< Leviticus 11 >

1 And the LORD spoke unto Moses and to Aaron, saying unto them,
Yahweh akazungumza na Musa na Aroni, akasema,
2 Speak unto the children of Israel, saying, These are the beasts which all of you shall eat among all the beasts that are on the earth.
“Sungumzeni na watu wa Israeli muwaambie, 'Hivi ndivyo viumbe vyenye uhai ambavyo mwaweza kula miongoni mwa wanyama walioko juu ya nchi.
3 Whatsoever parts the hoof, and is cloven footed, and chews the cud, among the beasts, that shall all of you eat.
Mnaweza kula mnyama yeyote aliye na kwato zenye kugawanyika na ambaye pia hucheua.
4 Nevertheless these shall all of you not eat of them that chew the cud, or of them that divide the hoof: as the camel, because he chews the cud, but divides not the hoof; he is unclean unto you.
Hata hivyo, kuna baadhi ya wanyama ambao ama hawacheui au hana kwato zilizogawanyika, nanyi msiwale hao, wanyama kama ngamia, kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika. Kwa hiyo ngamia ni najisi kwenu.
5 And the coney, because he chews the cud, but divides not the hoof; he is unclean unto you.
Pimbi pia: kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika mara mbili, huyo pia ni najisi kwenu.
6 And the hare, because he chews the cud, but divides not the hoof; he is unclean unto you.
Na sungura pia: kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika mara mbili, huyu naye ni najisi kwenu.
7 And the swine, though he divide the hoof, and be cloven footed, yet he chews not the cud; he is unclean to you.
Na nguruwe pia: ingawaje yeye anazo kwato zilizogawanyika lakini hacheui, kwa hiyo yeye ni najisi kwenu.
8 Of their flesh shall all of you not eat, and their carcass shall all of you not touch; they are unclean to you.
Msile aina yoyote ya nyama yao, wala msiiguse mizoga yao. Hao ni najisi kwenu.
9 These shall all of you eat of all that are in the waters: whatsoever has fins and scales in the waters, in the seas, and in the rivers, them shall all of you eat.
Nao wanyama waishio majini mnaoweza kuwala ni wale wote walio na mapezi na magamba, iwe waliomo baharini au mitoni.
10 And all that have not fins and scales in the seas, and in the rivers, of all that move in the waters, and of any living thing which is in the waters, they shall be an abomination unto you:
Lakini viumbe wote hai wasio na mapezi na magamba waliomo baharini au mitoni, pamoja na wale waendao majini na viumbe hai waliomo majini —watakuwa chukizo kwenu.
11 They shall be even an abomination unto you; all of you shall not eat of their flesh, but all of you shall have their carcasses in abomination.
Kwa kuwa watakuwa chukizo, msile nyama yao, pia mizoga yao sharti itakuwa chukizo.
12 Whatsoever has no fins nor scales in the waters, that shall be an abomination unto you.
Chochote kisichokuwa na mapezi au magamba kilichomo majini ni lazima kiwe chukizo kwenu.
13 And these are they which all of you shall have in abomination among the fowls; they shall not be eaten, they are an abomination: the eagle, and the vulture, and the buzzard,
Nao ndege mtakaowachukia na msiopaswa kuwala ni hawa wafuatao: tai, furukombe, kipungu,
14 And the vulture, and the kite after his kind;
mwewe mwekundu, aina yoyote ya kipanga,
15 Every raven after his kind;
kila aina ya kunguru,
16 And the owl, and the night hawk, and the cuckoo, and the hawk after his kind,
kiruka-njia, kipasuasanda, Shakwe, na aina yoyote ya mwewe.
17 And the little owl, and the cormorant, and the great owl,
Ni lazima pia bundi mdogo na bundi mkubwa muwaone kuwa chukizo, mnandi,
18 And the swan, and the pelican, and the carrion vulture,
bundi mweupe na mwari,
19 And the stork, the heron after her kind, and the lapwing, and the bat.
korongo na ina zote za koikoi, huduhudi na popo pia.
20 All fowls that creep, going upon all four, shall be an abomination unto you.
Wadudu wote wenye mabawa wanatembea kwa miguu minne kwenu ni machukizo.
21 Yet these may all of you eat of every flying creeping thing that goes upon all four, which have legs above their feet, to leap likewise upon the earth;
Lakini manaweza kula wadudu wenye mabawa wanaotembea kwa miguu minne ya kurukia ardhini yenye vifundo.
