< Amos 8 >

1 Thus has the Lord GOD showed unto me: and behold a basket of summer fruit.
Hiki ndicho ambacho bwana Yahwe amenionyesha. Tazama, kikapu cha matunda ya hari!
2 And he said, Amos, what see you? And I said, A basket of summer fruit. Then said the LORD unto me, The end has come upon my people of Israel; I will not again pass by them any more.
Akasema, “Unaona nini, Amosi?” Nikasema, “Kikapu cha matunda ya hari.” Kisha Yahwe akanambia, “Mwisho umefika kwa watu wangu Israeli; sintowaumiza tena.
3 And the songs of the temple shall be wailings in that day, says the Lord GOD: there shall be many dead bodies in every place; they shall cast them forth with silence.
Nyimbo za kwenye hekalu zitakuwa vilio. Katika siku hiyo-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe. Mizoga itakuwa mingi, katika kila sehemu wataitupa katika ukimya!”
4 Hear this, O all of you that swallow up the needy, even to make the poor of the land to fail,
Lisikilizeni hili, ninyi mkanyagao maskini na kumuondoa fukara wa nchi.
5 Saying, When will the new moon be gone, that we may sell corn? and the sabbath, that we may set forth wheat, making the ephah small, and the shekel great, and falsifying the balances by deceit?
wakisema, “Wakati mwezi mpya utakapoisha, hivyo tunaweza kuuza mazao tena? Wakati siku ya Sabato itakapoisha, ili kwamba tuuze ngano? Tutafanya kipimo kidogo na kuongeza bei, tukidanganya kwa mizani za udanganyifu.
6 That we may buy the poor for silver, and the needy for a pair of shoes; yea, and sell the refuse of the wheat?
Hivi ndivyo ambavyo tunaweza kuuza ngano mbaya, kununua fukara kwa fedha, na masikini kwa jozi moja ya kubadhi.”
7 The LORD has sworn by the excellency of Jacob, Surely I will never forget any of their works.
Yahwe ameapa kwa fahari ya Yakobo, “Hakika sintoweza kusahau kazi zao hata moja.”
8 Shall not the land tremble for this, and every one mourn that dwells therein? and it shall rise up wholly as a flood; and it shall be cast out and drowned, as by the flood of Egypt.
Je nchi haitatetemeka kwa hili, na kila mmoja aishiye kuombolezea? Yote hayo yatainuka kama Mto Naili, nayo itataabika juu na kupwa tena, kama mto wa Misri.
9 And it shall come to pass in that day, says the Lord GOD, that I will cause the sun to go down at noon, and I will darken the earth in the clear day:
“Itakuja siku ambayo -huu ndio usemi wa Bwana Yahwe- kwamba nitafanya jua litue wakati wa mchana, na nitaiweka giza dunia wakati wa mchana.
10 And I will turn your feasts into mourning, and all your songs into lamentation; and I will bring up sackcloth upon all loins, and baldness upon every head; and I will make it as the mourning of an only son, and the end thereof as a bitter day.
Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa maombolezo na nyimbo zenu zote kuwa masikitiko. Nitawafanya wote kuvaa nguo za magunia na kipara juu ya kila kichwa. Nitayafanya haya kama maombolezo kwa mwana pekee, na siku ya uchungu mwisho wake.
11 Behold, the days come, says the Lord GOD, that I will send a famine in the land, not a famine of bread, nor a thirst for water, but of hearing the words of the LORD:
Tazama, siku zinakuja -asema Bwana Yahwe- wakati nitakapoleta njaa katika nchi, sio njaa ya mkate, wala kiu ya maji, ila kusikia maneno ya Yahwe.
12 And they shall wander from sea to sea, and from the north even to the east, they shall run back and forth to seek the word of the LORD, and shall not find it.
watatangatanga kutoka bahari hata bahari; watakimbia kutoka kaskazini kwenda magharibi kutafuta neno la Yahwe, lakini hawatalipata.
13 In that day shall the fair virgins and young men faint for thirst.
Katika siku hiyo wanawali wazuri na wavulana watazimia kutokana na njaa.
14 They that swear by the sin of Samaria, and say, Your god, O Dan, lives; and, The manner of Beersheba lives; even they shall fall, and never rise up again.
Wale waapao kwa dhambi ya Samaria wataanguka na hawatainuka tena.”

< Amos 8 >