< Deuteronomy 27 >

1 And Moses with the elders of Israel commanded the people, saying, Keep all the commandments which I command you this day.
Musa na wazee wa Israeli waliwaamuru watu na kusema, “Zishikeni amri zote ninazowaamuru leo.
2 And it shall be on the day when all of you shall pass over Jordan unto the land which the LORD your God gives you, that you shall set you up great stones, and smear them with plaster:
Katika siku mtakapopita juu ya Yordani kwenye nchi ambayo Yahwe Mungu wako anawapatia, mnapaswa kutengeneza mawe kiasi makubwa na kuyachapa kwa lipu.
3 And you shall write upon them all the words of this law, when you are passed over, that you may go in unto the land which the LORD your God gives you, a land that flows with milk and honey; as the LORD God of your fathers has promised you.
Mnatakiwa kuyaandika juu yake maneno yote ya sheria hii pale mtakapovuka; ili muweze kwenda katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anawapatia, nchi inayotiririka kwa maziwa na asali, kama Yahwe, Mungu wa mababu zenu, alivyowaahidi.
4 Therefore it shall be when all of you be gone over Jordan, that all of you shall set up these stones, which I command you this day, in mount Ebal, and you shall smear them with plaster.
Mtakapovuka juu ya Yordani, yapangane haya mawe ninayowaamuru leo, juu ya mlima wa Ebali, na myapige kwa lipu.
5 And there shall you build an altar unto the LORD your God, an altar of stones: you shall not lift up any iron tool upon them.
Hapo mnapaswa kujenga dhabahu kwa Yahwe Mungu wako, dhabahu la mawe; lakini hautakiwi kuinua chombo cha chuma kujenga mawe.
6 You shall build the altar of the LORD your God of whole stones: and you shall offer burnt offerings thereon unto the LORD your God:
Unatakiwa kujenga dhabahu ya Yahwe Mungu wako kwa mawe yasiyokuwa na kazi; unatakiwa kutoa dhabihu ya kuteketeza juu yake kwa Yahwe Mungu wako,
7 And you shall offer peace offerings, and shall eat there, and rejoice before the LORD your God.
na utatoa sadaka ya pamoja na utakula pale; utafurahia mbele ya Yahwe Mungu wako.
8 And you shall write upon the stones all the words of this law very plainly.
Utaandika juu ya mawe maneno yote ya sheria hii kwa wazi.
9 And Moses and the priests the Levites spoke unto all Israel, saying, Take heed, and hearken, O Israel; this day you are become the people of the LORD your God.
Musa na makuhani, Walawi, waliongea na Waisraeli wote na kusema, “Nyamazeni na sikilizeni Israel: Leo mmekuwa watu wa Yahwe Mungu wenu.
10 You shall therefore obey the voice of the LORD your God, and do his commandments and his statutes, which I command you this day.
Mnapaswa basi kutii sauti ya Yahwe Mungu wenu na kutii amri na sheria zake ambazo ninawaamuru leo.”
11 And Moses charged the people the same day, saying,
Musa aliwaamuru watu siku hiyo hiyo na kusema,
12 These shall stand upon mount Gerizim to bless the people, when all of you are come over Jordan; Simeon, and Levi, and Judah, and Issachar, and Joseph, and Benjamin:
“Makabila haya yanapaswa kusimama katika mlima Gerizimu kuwabariki watu baada ya nyinyi kuvuka Yordani; Simeoni, Lawi, Judah, Isakari, Yusufu na Benyamini.
13 And these shall stand upon mount Ebal to curse; Reuben, Gad, and Asher, and Zebulun, Dan, and Naphtali.
Haya ni makabila ambayo lazima yasimame juu yam lima Ebali kutamka laana: Rubeni, Gadi, Asheri, Zabuloni, Dan na Naftali.
14 And the Levites shall speak, and say unto all the men of Israel with a loud voice,
Walawi watajibu na kusema kwa wanamume wote wa Israeli kwa sauti kubwa:
15 Cursed be the man that makes any graven or molten image, an abomination unto the LORD, the work of the hands of the craftsman, and puts it in a secret place. And all the people shall answer and say, Amen.
“Alaaniwe mwanamume atakayechonga sanamu au kinyago, chukizo kwa Yahwe, kazi ya mikono ya fundi, ambayo ataifanya sirini”. Kisha watu wote wanapaswa kujibu na kusema, ‘Amina’.
16 Cursed be he that sets light by his father or his mother. And all the people shall say, Amen.
Alaaniwe mwanamume atakayemuaibisha baba yake au mama yake. Kisha watu wote waseme, 'Amina'.
17 Cursed be he that removes his neighbour's landmark. And all the people shall say, Amen.
Alaaniwe mwanamume anayetoa alama ya ardhi.' Kisha watu wote na waseme, 'Amina'.
18 Cursed be he that makes the blind to wander out of the way. And all the people shall say, Amen.
Alaaniwe mwanamume asababishae kipofu kutoka nje ya barabara. Kisha watu wote waseme, ‘Amina’.
19 Cursed be he that perverts the judgment of the stranger, fatherless, and widow. And all the people shall say, Amen.
Alaaniwe mwanamume atumiaye nguvu kupokonya haki inayomstahili mgeni, yatima, au mjane. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
20 Cursed be he that lies with his father's wife; because he uncovers his father's skirt. And all the people shall say, Amen.
Alaaniwe mwanamume atakayelala na mke wa baba yake, kwa sababu atakuwa amechukua haki za baba yake’. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
21 Cursed be he that lies with any manner of beast. And all the people shall say, Amen.
Alaaniwe mwanamume atakayelala na aina yoyote ya mnyama’. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
22 Cursed be he that lies with his sister, the daughter of his father, or the daughter of his mother. And all the people shall say, Amen.
Alaaniwe mwanamume atakayelala na dada yake, binti wa baba yake, au binti wa mama yake. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
23 Cursed be he that lies with his mother in law. And all the people shall say, Amen.
Alaaniwe mwanamume atakayelala na mama mkwe’. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
24 Cursed be he that strikes his neighbour secretly. And all the people shall say, Amen.
Alaaniwe mwanamume atakayemuua jirani yake kwa siri’. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
25 Cursed be he that takes reward to slay an innocent person. And all the people shall say, Amen.
Alaaniwe mwanamume apokeaye rushwa kumuua mtu asiye na hatia’. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
26 Cursed be he that confirms not all the words of this law to do them. And all the people shall say, Amen.
Alaaniwe mwanamume asiyethibitisha maneno ya sheria hii, ili kwamba ayatii.’ Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.

< Deuteronomy 27 >