22 Even these of them all of you may eat; the locust after his kind, and the bald locust after his kind, and the beetle after his kind, and the grasshopper after his kind.
Na manaweza kula kula aina zote za nzige, senene, parare, au panzi.
23 But all other flying creeping things, which have four feet, shall be an abomination unto you.
Lakini wadudu wote warukao wenye miguu minne ni chulkizo kwenu.
24 And for these all of you shall be unclean: whosoever touches the carcass of them shall be unclean until the even.
Nanyi mtakuwa najisi hata jioni kutokana na wanyama hawa endapo mtagusa mizogo yao.
25 And whosoever bears ought of the carcass of them shall wash his clothes, and be unclean until the even.
Na yeyote atakayeokota mojawapo wa mizoga yao ni lazima atazifua ngua zake naye atakuwa najisi hata jioni.
26 The carcasses of every beast which divides the hoof, and is not cloven footed, nor chews the cud, are unclean unto you: every one that touches them shall be unclean.
Mnyama yeyote ambaye anazo kwato ziliachana ambazo hazikugawanyika kabisa au hacheui huyo ni najisi kwenu. Yeyote awagusaye atakuwa najisi.
27 And whatsoever goes upon his paws, among all manner of beasts that go on all four, those are unclean unto you: whoso touches their carcass shall be unclean until the even.
Mnyama yeyote anayetembea kwa vitanga vyake miongoni mwa wanyama waendao kwa miguu yote minne ni najisi kwenu. Yeyote agusaye mzoga kama huo atakuwa najisi hata jioni.
28 And he that bears the carcass of them shall wash his clothes, and be unclean until the even: they are unclean unto you.
Na yeyote aokotaye mzoga kama huo ni zazima atazifua nguo zake na kuwa najisi hata jioni. Wanyama hawa watakuwa najisi kwenu.
29 These also shall be unclean unto you among the creeping things that creep upon the earth; the weasel, and the mouse, and the tortoise after his kind,
Kuhusiana na wanyama wataambaao juu ya ardhi, hawa ndiyo walio najisi kwenu: kicheche, panya, aina zote za mijusi mikubwa, guruguru,
30 And the ferret, and the chameleon, and the lizard, and the snail, and the mole.
kenge, mijusi ya ukutani, goromoe, na kinyonga.
31 These are unclean to you among all that creep: whosoever does touch them, when they be dead, shall be unclean until the even.
Wanyama hawa wote ambao hutambaa, hawa ndiyo watakuwa najisi kwenu. Yeyote awagusaye atakuwa njisi hata jioni.
32 And upon whatsoever any of them, when they are dead, does fall, it shall be unclean; whether it be any vessel of wood, or raiment, or skin, or sack, whatsoever vessel it be, wherein any work is done, it must be put into water, and it shall be unclean until the even; so it shall be cleansed.
Na iwapo mmoja wao anakufa na kuanguka juu ya chombo, chombo hicho kitakuwa najisi, ama kiwe kimetengenezwa kwa mbao, nguo, ngozi, au gunia. Kiwe chombo cha namna gani na kiwe kwa matumizi gani, ni lazima kitalowekwa katika maji nacho kitakuwa najisi hata jio. Kisha kitakuwa safi.
33 And every earthen vessel, into where any of them falls, whatsoever is in it shall be unclean; and all of you shall break it.
Kwa hiyo kila chungu ambacho mnyama najisi atakiangukia juu yake au ndani yake, chochote kilichomo kwenye chungu hicho kitakuwa najisi, na ni lazima mtakivunja chungu hicho.
34 Of all food which may be eaten, that on which such water comes shall be unclean: and all drink that may be drunk in every such vessel shall be unclean.
Vyakula vyote ambavyo ni safi na kilichuhusiwa kuliwa, lakini kikaingiwa na maji kutoka kwenye chungu najisi kilichoanguka, nacho kitakuwa najisi.
35 And every thing whereupon any part of their carcass falls shall be unclean; whether it be oven, or ranges for pots, they shall be broken down: for they are unclean and shall be unclean unto you.
