< Isaiah 32 >

1 Behold, a king shall reign in righteousness, and princes shall rule in judgment.
Tazama, mfalme atatawala kwa haki, wakuu wataongoza kwa haki.
2 And a man shall be as an hiding place from the wind, and a covert from the tempest; as rivers of water in a dry place, as the shadow of a great rock in a weary land.
Kila mmoja atakuwa kama makazi kutoka kwenye upepo na kimbilio kutoka kwenye dhoruba, kama mifereji kwenye sehemu kavu, kama kivuli kwenye mwamba mkubwa katika nchi iliyochoka.
3 And the eyes of them that see shall not be dim, and the ears of them that hear shall hearken.
Halafu macho ya waie wanaoona hayataona giza, na masikio ya wale wanosikia yatasikia vizuri.
4 The heart also of the rash shall understand knowledge, and the tongue of the stammerers shall be ready to speak plainly.
Wenye upele watafikiria kwa makini kwa uelewa wao, na wenye kigugumizi watazungumza dhahiri na kwa urahisi.
5 The vile person shall be no more called liberal, nor the churl said to be bountiful.
Mjinga hataitwa tena muheshimiwa, wala muongo hataitwa mkuu.
6 For the vile person will speak villainy, and his heart will work iniquity, to practice hypocrisy, and to utter error against the LORD, to make empty the soul of the hungry, and he will cause the drink of the thirsty to fail.
Maana mjinga anazungumza ujinga, na moyo wake unapanga maovu na matendo ya wasiomcha Mungu, na anaongea mambo mabaya kuhusu Yahwe. Na anawafanya wenye njaa kuwa tupu na wenye kiu kukosa maji
7 The instruments also of the churl are evil: he devises wicked devices to destroy the poor with lying words, even when the needy speaks right.
Njia ya muongo ni maovu. Anajua kubuni mipango mibaya ya kuwalagai masikini kwa uongo, na hata kama masikini atazungumza ukweli.
8 But the liberal devises liberal things; and by liberal things shall he stand.
Lakini watu wa heshima wanapanga mipango ya kuheshimika; na kwa sabaubau ya matendo ya wenye heshima tuatasimama.
9 Rise up, all of you women that are at ease; hear my voice, all of you careless daughters; give ear unto my speech.
Nyanyukeni juu, enyi wanawake mlio wepesi, na sikilizeni sauti yangu; enyi mabinti msiowangalifu, nisikilizeni mimi.
10 Many days and years shall all of you be troubled, all of you careless women: for the vintage shall fail, the gathering shall not come.
Maana kwa mda mfupi zaidi ya mwaka ujasiri wenu utavunjika, nyie wanawake msiojali, maana mavuno ya zabibu yatakwama, mavuno hayatakuwepo.
11 Tremble, all of you women that are at ease; be troubled, all of you careless ones: strip you, and make you bare, and gird sackcloth upon your loins.
Tetemekeni, enyi wanawake, mliowadhaifu; taabikeni enyi msikuwa wangalifu; ondoeni nguo zenu nzuri mbaki wazi;
12 They shall lament for the teats, for the pleasant fields, for the fruitful vine.
Vaeni nguo za magunia katika viuno vyenu. Ole watakaojichukulia mashamba mazuri, kwa mzabibu ulio zaa sana.
13 Upon the land of my people shall come up thorns and briers; yea, upon all the houses of joy in the joyous city:
Kwenye aridhi ya watu wangu kutamea miiba na mbigiri, hata juu ya nyumba za furaha na mji ulio na shangwe.
14 Because the palaces shall be forsaken; the multitude of the city shall be left; the forts and towers shall be for dens for ever, a joy of wild asses, a pasture of flocks;
Maana jumba litaachwa, mji uliosongamana utakuwa faragha; kilima na mnara vitakuwa mapango daima, furaha ya punda, malisho ya mifugo;
15 Until the spirit be poured upon us from on high, and the wilderness be a fruitful field, and the fruitful field be counted for a forest.
mpaka roho itushukie sisi kutoka juu, na jangwa litakuwa shamba linalozaa, na shamba linalozaa litachukuliwa kama msitu.
16 Then judgment shall dwell in the wilderness, and righteousness remain in the fruitful field.
Wenye haki wataishi jangwani; na wenye haki wataishi katika shamba linalozaa matunda.
17 And the work of righteousness shall be peace; and the effect of righteousness quietness and assurance for ever.
Kazi ya mwenye haki itakuwa ni ya amani; na matokeo ya wenye haki, ni utulivu na kujiamini daima.
18 And my people shall dwell in a peaceable habitation, and in sure dwellings, and in quiet resting places;
Watu wangu wataishi katika makao ya amani, na katika nyumba salama na mahali tulivu pa kupumzikia.
19 When it shall hail, coming down on the forest; and the city shall be low in a low place.
Lakini hata kama ni mvua ya mawe na msitu umeharibiwa, na mji umeteketezwa,
20 Blessed are all of you that sow beside all waters, that send forth thither the feet of the ox and the ass.
yule ambae anaye panda pembezoni mwa mifereji atabarikiwa, na yule atakaye wapeleka ng'ombe na punda kuchunga.

< Isaiah 32 >