< Jonah 2 >

1 Then Jonah prayed unto the LORD his God out of the fish's belly,
Kisha Yona akamwomba Bwana Mungu wake kutoka katika tumbo la samaki.
2 And said, I cried by reason of mine affliction unto the LORD, and he heard me; out of the belly of hell cried I, and you heard my voice. (Sheol h7585)
Akasema, Nimemwita Bwana juu ya shida yangu naye akanijibu; kutoka tumbo la Kuzimu nililia kwa msaada! Uliisikia sauti yangu. (Sheol h7585)
3 For you had cast me into the deep, in the midst of the seas; and the floods compassed me about: all your billows and your waves passed over me.
Ulikuwa umenitupa ndani ya kina, ndani ya moyo wa bahari, na maji yaliyonizunguka; mawimbi yako yote na gharika yalipita juu yangu.
4 Then I said, I am cast out of your sight; yet I will look again toward your holy temple.
Nikasema, 'Nimefukuzwa mbele ya macho yako; lakini nitaangalia tena juu ya hekalu lako takatifu. '
5 The waters compassed me about, even to the soul: the depth closed me round about, the weeds were wrapped about my head.
Maji yalifunika kunizunguka karibu na shingo yangu; kina kilinizunguka; mwani ukakizinga kichwa changu.
6 I went down to the bottoms of the mountains; the earth with her bars was about me for ever: yet have you brought up my life from corruption, O LORD my God.
Nilikwenda chini ya milima; nchi na baa zake zimefungwa juu yangu milele. Lakini wewe umeinua uhai wangu shimoni, Bwana, Mungu wangu!
7 When my soul fainted within me I remembered the LORD: and my prayer came in unto you, into your holy temple.
Wakati nafsi yangu ilipozimia ndani yangu, nikamwita Bwana; basi sala yangu ilikujia, katika hekalu lako takatifu.
8 They that observe lying vanities forsake their own mercy.
Wote ambao huzingatia miungu isiyofaa hukataa uaminifu wako wao wenyewe.
9 But I will sacrifice unto you with the voice of thanksgiving; I will pay that that I have vowed. Salvation is of the LORD.
Lakini mimi, nitakuchinjia kwa sauti ya shukrani; Nitayatimiza yale niliyoapa. Wokovu hutoka kwa Bwana!
10 And the LORD spoke unto the fish, and it vomited out Jonah upon the dry land.
Kisha Bwana akanena na samaki, akamtapika Yona juu ya nchi kavu.

< Jonah 2 >