Na kitu chochote kinachoweza kunywewa kutoka kwenye chungu kama hicho kitakuwa najisi. Kila kitu kitakachoangukiwa juu yake na kipande cha mzoga wa mnyama najisi nacho kitakuwa najisi, ama liwe ni jiko au vyungu vya kupikia. Ni najisi na ni lazima kiwe najisi kwenu.
36 Nevertheless a fountain or pit, wherein there is plenty of water, shall be clean: but that which touches their carcass shall be unclean.
Chemchemi au kisima cha maji ya kunywa yanapokusanyika patabaki kuwa safi iwapo kiumbe najisi kama hicho kitaangukia humo. Lakini ikiwa yeyote anaugusa mzoga wa mnyama aliye najisi uliomo ndani ya maji, yeye atakuwa najisi.
37 And if any part of their carcass fall upon any sowing seed which is to be sown, it shall be clean.
Iwapo sehehemu yoyote ya mzoga wa mnyama aliyenajisi inaangukia juu ya mbegu zozote zilizo kwa ajili ya kupanda. Mbegu hizo zitakuwa bado zingali safi.
38 But if any water be put upon the seed, and any part of their carcass fall thereon, it shall be unclean unto you.
Lakini kama maji yanawekwa juu ya mbegu, na kama sehemu ya mzoga unaangukia juu yake, nazo zitakuwa najisi kwenu.
39 And if any beast, of which all of you may eat, die; he that touches the carcass thereof shall be unclean until the even.
Iwapo mnyama yeyote awezaye kuliwa anakufa, naye yeyote amgusaye atakuwa najisi hata jioni.
40 And he that eats of the carcass of it shall wash his clothes, and be unclean until the even: he also that bears the carcass of it shall wash his clothes, and be unclean until the even.
Na yeyote alaye chochote cha mzoga huo atalazimika kufua nguo zake naye atakuwa anjisi hata jioni. Na yeyote aokotaye mzoga kama huo atafua nguo zake na kuwa najisi hata jioni.
41 And every creeping thing that creeps upon the earth shall be an abomination; it shall not be eaten.
Kila mnyama atambaaye juu ya ardhi atakuwa chukizo; hatakuwa wa kuliwa.
42 Whatsoever goes upon the belly, and whatsoever goes upon all four, or whatsoever has more feet among all creeping things that creep upon the earth, them all of you shall not eat; for they are an abomination.
Chochote kitambaacho kwa kujivuta juu ya tumbo lake, na chochote kitembeacho kwa miguu yake yote minne, au chochote kilicho na miguu mingi—wanyama wote ambao hutambaa juu ya nchi, hawa msiwale, kwa sababu watakuwa machukizo.
43 All of you shall not make yourselves abominable with any creeping thing that creeps, neither shall all of you make yourselves unclean with them, that all of you should be defiled thereby.
Msijinajisi wenyewe kwa kiumbe chochote nnajisi kitaambacho; msijinasi wenyewe kwavyo, ili kwamba msije mkachafuliwa navyo.
44 For I am the LORD your God: all of you shall therefore sanctify yourselves, and all of you shall be holy; for I am holy: neither shall all of you defile yourselves with any manner of creeping thing that creeps upon the earth.
Kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu. Nanyi lazima muwe watakatifu, kwa hiyo na iweni watakatifu, kwa sababu Mimi ni mtakatifu. Haiwapasi kujichafua kwa aina yoyote ya kiendacho juu ya nchi.
45 For I am the LORD that brings you up out of the land of Egypt, to be your God: all of you shall therefore be holy, for I am holy.
Kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh, aliyewaleta ninyi kutoka nchi ya Misri, ili niwe Mungu wenu. Kwa hiyo lazima muwe watakatifu, kwa kuwa Mimi ni mtakatifu.
46 This is the law of the beasts, and of the fowl, and of every living creature that moves in the waters, and of every creature that creeps upon the earth:
Hii ndiyo sheria kuhusu wanyama, ndege, kila kiumbe hai kiendacho majini, na ya kila kiumbe kitambaacho juu ya nchi,
47 To make a difference between the unclean and the clean, and between the beast that may be eaten and the beast that may not be eaten.
kwa jili ya kilie kinachopaswa kutofautishwa kati ya kilicho najisi na kilicho safi, na kati ya vitu vilivyokufa na vilivyo hai ambavyo vyaweza kuliwa na vitu vyenye uihai visivyoweza kuliwa.”

< Leviticus 11 >