msiwatoe watoto wenu ili kuwapitisha kwenye moto, ili kwamba muwatoe sadaka kwa Moleki, kwa sababu msije mkalinajisi jina la Mungu wenu. Mimi ndimi Yahweh.
22 You shall not lie with mankind, as with womankind: it is abomination.
Usilale na mwanaume mwingine kama ulalavyo na mwanamke. Jambo hili lingekuwa uovu.
23 Neither shall you lie with any beast to defile yourself therewith: neither shall any woman stand before a beast to lie down thereto: it is confusion.
Usilale na myama yeyote na kujitia unajisi kwake. Haimpasi mwanamke kufikiria kulala na mnyama ye yote. Huo ungekuwa upotovu.
24 Defile not all of you yourselves in any of these things: for in all these the nations are defiled which I cast out before you:
Msijichafue wenyewe katika njia hizi, kwa kuwa katika njia hizi mataifa yamechafuliwa, mataifa ambayo Nitayafukuza yatoke kwa ajili yenu.
25 And the land is defiled: therefore I do visit the iniquity thereof upon it, and the land itself vomits out her inhabitants.
Ni kwa sababu nchi imenajisiwa, hivyo niliiadhibu dhambi yao, nayo nchi ikawatapika wakazi wake
26 All of you shall therefore keep my statutes and my judgments, and shall not commit any of these abominations; neither any of your own nation, nor any stranger that sojourns among you:
Kwa hiyo, yawapasa kuzishika amri zangu na maagiza yangu, na msifanye aina yoyote ya mambo haya ya machukizo, wala Mwisraeli mzaliwa au Mgeni aishie miongoni mwenu.
27 (For all these abominations have the men of the land done, which were before you, and the land is defiled; )
Kwa kuwa ni uovu huu ambao watu wametenda, wale ambao waliishi hapa kabla yenu, na sasa nchi imenajisiwa.
28 That the land spew not you out also, when all of you defile it, as it spewed out the nations that were before you.
Kwa hiyo, muwe waangalifu ili kwamba nchi isiwatapike nyinyi baada ya kuwa mmeinajisi, kama ilivyowatapika wale watu waliokuwako kabla yenu.
29 For whosoever shall commit any of these abominations, even the souls that commit them shall be cut off from among their people.
Yeyote anayefanya mambo haya ya kuchukiza, watu wafanyao mambo hayo ya kuchukiza lazima watakatiliwa mbali kutoka miongoni mwa watu wao.
30 Therefore shall all of you keep mine ordinance, that all of you commit not any one of these abominable customs, which were committed before you, and that all of you defile not yourselves therein: I am the LORD your God.
Kw a hiyo inawapasa kuzishika amri zangu na sitende mojawapo ya desturi hizi zenyekuchukiza ambazo zilitendwa hapo kabla yenu, ili msijinajisi wenyewe kwa hizo. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.

< Leviticus 18 >